JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TAARIFA ZAIDI KUHUSU MAHUJAJI KUTOKA TANZANIA WALIOFARIKI AU KUJERUHIWA HUKO SAUDI ARABIA

Share This
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAARIFA ZAIDI KUHUSU MAHUJAJI KUTOKA TANZANIA WALIOFARIKI AU KUJERUHIWA HUKO SAUDI ARABIA

Mahujaji wengine wane (4) kutoka Tanzania ambao walikuwa miongoni mwa wale waliokuwa hawaonekani tangu ajali ya kukanyagana kwa mahujaji ilipotokea Makkah nchini Saudi Arabia tarehe 24 Septemba 2015 wametambuliwa kuwa, ni miongoni mwa mahujaji waliofariki  dunia. Kutambuliwa kwa mahujaji hao kunafanya idadi ya mahujaji wa Tanzania waliopoteza maisha katika ajali hiyo kufikia thelathini na mbili (32). 

Majina ya Mahujaji hao kutoka kikundi cha Khidmat Islamiya ni:-
1. Abdul Idd Hussein
2. Adam Abdul Adam
3. Rashida Adam Abdul
4. Khadija Abdukhalik Said 

Aidha, hadi sasa mahujaji saba (7) kutoka Tanzania bado hawajulikani walipo na jitihada za kuwatafuta bado zinaendelea. Majina ya Mahujaji hao ni:
1. Burhani Nziru Matata
2. Farida Khatun Abdulghani
3. Juma Jecha Jaku
4. Laila Manunga
5. Nassor Mohammed Hemed
6. Saleh Mussa Said
7. Shabinabanu Ismail Dinmohamed

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, 
Dar es Salaam
20 Novemba, 2015

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad