JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


NHIF YAJA NA MPANGO WA BIMA YA AFYA KAYA KWA KAYA

Share This
 Mwakilishi wa Kaimu Mkuruegenzi Mkuu wa NHIF, Eugen Mikongoti akifungua kikao kilichowashirikisha wenyeviti wa bodi na makatibu wa Vituo Vya Afya, Zahanati na Hospitali wa Manispaa ya Temeke juu ya mpango wa bima ya afya kwa kayo iliyofanyika leo jijni Dar es Salaam.
 Meneja wa Mkoa wa Temeke wa NHIF, Costantino Makala akitoa maada katika kikao hicho leo latika ukumbi wa Temeke jijini Dra es Salaam.wa katikati ni Mwakilishi wa Kaimu Mkuruegenzi Mkuu wa NHIF,Eugen Mikongoti Kushoto ni Mganga Mkuu wa Manispaa Temeke,Silvia Mamkwe.
Sehemu ya Wenyeviti wa Bodi na Makatibu wa Vituo vya Afya ,Zahanati na Hospitali katika kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii)

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umesema mpango wa huduma ya afya katika kaya utasaidia upatikanaji wa huduma bora ya matibabu kwa jamii kutokana na mchango wao wa uanachama.

Akizungumza leo Wenyekiti wa Bodi na Makatibu Afya wa Manispaa ya Temeke, Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Eugen Mikongoti amesema sharia iko tayari kwa ajili ya mpango huo kinachotakiwa ni utekelezaji kwa wananchi katika kupata huduma hiyo.

Mikongoti amesema kuwa kila mtu mmoja katika kaya kwa Manispaa ya Temeke atachangia Sh.50000 ambapo atapata matibabu kwa mwaka mmoja katika Vituovya Afya,Zahanati na Hospitali katika Manispaa hiyo.

Amesema fedha ambazo watachangia zitatumika katika kununua dawa na vifaa tiba katika Manispaa hiyo hivyo kila mwananchi atakayejiunga na mpango huo matibabu kwa kutambua mchango wake na dawa lazima ziwepo pamoja na vifaa tiba.

Mikongoti amesema kuwa fedha zinazochangwa na wanachama katika mpango ho zitatumika kwa malenfo yaliyokusudiwa na serikali itachangia asilimia 50.

Amesema NHIF itahakikisha kila mwananchi anakuwa na bima ya afya ili kuweza kupata matibabu yake wakati akifikwa na magonjwa kwani wakati mtu anaweza kuugua ugonjwa na kuweza kushindwa kupata matibabu kutokana na kutokwepo katika mapango wowote.

“NHIF itakuwa karibu na wananchi kama tunavyofanya nia yetu ni kutaka kila mwananchi anakuwa na bima ya afya ya kumfanya maisha yake yawe  mazuri ya uhakika wa matibabu”amesema Mikongoti.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad