Kawaida unapokuwa umeingia katika mkataba au makubaliano katika jambo lolote
lile kunakuwa na masharti ambayo unapaswa kuyatimiza au kutimiziwa. Na hapa
nazungumzia mikataba yote uwe wa kuuza mbuzi au ule wa kujenga ghorofa mia,
yote ni mikataba. Masharti hayo huwa ndio makubaliano yenyewe au twaweza
kusema kuwa ndio mkataba wenyewe. Kila upande unawajibika juu ya utekelezaji
wa masharti hayo. Yeyote anayefikia hatua ya kukiuka masharti hayo au hata
kukiuka sharti moja tu, hana namna ila kukubaliana na hatua na utaratibu wa
kisheria kuhusu uvunjwaji au ukiukwaji wa mikataba.
1.KUKIUKA MKATABA AU MAKUBALIANO.
Uvunjaji wa mkataba unaweza kutokea katika njia nyingi. Moja ni ile ya kawaida ambapo mtu huamua kujitoa kwa kusema,kutamka au kuandika kuwa sasa sitafanya hili na lile hata kama lipo katika makubaliano yetu. Pili njia nyingine ya kuvunja mkataba ni pale ambapo mtu hasemi kwa kutamka kwamba sasa sitafanya hili wala lile isipokuwa hatimiza wala hatekelezi kile mlichokubaliana. Ifahamike kuwa mtu anapoingia mkataba na mtu mwingine au kampuni na kampuni au kampuni na mtu sheria inalazimisha kutekeleza kwa usahihi yale yote yaliyokubaliwa katika mkataba huo. Utekelezaji wa baadhi ya masharti na kuacha mengine au kutotekeleza yote kabisa ni uvunjaji au ni kujitoa katilka mkataba kwa mujibu wa sheria. Aidha nasisitiza kuwa ili mtu ajitoe katika mkataba sio lazima aseme kuwa nimejitoa katika mkataba. Kitendo cha kutofuata makubaliano kama yalivyokubaliwa ni kujitoa katika mkataba moja kwa moja.
2.KUMDAI FIDIA ALIYEKIUKA MKATABA AU MAKUBALIANO.
Si vyema mtu akafanya makubaliano na mtu mwingine halafu akapotea bila kutekeleza kile kilichokubaliwa. Ni sababu hii inayonifanya kuwaambia watu kuwadai fidia wale wanaokiuka masharti. Kudai kulipwa fidia baada ya kuvunjwa mkataba ni takwa la kisheria na hivyo si ukorofi kama ambavyo mtu anaweza kufikiri.
Kusoma zaidi BOFYA HAPA
1.KUKIUKA MKATABA AU MAKUBALIANO.
Uvunjaji wa mkataba unaweza kutokea katika njia nyingi. Moja ni ile ya kawaida ambapo mtu huamua kujitoa kwa kusema,kutamka au kuandika kuwa sasa sitafanya hili na lile hata kama lipo katika makubaliano yetu. Pili njia nyingine ya kuvunja mkataba ni pale ambapo mtu hasemi kwa kutamka kwamba sasa sitafanya hili wala lile isipokuwa hatimiza wala hatekelezi kile mlichokubaliana. Ifahamike kuwa mtu anapoingia mkataba na mtu mwingine au kampuni na kampuni au kampuni na mtu sheria inalazimisha kutekeleza kwa usahihi yale yote yaliyokubaliwa katika mkataba huo. Utekelezaji wa baadhi ya masharti na kuacha mengine au kutotekeleza yote kabisa ni uvunjaji au ni kujitoa katilka mkataba kwa mujibu wa sheria. Aidha nasisitiza kuwa ili mtu ajitoe katika mkataba sio lazima aseme kuwa nimejitoa katika mkataba. Kitendo cha kutofuata makubaliano kama yalivyokubaliwa ni kujitoa katika mkataba moja kwa moja.
2.KUMDAI FIDIA ALIYEKIUKA MKATABA AU MAKUBALIANO.
Si vyema mtu akafanya makubaliano na mtu mwingine halafu akapotea bila kutekeleza kile kilichokubaliwa. Ni sababu hii inayonifanya kuwaambia watu kuwadai fidia wale wanaokiuka masharti. Kudai kulipwa fidia baada ya kuvunjwa mkataba ni takwa la kisheria na hivyo si ukorofi kama ambavyo mtu anaweza kufikiri.
Kusoma zaidi BOFYA HAPA



No comments:
Post a Comment