JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


UINGEREZA KUSAIDIA UFIKIWAJI WA HAKI NCHINI.

Share This
Mshauri wa Makosa ya Jinai kutoka Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania Bw. Andy Stephens (aliyesimama) akizungumza  katika mkutano aliofanya na Wanasheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria kuhusu namna nchi yake itakavyoshirikiana na Tanzania katika kuboresha utoaji wa haki nchini hasa katika maeneo ya upelelezi, uendeshaji wa mashtaka na utoaji haki katika Mahakama zetu. Mazungumzo hayo yamefanyika leo (24/3/2016) katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Katiba na Sheria.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (aliyeweka mkono kichwani) akimsikiliza kwa makini Mshauri wa Makosa ya Jinai kutoka Ubalozi wa Uingereza Bw. Andy Stephens (aliyesimama) alipokuwa akizungumza kwenye kikao na Wanasheria wa Wizara ya Katiba na Sheria kuhusu nchi ya Uingereza itakavyoshirikiana na Tanzania katika kuboresha utoaji haki nchini hasa kwenye Mahakama za Tanzania. Kikao hicho kimefanyika leo (24/3/2016) katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Katiba na Sheria.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad