jlogo

Karibuni Jamvini Wanajamii

topads

Post Top Ad

demo-image

WANANCHI WAJITOKEZA KWA WINGI KWENYE MAONESHO YA SIKU YA BAHARI DUNIANI

Share This
 Wananchi mbalimbali wakiwa katika banda la Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), katika maonyesho ya siku ya bahari duniani yanayoadhimishwa kitaifa Mkoani Mtwara Leo, Asubuhi.
DSC_5712
  Wananchi mbalimbali wakipewa machapishi na mtaalam wa Mamlaka ya  Usafiri Baharini Zanzibar (ZMA), wakati walipotembelea banda la Mamlaka hiyo leo asubuhi, wakati wa maadhimisho ya siku ya bahari duniani yanayoadhimishwa kitaifa mkoani Mtwara.
DSC_5714
  Wananchi mbalimbali wakiwa katika banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), kwenye maonyesho ya Siku ya Bahari yanayoadhimishwa kitaifa mkoani Mtwara, kama walivyokutwa leo asubuhi.
DSC_5717
 Kepteni Emmanuel Marijani kutoka Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(SUMATRA), akiwapa wananchi maelezo ya namna boti zinavyotakiwa kujengwa kwa kiwango maalum kimataifa wakati walipotembelea banda la Mamlaka hiyo leo asubuhi katika maadhimisho ya siku ya bahari duniani yanyoadhimishwa kitaifa Mkoani Mtwara.
DSC_5721
 Mtaalam kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya jamiiMifuko ya Jamii, akiwapa maelezo namna taasisi hiyo inavyofanya kazi katika maonyesho ya Siku ya BAhari Duniani yanayofanyika kitaifa Mkoani Mtwara.
DSC_5723
Wananchi wa Mkoani Mtwara, wakimsikiliza Afisa Mteule Daraja la Pili WOII kutoka Kikosi cha Wanamaji, Makao Makuu, Kigamboni, Dar es Salaam, Jackson Kavula, wakati wananchi hao walipotembelea banda la NAVY katika maonyesho ya Siku ya BAhari Duniani, yanayoadhimishwa Kitaifa Mkoani Mtwara.
(Habari Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikali-Uchukuzi)
Comment Using!!

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad