JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


ITUMIENI BRN KULETA MABADILIKO:KIKWETE

Share This
Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete ambaye siku chache zijazo atamaliza muhula wake wa pili na wa mwisho wa kuiongoza Tanzania, amewaaga watumishi wa umma nchini kwa kutoa rai kuwa ili kuendeleza mageuzi katika kuwatumikia wananchi ni vyema wakautumia vyema mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).

Rais Kikwete aliyasema hayo katika sherehe maalum iliyoandaliwa na watumishi wa umma kumuaga na kufanyika Dar es Salaam Alhamisi usiku. Watumishi wa umma walitumia fursa hiyo kumpa Rais tuzo na zawadi mbalimbali na kumshukuru kwa mageuzi makubwa aliyoyaasisi katika kuboresha maslahi ya watumishi na mfumo mzima wa mageuzi.

Akitaja moja ya mambo ambayo Rais Kikwete atakumbukwa nayo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema kuasisiwa kwa mfumo wa usimamizi na utekelezaji wa miradi wa BRN katika awamu ya pili ya Rais Kikwete kumesaidia kuongeza nidhamu ya utendaji unaopimika na ambao umesaidia kuleta mageuzi makubwa.

“BRN imeleta nidhamu ya kuweka vipaumbele, kuvifuatilia kwa karibu na kuwawekea watumishi mfumo wa kupimwa kutokana na yale waliyotakiwa kuyatekeleza. Tunakushukuru kwa kuasisi mfumo huu,” alisema.

Akionekana kufafanua hilo, Rais Kikwete alieleza historia na chimbuko la BRN kuwa ni matokeo ya mafanikio ya ziara zake za nje ya nchi ambapo akiwa Malaysia alijifunza jinsi nchi hiyo ilivyopata maendeleo makubwa na ya haraka kupitia mfumo kama wa BRN.

“Si vibaya kuiga jambo jema. Niliposikia kuhusu ufanisi wa mfumo huu kule Malaysia niliomba fursa ya kuelezwa zaidi na ndipo nasi tukakubaliana kuuanzisha hapa nchini. Na katika kipindi kifupi zile sekta za mwanzo zilizoingizwa katika BRN utofauti umeanza kuonekana,” alisema Rais Kikwete.

Akifafanua kuhusu mfumo huo unavyofanyakazi Rais aliongeza kuwa moya ya nidhamu za BRN ni kufanya uchambuzi wa kina wa kimaabara ambapo wataalum wa sekta husika; kutoka sekta za umma na binafsi hukaa pamoja ili kuchambua, kubaini changamoto na namna ya kuzifanyia utatuzi.

Aliongeza kuwa baada ya kubaini mambo yanayohitaji kufanyiwakazi, mfumo wa BRN unasisitiza katika kuchagua vipaumbele vichache ambavyo hutekelezwa kwa mfumo wenye usimamizi madhubuti, ukomo wa utekelezaji huku pia wahusika wakisaini mikataba ya kuhakikisha malengo waliyowekwa yanatokea.

“Huu ni mfumo wa utendajikazi ambao kila mmoja wetu anapaswa kuuchukua na kuutumia kuendesha shughuli zake,” alisema Rais huku akitoa mfano wa Mahakama ya Tanzania ambao waliichukua nidhamu BRN katika kupunguza mrundikano wa kesi hata kabla sekta hayo haijaingizwa rasmi katika BRN.

“Siku moja Jaji Mkuu akaniambia kuwa wameanzisha BRN yao ambapo kila Jaji alipewa lengo na idadi ya kesi za kufanyiakazi kwa mwaka  na kweli baada ya muda mfupi ule mrundikano wa kesi ukapungua sana,” alisema Rais na kusisitiza.

Sekta za awali zilizoingizwa katika BRN tangu Julai 2013 ni elimu, kilimo, nishati, maji, uchukuzi na ukusanyaji wa mapato. Kutokana na mafanikio yaliyoanza kuonekana katika sekta hizo Julai mwaka huu sekta za afya na uboreshaji wa mazingira ya biashara nazo zimeanza kusimamiwa kupitia mfumo wa BRN.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad