JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


WASHINDI 16 WAPATIKANA KATIKA DROO YA AIRTEL MKWANJIKA

Share This
 Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando (katikati) akiongea na

moja ya  washindi kupitia simu ya mkononi wakati wa kuendesha droo ya
kwanza ya promosheni ya Airtel Mkawnjika ambapo washindi 16 kutoka
katika mikoa mbalimbali walipatikana.  Akishuhudia  Msimamizi wa bodi
ya michezo ya kubahatisha nchini , Bwana Abdallah Hemed  na Afisa
Masoko wa Airtel Bi Rebecca Mauma (kulia)

Meneja Uhusiano wa Airtel, Jackson Mmbando (katikati) akiongea na
waandishi wa habari wakati wa kuendesha droo ya kwanza ya promosheni
ya Airtel Mkawnjika ambapo washindi 16 kutoka katika mikoa mbalimbali
walipatikana.  Akishuhudia  Msimamizi wa bodi
ya michezo ya kubahatisha nchini , Bwana Abdallah Hemed  na Meneja
masoko wa Airtel bi Anethy Muga (kulia)


KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel leo imechezesha droo ya kwanza ya
promosheni ya Airtel Mkwanjika  na kuwapata washindi 16 wa  siku nne
za mwanzo
Promosheni ya Airtel Mkwanjika imezinduliwa na Airtel wiki iliyopita
ikiwa na lengo la kuwazawadia wateja wake katika msimu huu wa siku kuu
za mwisho wa mwaka na X-mass  ambapo jumla ya shilingi milioni 300
zimetengwa na kampuni hiyo kushindaniwa na wateja wake kama  zawadi.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa droo hiyo Meneja Uhusiano
wa Airtel Jackson Mmbando alisema “Airtel Mkwanjika leo tumewanyakuwa
washindi 16 wa siku nne za mwanzo ambapo kila siku ni washindi wanne
na kila mmoja ataweza kujizolea hadi shilingi milioni moja katika
boksi letu la Airtel Mkwanjika.

Mmbando aliwataja walioibuka washindi wa kuingia katika boksi la
Airtel Mkwanjika kuwa Mama Masisimba ,  Abdallah S Rashid, Amani
Maruma, Msafiri Saidi Ruwia , Hassani Hamis Suleyman na  Aida Asabwile
Mwafi wakazi wa mkoa wa Dar, es  salaam. 

Carston Magoah na Godfrey
Frank Kamota wakazi wa Morogoro, Hassan Ngakoma mkazi wa Manyara ,
Safari Aidaru mkazi wa Mbulu, Lupembe Massanja  kutoka Rufiji , Rachel
Obedi Muhumu mkazi wa Moshi na Rodrique kimei  mkazi wa Msumbiji.
Washindi hawa  watapigiwa simu na kupatiwa maelekezo zaidi jinsi ya
kupata na kupoke zawadi zao.

Nae Meneja Masoko wa Airtel Bi Anethy Muga alisema “Promosheni yetu
imeanza kufanikiwa kwa kuwa tayari tumewapata wateja wetu 16 na
tumeshaandaa jumla ya milioni 16 ilikila mmoja akishajizolea pesa
kwenye sanduku la pesa papo hapo tutampatia pesa yake aliyokusanya
kupitia Airtel Money ili akasherehekee sikukuu kwa furaha zaidi”
Promosheni ya “Airtel MKWANJIKA” itawawezesha wateja wote wanaojinga
na kifurushi chochote cha yatosha au kuongeza muda wa maongezi wa
kiwango chochote kwenye simu zao kuingia moja kwa moja kwenye droo ya
siku na kupata nafasi ya kujishindia pesa taslimu.

Hakuna gharama ya ziada wala  malipo yeyote unaongeza salio kwa
kutumia vocha, huduma ya Airtel money au kununua vifurushi vya yatosha



na kujishindia pesa kila siku” alisisitiza Muga.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad