JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


WANAWAKE LINDENI KURA ZENU:BAWACHA

Share This
Mke wa Mgombea Urais wa Chadema, Edward Lowassa, Regina Lowassa akiwa katika mkutano wa hadhara
Mke wa Mgombea Urais wa Chadema, Edward Lowassa, Regina Lowassa akiwa katika mkutano wa hadhara.

BARAZA la Wanawake la Chama Cha Demokrasia (Chadema) Taifa, Bawacha, limewataka wanawake nchi nzima kupiga kura na kukaa mita 200 ili kulinda kura zao kwani ni haki yao kisheria.
Kauli hiyo imetolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Bawacha Kunti Yusuph wakati wa mkutano na wanawake, uliofanyika katika ofisi za Chadema kanda ya ziwa Victoria jijini hapa.

Kunti ambaye ni mratibu wa mikutano ya kukutana na wanawake ya mke wa Mgombea Urais wa Chadema, Edward Lowassa, Regina Lowassa, amesema kuwa kupitia wanawake wa Mwanza, wanawake nchi nzima wanapaswa kupiga kura na kulinda kura zao.

Amesema endapo wanawake na watanzania kwa ujumla watapiga kura na kuondoka watakuwa wamevunja sheria ya nchi hivyo amewaomba kulinda kura zao kwani ndio maisha yao.




Hata hivyo Regina aliwaomba wanawake na watanzania kwa ujumla kupiga kura kuanzia ngazi ya Udiwani, Ubunge na nafasi ya Urais kwa maendeleo ya Taifa. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad