Madiwani
wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, wamemchagua Michael Urio
(Diwani wa Kata ya Kunduchi ), kuwa Naibu Meya Mteule wa Halmashauri ya
Manispaa ya Kinondoni.
Michael
Urio ameshinda uchaguzi wa kiti cha unaibu Meya kwa kura 16 kati ya 26
za wabunge na madiwani wa kinondoni kwenye uchaguzi uliofanyika LEO.
Uchaguzi
huo umefanyika ikiwa ni baada ya kumalizika kwa kipindi cha mwaka mmoja
cha uongozi wa Naibu Meya aliyekuwa madarakani ambaye ni Joseph
Rwegasira.
Uchaguzi
huo wa ndani ya chama cha mapinduzi ulihusisha wagombea wawili ambao ni
Joseph Rwegasira aliyekuwa akitetea kiti chake na Michaeli Urio (Diwani
wa Kunduchi)
Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Urio alisema , “Ninawashukuru sana
waheshimiwa madiwani kwa kuonyesha imani kubwa kwangu, naomba
niwahakikishie kwa kushirikiana na Mstahiki meya tutahakikisha
tunafanyakazi kwa pamoja ili kuwaletea maendeleo wananchi wetu ndani ya
Manispaa yetu ya kinondoni.”
Uchaguzi huo ulisimamiwa na Meya wa Kinondoni Mnyonge Songoro, ambae alikuwa mwenyekiti wa uchaguzi songoro.
Akizungumza
kwa niaba ya chama cha mapinduzi Mwendez wa CCM wilaya ya Kinondoni
Lilian Lwebangila alisema chama cha mapinduzi ni wako,mavu katika
chaguzi na aliwaasa Naibu Meya aliyemaliza muda na huyu alieshinda
kushirikiana katika kuijenga Kinondoni
Makundi
hayakosi ndani ya chaguzi lakini baada ya kumalizika kwa uchaguzi sisi
woote ni wamoja alimaliza na kumponeza Urio kwa kuteuliwa kuwa Naibu
Meya Kinondoni.
Diwani Urio ashinda unaibu Meya Kinondoni
Share This
Tags
# HABARI
Share This
Jiachie Blog
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
A Tanzanian blog operating since 2007, covering Local News, Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers / viewers.
No comments:
Post a Comment