JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


UFAFANUZI MUHIMU KUHUSU MATUMIZI YA NAPHTA

Share This
KUMEKUWA na hoja iliyowasilishwa na mtu mmoja kwenye mitandao ya kijamii kuhusu matumizi ya NAPTHA kwa kurusharusha mwanga kidogo kwa uzalishaji wa hii NAPTHA.

 NAPTHA huzalishwa kwa wingi kutokana na usafishaji mafuta ghafi (crude oil) ambapo, crude oil hutiwa katika kinu cha moto au joto kali inayopelekea kuzalisha mafuta na gesi tofauti katika layers tofauti.

Layers hizi hutofautisha mafuta na gesi tofauti yaani PETROL, KEROSENE (mafuta ya taa) na DIESEL mpaka chini kabisa kunapatikana LAMI.

Hali kadhalika gesi aina tofauti kama butane, propane, nakadhalika hupatikana hapa, nivyema pia  na kuwajuza Watanzania kuwa hii gesi ya kupikia majumbani, iitwayo Liquefid Petroleum Gas au LPG, inayosambazwa katika mitungi kama ORYX, MIHAN, CAM GAS, LAKE GAS nakadhalika hutokana na mchanganyiko wa PROPANE NA BUTANE kupata LPG. 

Huingizwa nchini kutoka nchi zinazozalisha mafuta na kusambazwa hapa nchini katika mitungi ya gesi ya kilo 3, 6, 15, 38, na hadi mitungi mikubwa ya kilo 500, 1000 nakadhalika.

Sasa tofauti za mafuta haya huja kwenye parameters tofauti kama boiling points, flammability rates, viscocity, density nakadhalika nakadhalika.
Refineries tofauti duniani huenda wakazalisha bidhaa Fulani na Fulani zaidi kulingana na mikakati yao , mfano huenda akaseti kupata petro zaidi.

Ama ikirudi kwenye NAPTHA, hii imeegemea zaidi katika PETROLI na tofauti zinakuja kwenye parameters kama ilivyitajwa hapo juu. 

Kutoka uchimbaji wa mafuta ghafi (crude oil) na usafishaji wa mafuta yaani petroleum refinery, ifahamike kwa Watanzania refinery tuliyokuwa nayo ya TIPER ambayo kwa leo ni mali ya kampuni ya ORYX. Refinery hii ilitumika miaka ya nyuma kusafisha mafuta, kwa maana mafuta ghafi yaliingizwa nchini, na uzalishaji au usafishaji wa mafuta kama nilivyoeleza awali ulifanyika hapa nchini. Refinery hii ilikufa kifo cha mende, ingawaje ki uchumi ilikuwa na faida.
                                                                                          
Katika uchimbaji wa NATURAL GAS, pia hupitia hatua kama ya hapo juu, ila hapa huingizwa kwenye mtungi mkubwa kwanza wa High Pressure Separator, ambapo GAS ASILIA huchujwa, ikielea juu kwa sababu ya wepesi wake (density), na chini yake kubaki CONDENSATE. 

Hii condensate, hukamuliwa maji (water) na kutolewa na ilibaki kuingizwa tena katika Low Pressure Separator. Hali kadhalika hupatikana maji na mabaki kuwa aina tofauti za kinachofanana na mafuta ghafi, Zao hili sasa, huwekwa katika treatment tofauti kupata kitu gani mzalishaji anataka….ambapo, pamoja na mengineyo hupatikana NAPTHA.
Hii NAPTHA sasa hupitia pia michakato tofauti kama vile kuiondolea sulfur na treatments nyinginezo zinazoweza kukupatia PETROL.
Vile vile, kutokana na NAPTHA, tunaweza pata SOLVENTS, sabuni za maji au cleaning fluids, diluents (nimekosa neno la Kiswahili hapa) za rangi, varnish, asphalt, pamoja na bidhaa kama solvents katika makampuni ya mpira (rubber) , viberiti vya gesi, hata mali ghafi katika dry cleaners na kutengeneza mbolea.
Sasa basi, Watanzania tunapotezwa sana katika propaganda kuliko kuelewa vitu, na kuchangamkia Fursa Kuliko kumshambulia OILCOM, hapa naona fursa nyingi, nyingi, na nyingi ambazo OILCOM aliona baadhi, na sio kwa U-HASI BALI KWA U- CHANYA.
Zipo sheria za OSHA zinazosimamia athari au maelekezo ya viwango vya matumizi ya NAPTHA. Na sheria nyingine nyingi katika hili.

TPDC ilitengaza tenda ya kuuza CONDESATE. Wadau mbalimbali waliomba na aliyeshinda akapewa. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad