jlogo

Karibuni Jamvini Wanajamii

topads

Post Top Ad

demo-image

MKUU WA WILAYA YA SHINYANGA AFANYA MKUTANO NA AKINA MAMA ZAIDI YA 300 KUPAMBA NA KIPINDUPINDU SHINYANGA

Share This


Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza wakati wa mkutano wake na wanawake zaidi ya 300 katika manispaa ya Shinyanga uliofanyika katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine alisema wanawake ni jeshi kubwa na ni walimu wakubwa katika familia hivyo wana nafasi kubwa ya kupambana na kipindu pindu kwa kuimarisha na kuhamasisha usafi kwa akina baba,watoto na hata wanawake wenzao.
P1200374
"Kipindu pindu ni hatari sana...kinaua lazima tupambane nao kwa nguvu zote..nimewaita ili kila mmoja ajue Shinyanga tuna janga..sasa kila mtu achukue hatua,ugonjwa huu unatokana na uchafu..akina mama mna nafasi kubwa sana katika hili...."alisema Matiro.
P1200420
Akina mama wakiwa wamenyoosha mikono...kwamba wako tayari kupambana na kipindupindu.
P1200420

Hapa ni katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga ambako wanawake/akina mama zaidi ya 300 wa manispaa ya Shinyanga wamekutana kujadili namna ya kupambana na ugonjwa wa Kipindupindu ambao umeukumba mkoa wa Shinyanga.Mkutano huo umeitishwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.Akina mama hao waliojitokeza kwa wingi leo jioni Oktoba 06,2015 wameweka mikakati mbalimbali ya kutokemeza ugonjwa kipindupindu ambapo Jana pekee wagonjwa 9 wamelazwa katika kambi maalum jirani na hospital ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga ambapo kati ya hao 9 wawili wamefariki dunia.
P1200360
Mkuu huyo wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro aliwaeleza akina mama hao kuwa chanzo cha ugonjwa huo ni uchafu yaani kula au kunywa kinyesi cha mtu mwingine hivyo ili kuhakikisha ugonjwa kipindu pindu ni vyema wananchi wakajenga vyoo,kuepuka kunywa maji yasiyochemshwa,kula vyakula vya moto,kuosha matunda kabla ya kula sambamba na kuepuka kunywa pombe za kienyeji.
P1200363
Afisa afya mkuu wa manispaa ya Shinyanga Elly Nakuzelwa akizungumza wakati wa mkutano huo ambapo alisema ugonjwa huo unazidi kuenea kwa kasi katika manispaa ya Shinyanga ambapo jana pekee wagonjwa 9 walifikishwa katika kambi maalum ya wagonjwa wa kipindu pindu jirani na hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga.
P1200365
Afisa afya huyo alisema ili kuhakikisha ugonjwa huo unatokomezwa katika manispaa ya Shinyanga tayari wamepiga marufuku tabia ya akina mama lishe na baba lishe kutembeza vyakula mtaani,unywaji pombe za kienyeji,kuzuia matanga kwenye familia yoyote iliyopatwa na kifo pamoja na kula vyakula kwenye sherehe yoyote.
P1200366
Afisa afya mkuu wa manispaa ya Shinyanga Elly Nakuzelwa aliwataka wakazi wa Shinyanga kufika haraka hospitali pindi wanapoona dalili za ugonjwa wa kipindupindu ikiwemo kuharisha na kutapika mfululizo.
P1200367
Mkutano unaendelea
P1200371
Nakuzelwa aliwataka wananchi kujenga tabia ya kufunika vyoo vya shimo,kuepuka kula vyakula kwenye mikusanyiko ya watu wengi,kuacha kutembeza vyakula mtaani,kuuza vyakula shuleni,kununua mboga zinazouzwa chini badala ya kwenye meza.
P1200372
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisisitiza juu ya matumizi ya vyoo majumbani kwani chanzo kikubwa cha ugonjwa wa kipindupindu ni kunywa au kula kinyesi cha mtu mwingine baada ya kuchanganyikana na vyakula ama maji anayokunywa binadamu.
P1200376
Akina mama kutoka manispaa ya Shinyanga wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini ambapo walikubaliana kuimarisha usafi ili kutokomeza ugonjwa hatari wa kipindupindu
P1200378
Miongoni mwa dalili za ugonjwa wa kipindu pindu zilizotajwa ukumbini ni pamoja na kuharisha na kutapika mfululizo.
P1200383
Meza kuu wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini
P1200387
Akina mama wakifuatilia kilichokuwa kinajiri ukumbini
P1200389
Viongozi mbalimbali wa mitaa katika manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye mkutano wa akina mama katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga
P1200391
Mmoja wa akina mama hao akichangia mawili matatu katika mkutano huo
P1200392
Katika mkutano huo pia ilibainika kuwa wananchi wengi mjini Shinyanga hawana vyoo hali ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa kuenea kwa ugonjwa wa kipindupindu
P1200393
Wanawake hao pia walisisitizwa kujenga tabia ya kuwaelimisha wanaume juu ya umuhimu wa kujenga vyoo
P1200394
Mkutano unaendelea
P1200412
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumzia kuhusu amani ya nchi ambapo alisema serikali imejipanga vyema kukabiliana na watu waliojiandaa kufanya vurugu ikiwemo kuzuia wanawake na wazee wasipige kura siku ya uchaguzi mkuu nchini utakaofanyika Oktoba 25,2015.
P1200395
Wanawake hao pia walihamasishana kushiriki uchaguzi mkuu ujao huku wakiiomba serikali kuimarisha ulinzi kwao na wazee kwani kumezuka uvumi kuwa kuna watu watawazuia kushiriki uchaguzi Oktoba 25 mwaka huu
P1200396
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akawahamasisha wanawake kushiriki katika shughuli za maendeleo badala ya kutegemea wanaume...akasisitiza juu ya umuhimu wa kujiunga katika vikundi vya wajasiriamali ili serikali iweze kuwasaidia kwa urahisi zaidi badala ya kufuata mtu mmoja mmoja
P1200397
Akina mama wakisikiliza kilichokuwa kinajiri ukumbini
P1200398
Mkutano unaendelea
P1200400
Mkutano unaendelea
P1200402
Mkutano unaendelea
P1200403
Maendeleo bila amani ni kazi bure...akina mama wakahamasishana kushiriki kulinda amani ya nchi....
P1200404
Hakuna kutishana siku ya uchaguzi...mkuu wa wilaya ya Shinyanga akawahakikishia ulinzi siku ya uchaguzi huku akiwataka kulinda kadi zao za kupigia kura.



P1200405


Wanawake na maendeleo ndiyo makubaliano waliyoafikiana.....
P1200406
Mkutano unaendelea
P1200409
Mkutano unaendelea
P1200410
Mkutano unaendelea
P1200411
Mkutano unaendelea
P1200422
Afisa mtendaji kata ya Shinyanga Mjini Mathias Masalu akizungumza katika mkutano huo
P1200424
Mwenyekiti wa mtaa wa Kaunda Joha Mussa akifunga mkutano huo
P1200426
Akina mama wakitawanyika baada ya mkutano
P1200429
Kila mmoja na njia yake...kushoto ni Mama Steve na Marietha William wakirudi kwao
Picha zote na Kadama Malunde- Malunde 1 blog
Comment Using!!

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad