MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara,
Abdulrahman Kinana, amewahakikishia wananchi wilayani Hanang Mkoa wa
Manyara hususan waliokumbwa na janga la mafuriko, kwamba maelekezo ya
Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, yatatekelezwa kikamilifu na idara na
taasisi zote kama walivyoagizwa chini ya usimamizi wa Waziri Mkuu
Kinana
ameyasema hayo leo Desemba 4, 2023 alipowatembelea waathirika wa
mafuriko hayo katika baadhi ya vijiji vya Wilaya ya Hanang.
Kinana
amewatembelea na kuwafariji wananchi waliopoteza ndugu zao na
waliojeruhiwa na kulazwa hopitalini kutokana na janga hilo ambapo
amewapa pole na kuwaomba wawe na subira katika kipindi hiki kigumu
wanachopitia.
No comments:
Post a Comment