Kanyandabila ameyatoa maelekezo hayo leo Septemba 18, 2023 wakati wa Ziara fupi ya Timu ya Menejimenti ya Halmashauri (CMT) ya kukagua hali ya usafi katika viunga vya Manispaa ya Tabora.
Aidha Ndugu Kayandabila ameunda timu ndogo itakayoshirikiana na Kitengo cha Taka Ngumu katika kuratibu na kusimamia kazi zote za usafi mjini hapo, lengo kubwa ikiwa ni kuongeza ufanisi wa shughuli za usafi katika Manispaa yetu.
Wajumbe wa CMT nao baada ya kujionea hali mbaya katika maeneo ya kukusanyia taka, wameafiki kwa pamoja umuhimu wa timu hiyo ndogo ambayo itaongeza nguvu kwenye kitengo cha taka ngumu.
.jpeg)

.jpeg)



No comments:
Post a Comment