Dar es Salaam: CERA Sanitaryware, chapa inayokua kwa kasi imezinduliwa kwenye hoteli ya
Ramada Encore jijini Dar es salaam hivi karibuni. CERA inashirikiana na Imports International(T)Ltd (IIL), wadau wao
nchini kwa ajili ya usambazaji, huduma kwa wateja na kujenga chapa ya CERA nchini Tanzania.
Imports International (T) Ltd –IIL – imebobea na inajulikana kwa kuleta mafanikio makubwa
katika kuwakilisha bidhaa za kifahari za kimataifa hapa nchini kupitia maadili mazuri ya ufanyaji
biashara na huduma bora kwa wateja.
Mkurugenzi Mkuu wa IIL Bw. Trushal Jethwa ni mtu mwenye maono mazuri na ana dhamira ya
dhati ya kutoa mchango mkubwa kuboresha ufanisi katika sekta ya ujenzi kwa kuleta bidhaa
bora zinazokidhi viwango vya kimataifa, nchini Tanzania. Tokea mwaka 2004, IIL imejikita katika
usambazaji wa bidhaa bora zinazofaamika kimatafika kutoka Makampuni mbalimbali duniani
kama Saint Gobain, Gyproc, Weber, ISOVER, Insutech n.k.
Cera Sanitaryware Limited, kampuniya vifaa vya bafuni inayokua kwa kasi India, imekuwa
mstari wa mbele katika ubunifu tangu uanzilishi wake manmo mwaka 1980. CERA imeweza
kunyakua tunzo mbalimbali kwenye sekta ya ujenzi. Pia, imefanikiwa kushinda tunzo ya “Bidhaa
Bora Ya Mwaka” kwa miaka 4 mfululizo katika maudhui ya ubunifu. Sio hivyo tu, CERA
imetunukiwa “Chapa Inayoaminika na wateja” katika utafiti uliofanywa na gazeti la Reader’s
Digest. Katika soko la Indiam wateja wameitunuku CERA na tunzo ya “Power Brand” .
Kampuni
ya CERA inahesabika kati ya chapa kubwa za bara la Asia. CERA pia ipo kati ya chapa 100 zenye
tuzo ya “Architecture & Design”. Pamoja na hayo, CERA pia inajulikana kwa teknolojia ya
“green”, ambayo inajali mazingira, katika utengenezaji wa bidhaa zao zote. Ina mkusanyiko
kubwa ya bidhaa zinatomia matumizi madogo ya maji. Kampuni ya CERA ina uwepo katika nchi
38, ndani ya mabara 4, na hakika hii huifanya kuwa kampuni ya kimataifa inayofikia kila
kiwango kilichwekwa kwa ajili ya vifaa vya bafuni.
Bw. Dilip Thakkar, Meneja Mkuu (Export) wa Cera Sanitaryware Limited alikuwepo kwenye
uzinduzi huo kukutana na wasanifu, washauri, wadau wa ujenzi. Alielieza kuhusu maono yake
ya chapa ya CERA barani Africa – hasa nchini Tanzania. Aliongelea pia kuhusu kufungua
showroom ya CERA katika jengo kuu la IIL iliyopo barabara ya Nelson Mandela karibu na
Wiazara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambayo itakua suluhisho la wateja wote na kuongeza
matarajio ya watanzania kujipatia mabafu yenye ubora zaidi.
Bidhaa zote za CERA, yaani vyoo
na bafu, mabomba, vigae, mabeseni ya kunawia n.k. vitakuwepo kwenye showroom ambayo
itafunguliwa saa 3 asubuhi hadi saa 11 na nusu jioni kutoka Jumatatu hadi Ijumaa and saa 3 na
nusu asubuhi hadi saa 8 na nusu mchana kwa siku ya Jumamosi.
Kwenye tukio hili, Bw. Zaheer ambaye ni meneja wa CERA Tanzania na soko la Afrika, alishukuru
wageni wote waliokuwepo na kuahidi kwamba yeye na timu yake watahakikisha wateja wote
wataridhika kwa 100% na bidhaa zote za CERA.
No comments:
Post a Comment