JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TANZANIA YAPOKEA BILIONI 210 KUTOKA JAPANI

Share This
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile na Balozi wa Japani nchini Bw. Masaharu Yoshida wakibadilishana hati ya mkataba wa mkopo wa Shilingi Bilioni 210 kwa ajili ya mradi wa Umeme kati ya Tanzania na Kenya.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt.Servacius Likwelile na Balozi wa Japani nchini Bw.Masaharu Yoshida wakisaini mkataba wa mkopo. Nyuma yao kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Eng. Omar Chambo, kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Japani Seiji Kihara wakishuhudia tukio hilo katika ukumbi wa Wizara ya Fedha Jijini Dares Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt.Servacius Likwelile akitoa ufafanuzi wa matumizi ya mkopo wa bilioni 210 baada ya kusaini mkataba wa mkopo huo katika ukumbi wa Wizara ya Fedha jijini Dar es Salaam.

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesaini mkataba na Serikali ya Japani kiasi cha shilingi Bilioni 210 kwa ajili ya maendeleo ya mradi wa njia ya kusafirishia umeme kati ya Tanzania na Kenya ambao utasaidia upatikanaji wa umeme wa kutosha.

Mkataba huo wa masharti nafuu ulisaininiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile na Balozi wa Japani nchini Tanzania Bw. Masaharu Yoshida jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kusaini mkataba huo Dkt. Likwelile alisema kuwa fedha hizo zitaelekezwa katika kusambaza nyaya za umeme zenye KV400, na urefu wa kilometa 414.5 kati ya Singida na Namanga kupitia Babati na Arusha.

Alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kutachochea maendeleo ya jamii na uchumi nchini kwa kuleta muungano wa kibiashara katika nchi za Afrika Mashariki.

Naye Balozi wa Japani nchini Tanzania Bw. Masaharu Yoshida alisema kuwa mkopo huo utafanikisha kusambaza nyanya za umeme zenye urefu wa takribani kilometa 508 kati ya Tanzania na Kenya ambapo Tanzania itasambaza kilometa 415 wakati Kenya itakuwa na kilometa 93.

Japani imekuwa ikisaidia Tanzania katika miradi ya umeme kwa muda mrefu, miradi ambayo tayari imekamilika ni pamoja na usambazaji umeme Zanzibar, mradi wa usambazaji nyaya za umeme mkoani Kilimanjaro na mradi wa kutengeneza nyaya mpya za umeme jijini Dar es Saalam.

IMETOLEWA NA WIZARA YA FEDHA
KITENGO CHA MAWASILIANO 

16/12/2015.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad