JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


C-SEMA , TAJOC WAJADILI ULINZI MTOTO

Share This
 Afisa Mtendaji Mkuu wa C-SEMA, Kiiya Kiiya akizungumza na Waandishi wa Habari za Watoto (TAJOC) na Wadau Watunga Sera katika kampeni Nijali Mtoto wa Tanzania iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Mshauri Mwandamizi wa Kituo cha Huduma ya Simu kwa Mtoto wa C-SEMA, Thelma Dhaje akizungumza na Waandishi wa Habari za Watoto (TAJOC) na Wadau Watunga Sera katika kampeni Nijali Mtoto wa Tanzania iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Wadau wa Watoto wakiwa katika picha ya pamoja jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
WATOTO  wametakiwa kupewa ulinzi katika jamii katika kuweza kuwa na kizazi kinachojiamini na kufanya watoto kuwa wanajiamni ni kuondokana na mila potofu ambazo zinawakandamiza ikiwemo ukeketaji kwa watoto wa kike.

Akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari za Watoto (TAJOC) na Wadau Watunga Sera katika kampeni Nijali Mtoto wa Tanzania, Mkurugenzi wa C-SEMA, Michael Kehongoh amesema ulinzi wa watoto unatakiwa kupewa kupaumbele ikiwemo kutenga bajeti ya watoto.

Kehongoh amesema katika mazingira yaliyopo mtoto anatakiwa ulinzi wa kumuwezeha kuishi ikiwa ni pamoja na serikali kuunda timu za ulinzi ambapo ni Halmashauri chache ambazo zimeweza kufanya hivyo.
Amesema maafisa ustawi wa jamii ni kiungo katika usimamizi wa watoto kwa serikali kuweka kipaumbele cha bajeti ya kuweza kutekeleza majukumu yao.

Kehongoh Maafisa ustawi wa jamii kwa nchi zilizoendelea zimeweka kipaumbele kutokana na kazi wanazozifanya zinahusiana moja kwa moja na jamii na watu wengine wanatakiwa kupata taarifa kwa watu hao.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa TAJOC, Edward Qorro amesema waandishi kuhabarisha masuala yanayohusu watoto ni jukumu letu hivyo kunahitaji ushirikiano katika kupeana taarifa juu ya ulinzi wa watoto.


Amesema kazi ambayo imekuwa kikwazo ni kuwafikia watoto pale inapotokea tatizo hapo hapo kutokana na changamoto ya rasilimali fedha.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad