JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


VETA YAKUTANA NA WADAU WA UMEME,VIWANDA NA MAGARI KUJADILI UTEKELEZAJI WA MAFUNZO

Share This



Washiriki wa warsha hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na mwakilishi wa mgeni rasmi ambaye ni mshauri wa mradi huo Bw. Ahmed Athumani.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Soko la Ajira ,Mipango na Maendeleo wa VETA, Ahmed Athuman akizungumza katika warsha ya wadau wadau wa viwanda,umeme na magari kujadili utekelezaji wa mradi wa mafunzo yanayotolewa kwa ushirikiano kati VETA na wadau hao iliyofanyika katika ukumbi wa Giraffee Hoteli jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wadau wakifatilia maada mbalimbali katika kujadili utekelezaji wa mradi wa mafunzo yanayotolewa kwa ushirikiano kati VETA na wadau hao iliyofanyika katika ukumbi wa Giraffee Hoteli jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii
MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)imekutana na wadau wa viwanda,umeme na magari kujadili utekelezaji wa mradi wa mafunzo yanayotolewa kwa ushirikiano kati yake na viwanda.

Akizungumza na wadau wa mamlaka hiyo wakati akifungua warsha hiyo Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Soko la Ajira ,Mipango na Maendeleo wa VETA, Ahmed Athuman alisema moja ya sababu zinazokwamisha ajira kwa vijana nchini ni ukosefu wa mafunzo ya vitendo kwa vijana wanaohitimu katika taasisi mbalilmbali unaosababishwa na kutokukwepo kwa ushirikiano thabiti kati ya Taasisi za Mafunzo na Viwanda.

Amesema kuwa VETA inatoa mafunzo yatakayomuwezesha muhitimu kuajiriwa au kujiajiri kutokana na mafunzo ya vitendo yanayotolewa kutokana na mahitaji yaliyopo nchini 


Ahmed amesema kuwa ushirikiano wa wadau utaleta matokeo chanya kwa vijana kuweza kufanya kazi kutokana mafunzo walioyapata katika taasisi za mafunzo ya ufundi Stadi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad