JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MFUMO WA KIMTANDAO UNAOWEZESHA KUPOKEA NA KUHAMISHA MIAMALA YA KIFEDHA KUTOKA BENKI MOJA KWENDA NYINGINE UNAORATIBIWA NA BENKI KUU YA TANZANIA (BOT)

Share This
 MFUMO WA KIMTANDAO UNAOWEZESHA KUPOKEA NA KUHAMISHA MIAMALA YA KIFEDHA KUTOKA BENKI MOJA KWENDA NYINGINE UNAORATIBIWA NA BENKI KUU YA TANZANIA (BOT)  YAANI ‘TANZANIA INTER-BANK SETTLEMENT SYSTEM’ (TISS) WAONGEZA UFANISI KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM
 Kaimu Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Bw. Hebel Mhanga, akibadilishana mawazo na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Bw. Gabriel Migire, leo asubuhi kabla Kaimu Katibu Mkuu hajaongea na waandishi wa habari pamoja na wadau kuhusu mafanikio yaliyopatikana kwa kuongeza muda malipo ya kibenki kupitia mfumo wa TISS.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Bw. Gabriel Migire (wa tatu kutoka kushoto), akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) na wadau mbalimbali, kuhusu mafanikio yaliyopatikana kwa kuongeza muda malipo ya kibenki kupitia mfumo wa TISS.
 Wadau mbalimbali wa Bandari ya Dar es Salaam na waandishi wa habari wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Bw Gabriel Migire (hayupo pichani) wakati akieleza mafanikio yaliyopatikana kwa kuongeza muda malipo ya kibenki kupitia mfumo wa TISS, leo asubuhi katika ofisi za Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania(TPA).
 
 Mkurugenzi wa mfumo wa malipo kitaifa wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Bw, Benard Dadi, akieleza mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa kuongeza muda wa malipo ya kibenki kupitia mfumo wa TISS, leo asubuhi katika Ofisi za Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA). Mkurugenzi huyo ameziomba benki kukubali kupokea na kuhamisha malipo kupitia mtandao wa TISS kwa zaidi ya muda wa awali wa ukomo ambao ulikuwa saa saba mchana.
Kamishna wa Forodha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Tiagi Kabisi, akieleza namna mifumo mbalimbali inayotumiwa na Mamlaka ambayo imeunganishwa na Mfumo wa TISS ilivyoongeza mapato na kurahisha huduma mbalimbali za malipo, leo asubuhi katika Ofisi za Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).
 (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad