JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


PROFESA MUHONGO AKUTANA NA KAMPUNI YA AFRICOMMERCE INTERNATIONAL LTD

Share This
WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Africommerce International Limited, Elisante Muro na kuzungumzia fursa mbalimbali za uwekezaji nchini hususan katika sekta ya Nishati.

Muro alimtembelea Waziri Muhongo na kueleza nia ya Kampuni yake kuwekeza kwenye mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirishia mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza na vilevile uwekezaji kwenye mradi wa ujenzi wa nguzo za umeme za zege. 
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Africommerce International Limited, Elisante Muro wakati wa kikao cha kujadili fursa za uwekezaji.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Africommerce International Limited, Elisante Muro (hayupo pichani) ambaye alimtembelea Waziri huyo kuzungumzia fursa za uwekezaji kwenye sekta ya nishati nchini. Wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu- Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo akifuatiwa na Naibu Katibu Mkuu- Madini, Profesa James Mdoe.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza jambo wakati wa kikao na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Africommerce International Limited, Elisante Muro (hayupo pichani) wakati wa kikao cha kujadili fursa za uwekezaji. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu- Madini, Profesa James Mdoe na wa kwanza kulia ni Naibu Katibu Mkuu- Nishati, Dkt. Mhandisi, Juliana Pallangyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad