Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
IKIWA zimebakia siku nane kufikia Uchaguzi Mkuu, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda amewataka wananchi wa wilaya hiyo kusimamia amani na utulivu wa nchi bila kufanya hivyo ahadi za wagombea wote hazitoweza kutekelezeka na badala yake kuanza kuugua maumivu ya uchaguzi huo
Makonda ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kinondoni pamoja na wenyeviti wa serikali za mitaa, wagombea wa ngazi mbalimbali za uongozi, wasimamizi wa uchaguzi na viongozi wa vyama vya siasa .
“ Sisi sote tunatoka katika itikadi tofauti tofauti lakini wote tupiganie maendeleo yaTaifa kwa ujumla kuweza kupiga kura kwa staha kuweza kulinda amani na vikundi vyovyote visiweze kukaa katika eneo la kupigi kura" amesema Makonda.
Amesema Wilaya ya Kinondoni isiwe chanzo cha kusambaza chuki na kwamba kila mwenyekiti wa serikali ya mtaa ajitambue kuwa ana mamlaka tosha yakusimamia na kutekeleza uwepo wa amani.
Makonda amesema viongozi wa mitaa wao ndio wenye mamlaka tosha ya kuhakikisha maeneo wanaoishi yanabakia kuwa na amani wakati wa upigaji kura na wakati wa kusubiria matokeo.
Amesema yapo baadhi ya maeneo ambayo watumishi wa serikali wanashindwa kutekeleza wajibu wao ili kuibua chuki kwa wananchi kuwa serikali haiwajibiki kwao, hivyo viongozi wa mitaa watakapooona hali kama hizo wawajibuike kutoa taarifa.
Aidha Makonda amepiga marufuku vikundi vinavyoundwa kwa ajili ya kusimamia kura na kwamba pindi akipata taarifa atawashughulika nao bila aibu katika kuweza kumalizika kwa uchaguzi huku amani ikitawala.
Nae Mkurugenzi wa Kinondoni, Mussa Natty amesema suala la ulinzi na usalama ni la kila mtu na kuwataka viongozi wa mitaa kutoa taarifa ya kile kinachofanyika katika maeneo yao.
Amesema wananchi wanatakiwa kukaa mita 200 baada ya kupiga kura, na kama kuna kijiwe ambacho kina wakereketwa wasiwepo katika eneo hilo ni amri.
No comments:
Post a Comment