WATANZANIA wametakiwa kuendelea kudumisha amani hasa kipindi cha uchaguzi kwani bado nchi yetu inasifika kwa amani dunia kote
kauli hiyo imetolewa na mwanaharakati wa amani Mhonda Joseph wakati akizungumza na waandishi wa habari jiji Dar es Salaam.
Mhonda amesema wananchi wahakikishe amani inakuwepo na hata wageni wanaoishi hapa kutokana na historia ya miaka ya nyuma ya hapa nchini kuwa ya amani.
Aidha amewataka watanzania wasikubali baadhi ya watu wachache kuja kuchochea utovu wa amani na wakumbuke amani ikipotea ni vigumu kuirudisha pindi itakapotoweka.
lakini pia Mhonda ameeleza kuwa hatua tuliyofikia ya kuwa na vyama vingi ni moja ya maendeleo ni mhimu kuhakikisha tunachagua kiongozi bora atakao watumikia watanzania wote kutokana na hali ya ugumu wa maisha kwa sasa.
hata hivyo amewataka mawakala kuhakikisha wanafanya kazi zao bila kukubali kufanya vurugu pindi wanaposimamia wakati wa kuhesabu
No comments:
Post a Comment