JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


BARAZA LA WATOTO RUANGWA LAPATA VIONGOZI.

Share This

Mwandishi wetu Lindi
BARAZA la watoto mkoani  Mkoani Lindi  limefanya uchaguzi wa Viongozi wataliongoza  kwa muda wa miaka miwili kuanzia mwaka 2016 hadi 2018 baada ya   viongozi waliokuwapo madarakani kumaliza muda wake kwa mujibu wa katiba.

Uchaguzi huo umefanyika katika ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa  
 Uliofadhiliwa na  shirika lisilo la kiserikali la Save the Children International  ambapo nafasi zilizogombewa ni pamoja na  Mwenyekiti,Makamu Mwenyekiti,Katibu,Katibu Msaidizi  Mtunza Hazina wajumbe kamati ya utendaji na  kundi maalumu.

 Msimamizi wa uchaguzi  Afisa maendeleo mkoa Lindi, Anna Maro alimtangaza Aziza Ahmad   kutoka wilaya Ruangwa kuwa Mwenyekiti  baada ya kupata  kura 9 na kuwashinda wapizani  wake Salamu Mwinja kutokaWilaya Kilwa aliyepata kura 6 na siwafu mpende kutoka Lindi aliyepata kura 5 huku Nafasi ya Makamu Mwenyekiti ikichukuliwa na Shaibu Peleu  kutoka wilaya Liwale badaa ya kupata kura 8 kati ya 18 zilizopigwa na kuwaacha wapizani  wake  wa wili  wakigawanya kura sita sita kila moja.

 Nafasi ya Katibu wa baraza hilo  ilichukuliwa na Abdul Selema kutoka wilaya ya kilwa  ambaye alipata kura 13 baada ya kumshinda mpizani wake Saidi Mohamedi kutoka Lindi mjini aliyepata kura 7 na  Katibu Msaidizi alipata  Swaumu Juma  aliyepata  kura 8 kati ya kura zote zilizopigwa.

Anna maro  alimtangaza Sadamu Hamidu kutoka Kilwa  kuwa Mhazini wa baraza hilo ambaye alipata kura 9 wakati Siwatu mpende  kutoka Lindi Mjini alipata nafasi ya Mhazini Msaidizi kwa kupata kura 9

kwenye Uchaguzi huyo  pia walichaguliwa wajumbe wawakilishi kundi maalumu wa baraza la Mkoa wa Lindi ambapo wajumbe   ambapoArkama Kihaku  kutoka wilaya ya Liwale alipata kura 17 na Nasoro isa kutoka Lindi Mjini alipata kura 2  

Akizungumzia majukumu ya baraza la watoto Daudi Busweli Afisa Maendeleo ya jamii kutoka shirika lisilo la kiserikali la save the children  ambalo linafadhili mabaraza ya watoto mkoa wa Lindi  na shughuli za na kusimamia haki za watoto kwa kushirikiana na asasi za kijamii  za  Kingonet, Ropa na Lingonet  alisema kuwa baraza la watoto linajukumu la kutambua haki za watoto na kuzisimamia haki hizo na kutafuta njia za kuondoa changamoto zinazosababisha watoto kutotendewa haki zao na jamii.
 Akizungumza kwa niaba ya viongozi waliochaguliwa kwenye uchaguzi huyo Mwenyekiti wa baraza hilo  Aziza Ahmadi    amesema kuwa baraza la watoto wilaya humo aliwavumilia wazazi, walezi na wananchi atakaye nyanyasa na  kuvunja  haki ya mtoto ya kupata elimu , Kulindwa kwa kumsababishia Mtoto wa kike hasa wanafunzi akwa  kumpa ujauzito ,kushindwa kumpeleka  shule kwa visingizio visivyo vya msingi.

Aidha Aziza Ahmadi  amewashauri watoto  hasa wa kike kuacha tamaa ambazo zinawaingiza kwenye matatizo yanayosababisha kupata mimba za utotoni ambazo zinaharibu malengo yao ,pia amewataka wazazi kuwalinda watoto wao ili wasiingie kwenye vishawishi hasa wanapokuwa shuleni kwani vishawishi hivyo ndivyo vinapelekea wao kushindwa kuendelea na masomo,

Aziza  amevitaja vishawishi hivyo kuwa ni pamoja na simu za Mkononi ambazo zinajenga uhusiano wa karibu wa wanaume au wanawake wenye tabia za kuwaingiza watoto kwenye matendo yanayokwenda kinyume na haki za watoto na maadili

Aidha ameiomba jamii kutoa ushirikiano kwa baraza la watoto ili liweze kufanya kazi yake bila vikwazo kwa maendeleo ya watoto ambao ni taifa tegemewa la kesho.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad