JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TUSKER FANYAKWELI KIWANJANI YAWAKUNA WAKAZI WA MBEZI BEACH NA KIMARA WIKI HII

Share This
 Mpenzi wa bia ya Tusker aliyefahamika kwa jina la Kikya Mathias akizungumza na mshereheshaji wa promosheni ya Tusker Fanyakweli Kiwanjani Gadner Habash kabla ya kupokea zawadi yake ya mfuko na fulana wakati wa hafla ya kuipongeza baa ya Coast Pub iliyopo Tangi Bovu-Mbezi Beach jijini Dar es salaam ambayo iliibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker. Akijiandaa kutoa zawadi hiyo (nyuma yake) ni Balozi wa bia ya Tusker Veronica Mbilinyi. Lengo kuu la kampeni hii ikiwa ni kuzifikia baa mbalimbali jijini Dar na mikoani na kuzihamasisha kufanya kweli linapokuja suala la utoaji huduma kwa wateja lakini pia kuzisaidia baa hizo kuongeza mauzo ya siku wakati wa promosheni.
 Mkazi wa Kibaha-Pwani Bi Emelda Joseph akipokea zawadi ya fulana toka kwa Msimamizi wa Mauzo wa Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Ubungo Victor Mhindi katika hafla ya kuipongeza baa ya Miti Mitatu ya Kimara-Korogwe jijini Dar es salaam mara baada ya baa hiyo kuibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker
 Mshereheshaji wa kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani Gadner Habash (aliyesimama) kwenye picha ya pamoja na Bw. Cheni Omary ambaye alijishindia bia za bure na fulana wakati promosheni ya Fanyakweli Kiwanjani ilipokua ikiendelea katika kiwanja cha Miti Mitatu kilichopo Korogwe jijini Dar es salaam.
 Mteja wa bia ya Tusker Ezra Mlawa (katikati) akizungumza na mshereheshaji wa kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani Gadner Habash (kulia) mara baada ya meza yake kufikiwa na zawadi ya bia za bure na fulanakatika hafla ya kuipongeza baa ya Miti Mitatu iliyopo Kimara-Korogwe jijini Dar es salaam ambayo iliibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker. (Kushoto) nibalozi wa bia hiyo Veronica Mbilinyi. Tofauti na jiji la Dar, kampeni hiyo pia inaendelea mikoa mbalimbali nchini kama Arusha, Moshi, Mwanza, Morogoro na Mbeya.
Mteja wa bia ya Tusker Bi. Elizabeth Ulomi (katikati) akipokea zawadi yake ya mfuko wenye fulana toka kwa Msimamizi wa Mauzo ya Kampuni ya bia ya Serengeti kanda ya Mbezi Beach Obedi Salema (kulia) wakati wa hafla ya kuipongeza baa ya Coast Pub iliyopo Tangi Bovu-Mbezi beach jijini Dar es salaam ambayo iliibuka mshindi wa wiki kwenye kampeni ya Fanyakweli Kiwanjani inayoendeshwa na bia ya Tusker.(kushoto) ni mshereheshaji wa promosheni hiyo Gadner Habash.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad