JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


JENGENI IMANI NA CCM KWA MAENDELEO ZAIDI - JIMSONI MHAGAMA

Share This
 Katibu  wa CCM wilaya ya  Mufindi, Jimsoni Mhagama 
KATIBU wa CCM wa wilaya ya Mufindi Bw. Jimson Mhagama amesema kuwa chama  cha mapinduzi (CCM ) kitaendelea  kuongoza kwa kuzingatia uadilifu, , amani, upendo, utulivu na kuleta maendeleo kwa wananchi wake  hivyo  kuwataka  wananchi kuchagua cheni nyenye msimamo wa kuwa na diwani, mbunge na rais wa CCM ili  kuendelea  kuwaletea maendeleo .
 
Bw. Mhagama aliitoa kauli  hiyo  jana alipokuwa akihutubia wananchi katika mkutano  wa  kampeni za udiwani wa kata ya Bomani kwa  kumnadi mgombea wa kata hiyo  Bw. John Chota  ,kuwa  wananchi waanze kumuunga mkono diwani, na mbunge anayegombea wa CCM Bw. Cosato Chumi kumchagua kuwa mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini pamoja na kuelekeza kura zote  kwa Mgombea wa Urais dkt. John Magufuli.
 
“Uongozi wowote wenye cheni moja ya kutoka chama kimoja ndiyo unaoweza kuleta maendeleo na hivyo ninawaomba kura zenu mzielekeze kwa diwani wetu John Chota, Mbunge wetu Bw.  Cosato Chumi pamoja na Rais wetu dkt. John Pombe Magufuli ili kuunda cheni moja ya mshikamano na kutokana na uwepo wa cheni hiyo kutakuwa na mfumuko sahihi wa maendeleo kwa wananchi katika sekta zote zikiwemo za elimu, kilimo, afya, barabara, ujasiliamali, kutunza mazingira, ajira kwa vijana na uwezeshaji wa akina mama”, alisema Bw. Jimson Mhagama.
 
Alisema kuwa kutokana na kuwepo kwa cheni moja ya kimaendeleo uongozi wa awamu ya Tano utakapoingia madarakani utahakikisha kuwa shule zote za sekondari zinapatiwa umeme, kuendeleza ujenzi wa maabara, kuhakikisha zinapatiwa walimu wa kutosha  na kuongeza kuwa elimu itatolewa bure kuanzia shule za msingi hadi sekondari kwa ajili ya kuhakikisha kuwa watanzania  walio wengi ambao ni vijana wanaelimika na kunufaika na matunda ya nchi yao.
 
Aidha, alisema kuwa mara baada ya uchaguzi Jimbo la Mafinga litahakikisha kuwa linajenga stendi kubwa ya kisasa ya mabasi yaendayo mikoani ambayo yanapita katika Mji wa Mafinga  ambapo alisema kuwa ujenzi wa stendi hyo utagharimiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa LAPF ambapo stendi hiyo inatarajia kugharimu zaidi ya shilingi Bilioni 3.5 na kuongeza kuwa utendaji huo utakwenda sambamba na wananchi kuchagua cheni moja ya CCM na siyo kuleta mchanganyo wa wagombea.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad