JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


WAZAZI WAMETAKIWA KUWAPELEKA WATOTO KUPATA MATONE YA VITAMIN 'A'

Share This
Na Chalilla Kibuda,Globu ya Jamii
WAZAZI na walezi nchini wametakiwa kuwapeleka 
watoto wao kwenye vituo vya afya ili wakapate matone 
ya vitamini A na dawa za minyoo ili kujikinga na maradhi 
mbalimbali yatokanayo na kukosekana kwa vitamini 'A'.

Wito huo umetolewa Dar es Salaam na Mtaalamu wa Chakula na Lishe kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe
Tanzania (TFNC), Francis Modaha, wakati alipokuwa akizungumza na waandishi habari kuhusu uhamasishaji wa utoaji wa matone ya vitamini A na dawa za minyoo.

Amesema matone ya vitamini 'A' yanatolewa kwa watoto wenye
umri wa miezi sita na miaka mitano mara mbili kwa mwaka ambapo kwa Tanzania hutolewa mwezi Juni na mwezi Desemba.

Modaha amesema wakati ziezi la utoaji wa matone ya Vitamini A likiendelea kwa awamu ya pili sasa mwezi huu, pia watoto wote wenye umri wa mwaka mmoja hadi miaka mitano hupatiwa dawa ya minyoo.

"Matone ya vitamini A na dawa za minyoo zinatolewa
katika vituo vyote vya afya,ambapo kazi ya utoaji ilianza Desemba Mosi mwaka huu na itaendelea hadi mwishoni wa mwezi huu, naomba wazazi walezi kuwapeleka watoto wenu ili wakapate huduma hizo”amesema Modaha.

Modaha, alitoa wito kwa wazazi na walezi kufahamu umuhimu wa vitamini 'A' kwa ukuaji mzuri wa watoto wao kiafya.

Alitaja baadhi ya sababu za upungufu wa vitamini
'A'
 kuwa ni pamoja na ulaji duni usiokidhi mahitaji ya vitamini'A' unyonyeshaji wa watoto maziwa ya mama usiofuata kanuni, magonjwa ya mara kwa mara na mgawanyo mbaya wa rasilimali.

Amesema vitamini 
'A'
 inahitajika kwa ajili ya ukuaji na
maendeleo mazuri ya mtoto, ikiwa ni pamoja na mifupa na macho.
Aidha amesema upungufu wa vitamini 
'A'
 unahusishwa na ongezeko vifo vya wanawake vinavyotokana na uzazi, vifo vya watoto, kutoona vizuri katika mwanga hafifu, watoto kuzaliwa kabla ya miezi tisa ya ujauzito na kasi ndogo ya ukuaji na maendeleo ya mtoto na kuongezeka kwa uwezekano wa mtoto kupata maradhi.

Alizitaja njia za kuzuia upungufu wa vitamini 
'A' 
kuwa ni
pamoja na kuhamasisha unyonyeshaji maziwa ya mama pekee katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo ya mtoto na kuendelea kumnyonyesha hadi miaka miwili na zaidi..


Alisema kumpa mtoto aliyefikisha umri wa miezi sita vyakula vya ziada ikiwa ni pamoja na vyakula vyenye 
vitamini 
'A'
 kwa wingi pamoja na kutoa nyongeza ya matone kwa watoto.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad