JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


AMANI NDIO SILAHA YA MTANZANIA KATIKA UCHAGUZI MKUU-JAJI MUTUNGI

Share This
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
MSAJILI wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Mstaafu, Francis Mutungi alisema kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 25 kuweka kipaumbele cha amani ambayo isiweze kuharibiwa kwa kutokana na uchaguzi.

Mtungi aliyasema hayo alipokutana na wahariri wa vyombo vya habari katika kusisitiza amani katika uchaguzi mkuu na kutaka waandishi kutumia kalamu vizuri kwani amani ikiharibika hakuna anayebaki salama.

Amesema matatizo ambayo yameanza kutokea katika kamapeni yanayotokana na mtu mmoja yasiwekwe katika sura ya taifa na kuonekana vyombo vya serikali vinashindwa kusimamia.

Jaji Mutungi amesema amani ikiangaliwa kwa jicho la karibu kwa kutambua kuna maisha baada  uchaguzi ambapo bila kufanya hivyo maisha hayatakuwepo.

“Waandishi kwa kutumia kalamu zenu mtafanya nchi ibaki kuwa na amani kwani wananchi wanaamini vyombo vya habari kwa kila hatua inayotokea katika uchaguzi mkuu”amesema Mutungi.

Aidha amesema amevitaka vyama vya siasa kutambua wajibu na sio kuangalia uchaguzi huru na haki kwani wajibu ndio utafanya vitu view salama na kuweza kuvuka suala hili la uchaguzi mkuu.
 Msajili wa Vyama vya Siasa nchini,Jaji Mstaafu,Francis Mutungi akizungumza  mkutano wa wahariri na waandishi (hawapo pichani) juu ya amani kuelekea uchaguzi mkuu 25 ,uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
 Wahariri na waandishi wa habari wakimsikilia Msajili wa Vyama vya Siasa nchini,Jaji Mstaafu,Francis Murungi hayupo pichani katika mkutano wake uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Wahariri na waandishi wa habari wakiwa katika picha ya pamoja na Msajili wa Vyama Siasa nchini,Jaji Mstaafu Francis Mutungi,jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad