JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MAHAFALI YA NNE SHULE YA SEKONDARI LOUIS MONTFORT, YOMBO, DAR ES SALAAM, NOV 21, 2015

Share This
Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Louis Montfort iliyoko jirani na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, akiwaongoza baadhi ya wahitimu wa kidato cha nne 2015, wa shuke hiyo kuburudisha kwenye mahafali ya nne iliyofanyika shuleni hapo Novemba 21, 2015.  
 Mkurugenzi wa Sheria wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, (TAA), ambaye pia anashughulikia Mahusiano, Ramadhan Maleta, (Kulia), akitoa hotuba wakati wa mahafali ya nne ya Shule ya Sekondari Louis Montfort, iliyoko Yombo jijini Dar es Salaam Novemba 21, 2015. Maleta ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, alisema TAA inafarijika sana kushirikiana na jamii iliyo jirani na viwanja vyake vya ndege kote nchini na kwamba itasaidia kutatua baadhi ya changamoto zinazoikabili shule hiyo ili kuendelea kushirikiana katika kutunza uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

  Mkurugenzi wa Sheria wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, (TAA), ambaye pia anashughulikia Mahusiano, Ramadhan Maleta, (Kushoto), akimkabidhi cheti, Mwanafunzi bora kielimu wa kidato cha nne Emmy Bosco Mduma, wakati wa Mahafali ya nne ya Shule ya Sekondari Louis Montfort iliyoko Yombo jijini Dar es Salaam, Novemba 21, 2015. Maleta ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, alisema TAA inafarijika sana kushirikiana na jamii iliyo jirani na viwanja vyake vya ndege kote nchini na kwamba itasaidia kutatua baadhi ya changamoto zinazoikabili shule hiyo ili kuendelea kushirikiana katika kutunza uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Katikati ni Mkuu wa Shule hiyo, Dkt.Jim Madavana.

Mkurugenzi wa Sheria wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, (TAA), ambaye pia anashughulikia Mahusiano, Ramadhan Maleta, (wapili kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na mwanafunzi wa kidato cha nne ambaye amefanya vizuri kwenye masomo ya kuhitimu kidato cha nne, Emmy Bisco Duma, (watatu kushoto), wakati wa mahafali ya nne ya Shule ya Sekondari Louis Montfort iliyoko Yombo jijini Dar es Salaam Novemba 21, 2015. Wengine kutoka kushoto ni viongozi wa Shule hiyo, Jimmy George, Mkuu wa Shule, Jim Madavana, na Mkuu wa Taaluma, Chiku J. Sekilasi.
 Mkurugenzi wa Sheria wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, (TAA), ambaye pia anashughulikia Mahusiano, Ramadhan Maleta, (kulia), akipokea zawadi kutoka kwa kiongozi wa Shule ya Sekondari ya Louis Montfort iliyo jirani na uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, wakati wa mahafali ya nne ya kidato cha nne shuleni hapo Novemba 21, 2015. Maleta ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, alisema TAA inafarijika sana kushirikiana na jamii iliyo jirani na viwanja vyake vya ndege kote nchini na kwamba itasaidia kutatua baadhi ya changamoto zinazoikabili shule hiyo ili kuendelea kushirikiana katika kutunza uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
(Picha Kwa Hisani ya TAA)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad