JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI (SBL) YAHITIMISHA KAMPENI YA “SERENGETI MASTA” KWA KISUMA TEMEKE

Share This
 Mshiriki wa shindano la mwisho la kumtafuta Serengeti Masta kwa wilaya ya Temeke Emmanuel Nyaulingo (kulia) akipokea zawadi ya fulana kabla ya shindano hilo kuanza rasmi ambalo lililofanyika mwishoni mwa wiki katika baa ya Kisuma iliyopo Temeke jijini Dar es salaam. (kushoto) ni balozi wa bia ya Serengeti Premium Lager Caroline Vincent na anayeshudia (katikati) ni mshereheshaji wa shindano hilo Richard Godwin. Kampeni hiyo inafikia tamati jijini Dar es salaam baada ya kumalizika mikoani pia ambapo imefanikiwa kuzifikia baa zaidi ya 200 kwa kipindi cha miezi mitatu ya Kampeni.
 Mshiriki wa shindano la Serengeti Masta Sebastian Kaluma akionja ladha tofauti za chapa za bia mbalimbali kutoka Kampuni ya bia ya Serengeti ili kuweza kuitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti Premium Lager katika shindano la kumtafuta Serengeti Masta wa wa wilaya ya Temeke ambalo lilifanyika katika baa ya Kisuma ya Temeke jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki hii. Shindano hilo la miezi mitatu linalodhaminiwa na bia ya Serengeti Premium Lager limewakutanisha wapenzi mbalimbali wa bia hiyo huku likitoa elimu juu ya bia yake na zawadi mbalimbali kama fedha taslim na fulana za bure katika kipindi chote cha kampeni.
 Msimamizi wa mauzo ya Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Temeke Amani Kimaro (Katikati) akionyesha kiasi cha Tsh. 100,000/= ambayo alimkabidhi mshindi wa shindano la Serengeti Masta Elisha Mwenga (kulia) ambaye aliyewabwaga wenzake wane (4) katika kuitambua ladha halisi ya bia Serengeti Premium Lager wakati wa shindano hilo ambalo lilifanyika katika Baa ya Kisuma iliyopo Temeke jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki hii. (Kushoto) ni mshereheshaji wa shindano hilo Richard Godwin.
 Msimamizi wa mauzo ya Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Temeke Amani Kimaro (Kushoto) akikabidhi kiasi cha Tsh. 100,000/= kwa mshindi wa shindano la Serengeti Masta Elisha Mwenga ambaye aliibuka mshindi wa jumla wa wilaya ya Temeke katika kuitambua ladha halisi ya bia Serengeti Premium Lager wakati wa shindano hilo lililofanyika mwishoni mwa wiki katika Baa ya Kisuma iliyopo Temeke jijini Dar es salaam. Shindano hilo la “Serengeti Masta” linalodhaminiwa na bia ya Serengeti linafikia tamati jijini Dar es salaam baada ya kuwafikia wapenzi mbalimbali wa bia hiyo huku wengi wakijinyakulia Tsh.50, 000/= mwanzoni mwa kampeni na kupewa cheo cha Serengeti Masta.

Mshindi wa jumla wa shindano la Serengeti Masta kwa wilaya ya Temeke Elisha Mwenga akionyesha juu fedha taslim Tsh. 100,000/= alizopokea wakati wa shindano la la kumtafuta mshindi wa jumla wa wilaya hiyo lililofanyika mwishoni mwa wiki hii katika baa Kisuma iliyopo Temeke jijini Dar es salaam. Ushindi wa jumla wa Bw. Elias umekuja baada ya kuwabwaga washiriki wenzake wanne katika mtanange wa mwisho wa kuitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti Premium Lager kati ya chapa nyingine nne za Kampuni ya bia ya Serengeti.  Shindano hilo la “Serengeti Masta” limefanikiwa kuwafikia wahudumu wa baa mbalimbali jijini Dar es salaam na mikoani katika kipindi chote cha Kampeni na kuwaelimisha  juu ya utoaji huduma kwa wateja wa bia hiyo jambo ambalo liliongeza mauzo ya bia hiyo katika baa zao.


Na Mwandishi wetu.
KAMPENI ya “Serengeti Masta” iliyokua ikiendeshwa na Kampuni ya bia ya Serengeti chini ya udhamini wa bia yake namba moja ya Serengeti Premium Lager, imefikia kilele jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki baada ya kampeni hiyo kuzunguka kwa muda wa miezi mitatu katika miji ya Arusha, Mbeya, Mwanza na Morogoro.

Katika kufunga Kampeni hiyo kwa kishindo, kwa kushirikiana mameneja wa bia ya Serengeti Premium Lager, walijipanga kuwafikia mashabiki wengi zaidi wa bia hiyo ambapo iliwalazimu kufanya shindano la “Serengeti Masta” katika baa tatu zilizopo jijini Dar es salaam kwa siku tofauti.

Sherehe hizo ambazo zilionekana kuwafurahisha mashabiki wengi wa bia ya Serengeti Premium Lager, ziliambatana na burudani ya mziki, zawadi za fedha taslim, fulana na bia za bure.

Baadhi ya baa za jijini Dar es Salaam, ambazo zilizochaguliwa kuimalizia promosheni hiyo ni pamoja na Kisuma iliyopo Temeke, Zambezi Ubungo na Havana Park ya Segerea.

Akiizungumzia promosheni hiyo mmoja wa wateja maarufu wa bia ya Serengeti Premium Lager aliyehudhuria shindano la “Serengeti Masta” katika baa ya  Kisuma iliyopo Temeke jijini Dar es Salaam, Bw. Salehe Kitwana, aliipongeza Kampuni ya bia ya Serengeti na mameneja wa bia hiyo, kwa kuibua kampeni ambayo imeweza kuwahamasisha wahudumu wa baa mbalimbali jijini Dar es Salaam na mikoani katika utoaji huduma bora kwa wateja wa bia hiyo, sambamba na kuwazawadia fedha taslim washiriki mbalimbali walioweza kuitambua ladha halisi ya bia ya Serengeti baada ya bia hiyo kushindanishwa na bia nyingine tano zinazotengenezwa na Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL).

“Promosheni kama hii inawaunganisha mashabiki na kuwafanya waipende bia yao zaidi na zaidi pia nadhani huu ni mfano wa kuigwa na bia nyingine zinaweza kujifunza mengi kutokana na promosheni kama hii”.alisema Bw. Salehe.

Naye Meneja Masoko wa bia ya Serengeti Premium Lager Bi. Anitha Msangi alisema,”Kampeni hii imekuwa ikiendeshwa kwa muda wa miezi mitatu sasa na kuanza kupamba moto baada ya mashabiki kuipokea kwa mikono miwili na kuifanya kuwa maarufu.

Alisisitiza kuwa, shindano la “Serengeti Masta” ni moja kati ya kampeni kubwa ambazo zimeweza kufanikiwa kiutekelezaji kwa mwaka huu, ikiwa ni moja ya kazi kubwa zilizofanywa na Kampuni ya bia ya Serengeti.

Bi. Msangi pia alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wateja wote wa bia ya Serengeti Premium Lager mameneja wa baa mbalimbali walioshiriki kwenye kampeni hii na wafanyakazi wote wa SBL nchi nzima kwa kuwaunga mkono na kushiriki kikamilifu katika kufanikisha zoezi zima la kampeni hiyo.

Aliongeza kuwa pamoja na ushiriki wa wateja kuwa mzuri lakini pia wamefanikiwa kuongeza mauzo ya bia ya Serengeti kufikia kiwango kikubwa kuliko hapo awali kwa mwaka huu.

Tafiti mbalimbali zilizofanywa na SBL katika kipindi cha miezi mitatu ya kampeni hii imedhihirisha kuwa kampeni hiyo haikufaidisha tu kampuni ya bia ya Serengeti bali pia baa zaidi ya 4000 zilizotembelewa na shindano hilo nchi nzima katika kipindi chote cha miezi mitatu.

Vilevile kampeni hiyo imeibua washindi mbalimbali waliopewa cheo cha Serengeti Masta ambao walijizolea fedha taslim na bia za bure, fulana na zawadi mbalimbali.

“Namshukuru Mungu na sisi pia tumebahatika kuweza kuwa sehemu ya kampeni hii kabla ya kufikia tamati na ninajiona kama mwenye bahati sana” alisema Meneja wa baa ya Kisuma Thomas Kimaro ambaye alihojiwa na waandishi wa habari wakati wa shindano la mwisho la Serengeti Masta lililofanyika kwenye baa yake.

Kimaro aliipongeza Kampuni ya bia ya Serengeti kwa kuwa mashuhuri wa kubuni mambo mapya kila kukicha na kuwasihi kuendelea kuleta promosheni kama hizi kwa kuwa zinaongeza mauzo ya bia hizo kwenye baa zao.                                                                                                              
Kampeni ya Serengeti Masta ilianzishwa mahususi kwa ajili ya kurudisha shukrani kwa wateja wa bia ya Serengeti Premium Lager mara baada ya bia hiyo kushinda kinyang’anyiro cha bia ya kimataifa yenye viwango bora katika tuzo za “monde selection” za mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad