Taasisi na makampuni wateja
wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) mkoani Arusha, wameipongeza benki
hiyo kwa kuwapelekea huduma ya malipo kidigitali inayojulikana kama NBC
Connect inayosaidia kuokoa muda na kuongeza ufanisi.
Baadhi ya
wateja walioalikwa katika uzinduzi wa huduma hiyo mkoani Arusha walisema
NBC connect itaziwezesha taasisi zao kufanya malipo kwa njia ya
usalama na bila kulazimika kufika kwenye matawi ya benki jambo ambalo
litasaidia kuokoa muda.
NBC Connect, ni huduma ya kisasa ya
kidigitali kwa makampuni na taasisi mbali mbali, ambayo huwezesha huduma
salama za kibenki kufanyika sehemu yoyote, muda wowote kwa njia ya
mtandao.
Joseph Buko
kutoka kampuni ya Rhotia Valley alisema pamoja na kusaidia kuokoa muda,
mfumo huo wa malipo kidigitali utaongeza ufanisi kwa kuwa unaruhusu
kufanya miamala mingi kwa wakati mmoja na kwa ufanisi.
“Tunaishukuru
benki ya NBC kwa kutulea huduma hii nzuri. Kulingana na mawasilisho yao
kwetu, ni wazi kuwa itatusaidia sana kuokoa muda na muhimu zaidi,
kuongeza ufanisi katika shughuli zetu za kila siku,” alisema
Mteja
mwingine aliyejitambulisha kama Yusuoh Zege kutoka University of
Arusha aliishukuru benki ya NBC kwa kuja na huduma hiyo ya kibunifu na
kuongeza kuwa inaonyesha namna ambavyo benki hiyo inawafikiria na
kuwajali wateja wake ambao ni taasisi binafsi na za serikali.
Akiongea
wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi wa wateja wakubwa Bw. James Metairon
alisema, "Tunafuraha kutambulisha NBC Connect kwa wakazi wa Arusha.
Mfumo huu wa kibenki wa kidigitali ni uthibitisho wa dhamira ya
kuwapatia wateja wetu huduma bora za kibenki ambazo ni rahisi, salama,
na kukidhi mahitaji yao. NBC Connect itawawezesha wateja wetu wenye
makampuni na taasisi mbali mbali kufanya huduma za kibenki popote pale,
wakati wowote, na kufurahia huduma hizo bila matatizo."
Pamoja
na huduma rahisi na za kisasa, NBC Connect itatoa usaidizi binafsi kwa
wateja kupitia kituo chake cha huduma kwa wateja ambapo mameneja wetu
wanapatikana ili kuwasaidia wateja kulingana na mahitaji yao nakutoa
mwongozo wa jinsi ya kutumia huduma hilo kwa ufanisi.
"Tunawaalika
wateja wetu wote wa Arusha wajionee urahisi na usalama wa NBC Connect.
Ni huduma ambayo inaleta mapinduzi mapya kwenye namna ambavyo huduma za
kibenki zinatolewa. Tuna uhakika kuwa wateja wetu watafaidika nayo kwa
kiasi kikubwa , "aliongeza
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo
Katibu msaidizi Tawala Mkoa wa Arusha Ndugu David Lyamongi aliishukuru
Benki ya NBC kwa ubunifu wao mzuri na kuwahimiza wateja kutumia mfumo
huo mpya wa kibenki ili kurahisisha shughuli zao za kibenki.
“Uzinduzi
wa NBC Connect Arusha unawakilisha mpango mkakati wa upanuzi wa benki
ya NBC ili kufikia taasisi mbali mbali na kuchangia ukuaji wa uchumi wa
nchi.
Benki ya NBC inasifika kwa dhamira yake ya kuwajibika kwa
jamii, ikiwa ni pamoja na kusaidia jamii kupitia mipango mbalimbali,
kama vile Mbio za Kimataifa za NBC Dodoma Marathon zinazohamasisha
matibabu ya saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake, msaada wa afya ya
uzazi kupitia kliniki zinazotembea, programu za elimu ya kifedha,
uwezeshaji wa vijana. kupitia udhamini wa Ligi Kuu ya NBC, hakika
napongeza juhudi hizi zinazofanywa na NBC” alisema.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia uzinduzi wa huduma ya NBC Connect inayowezesha kufanya miamala kwa urahisi kwa njia ya kidigitali. Hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo ilifanyika jijini Arusha.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa huduma ya NBC Connect,Naibu Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha David Lyamongi (watatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa benki ya NBC na baadhi ya wateja walioalikwa kwenye uzinduzi wa huduma ya NBC Connect inayowezesha kufanya miamala kwa urahisi kwa njia ya kidigitali. Hafla hiyo imefanyika jijini Arusha.
No comments:
Post a Comment