JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TWAWEZA, IBM NA BITES & BYTES WAANDAA MKUTANO WA KITEKNOLOJIA MACHI 29 NA 30 MWAKA HUU.

Share This

TWAWEZA, IBM NA BITES & BYTES WAANDAA MKUTANO WA KITEKNOLOJIA MACHI 29 NA 30 MWAKA HUU.

Mwanzilishi wa Bites& Bytes, Lilian Madeje (Kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na shindano la kiteknologia litakalofanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam Machi 29 na 30 mwaka huu. Kulia ni Mkuu wa Utafiti Twaweza, Elivis Mushi.
NBV wa benki ya CBA Group, Eric Luyangi(Katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kutoka kushoto ni Risha Chande, mwanzilishi wa Bites &Bytes, Lilian Madeje na wamwisho kulia ni
Mkuu wa Utafiti Twaweza, Elivis Mushi.

ASASI isiyo ya kiraia ya Twaweza na Kampuni ya IBM ikishirikiana na Bites &Bytes imeandaa mkutano mkubwa wa Kiteknolojia na uvumbuzi unaoitwa Bites &Bytes ambao utafanyika Machi 29 na 30 mwaka huu katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa na mwanzilishi wa Bites &Bytes, Lilian Madeje wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.

Liliani amesema kuwa lengo mkutano huo ni kuhamasisha uendelezaji wa mawazo mpya pamoja na uvumbuzi wa mawazo mapya ya kibiashara ili aanzishaji wapya wa mawazo waweze kuwapa mwanya wa kubadilishana mawazo na wadau wengine ili waweze kushirikiana kwa pamoja.

Pia Liliani amesema kuwa washiriki 16 wa mechanguliwa kushiriki katika shindano hilo la ubunifu wa biashara ambapo washiriki hao watashindania kuwania kitika cha shilingi milioni tano(5,000,000).

Nae NBV wa benki ya CBA Group, Eric Luyangi amesema kuwa katika shindano hilo la Software Developers wanalenga kuleta suluhisho la kuwezesha kufikisha takwimu na tafiti mbalimbali za Twaweza kwa kutumia mitandao tofauti tofauti.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad