*Kutumia Tsh 40 Milioni Kuboresha Elimu katika Wilaya ya Mwanga
Taasisi
ya kifedha ya Bayport Tanzania imetoa msaada wa wa kompyuta 30 kwa
Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro kama sehemu ya mkakati wake wa
Utawala wa Kijamii na Mazingira (ESG) kuboresha elimu katika shule za
Tanzania ukiweka msisitizo mkubwa katika kuthamini elimu kupitia
teknolojia.
Hafla ya makabidhiano ilifanyika katika shule za sekondari za Kighare na Kamwala za Mwanga mkoani humo.
Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Bayport, Bwana John Mbaga alisema katika hafla hiyo
wilayani humo jana kuwa, Bayport inaamini kila mtoto anastahili kupata
elimu bora, kwani elimu na teknolojia zina jukumu muhimu katika
kuwezesha hilo.
"Kupitia
jitihada zetu za ESG, tumedhamiria kuziba pengo la miundombinu katika
shule nchini Tanzania na kuwawezesha kizazi kijacho kwa zana
zinazohitaji katika mafanikio yao."
Katika
jitihada hii, Bayport imeungana na Airtel Tanzania na Taasisi ya Elimu
ya Tanzania na kupitia ushirikiano huu, Airtel itatoa huduma ya intaneti
bure, wakati Taasisi ya Elimu ya Tanzania itasambaza moduli ya
kujifunza kwa njia ya kidigitali.
Upande
wake, Bwana Christian Mtavanga, Msimamizi Mkuu wa Mfumo katika Taasisi
ya Elimu ya Tanzania, alisema kwamba aina hii ya moduli inajumuisha
masomo mbalimbali na mitihani ya iliyopita inayopatikana mtandaoni,
kuhakikisha uzoefu wa kujifunza bila vikwazo kwa wanafunzi.
Kwa
kuongeza, Afisa Mwedeshaji Mkuu wa Bayport, Bwana Nderingo Materu,
alisema, "Ushirikiano huu unadhihirisha nguvu ya ushirikiano sekta
binafsi katika kuleta matokeo chanya katika elimu. Bayport imetoa
kompyuta 30, viti na meza 30, spika, na televisheni ya inchi 65 yenye
thamani ya Tsh 40 milioni.
"Kwa
kuunganisha rasilimali na utaalamu, Bayport Financial Services na
washirika wake wanajenga mazingira ambapo kujifunza kwa kutumia
teknolojia kunaweza kustawi," alisema Afisa Mtendaji Mkuu wa Bayport.
Tukio
hilo lilihudhuriwa na wawakilishi kutoka Bayport, Balozi wa Bayport,
Bwana Haji Manara, Taasisi ya Elimu ya Tanzania, na uongozi wa shule za
Kamwala na Kighare.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bayport, Bwana John Mbaga (kushoto) akikabidhi sehemu ya msaada wa kompyuta 30 kwa Diwani wa Kata ya Kighare, Bwana. Bwana Innocent Mshemo, zilizotolewa na kampuni hiyo kama sehemu ya mkakati wake wa Utawala wa Kijamii na Mazingira (ESG) kuboresha elimu katika shule za Tanzania. Hafla hiyo fupi ilifanyika katika shule za sekondari za Kighare na Kamwala za Mwanga, mkoani Kilimanjaro jana
No comments:
Post a Comment