tamasha la bongo 50 lafana vilivyo usiku huu,kila mmoja auga mwaka kwa aina yake.!

Saturday, December 31, 2011
Sir Juma Nature akiliongoza kundi lake la Wanaume Halisi kutoka Temeke,akikamua jukwaani usiku huu kwenye tamasha la Bongo 50,ndani ya viwanja Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar,ambapo wakazi wa jiji hilo na vitongoji vyake walijumuika pamoja katika mpango mzima wa kuuaga mwaka kwa shangwe,tamasha hilo limedhaminiwa na kampuni ya simu za mikononi ya Airtel,kupitia huduma yake mpya ya Airtel Money.
Mmoja wa wasanii kutoka kundi la Wanaume Halisi Jb akikamua jukwaani.
Wasanii wa muziki wa kizazi kipya,Mwana FA sambamba na Mwanadada Linah kutoka THT wakiimba kwa pamoja wimbo wao 'Yalaiti'.ambao kwa mara kwanza uliimbwa na mwanamuziki Mkongwe nchini,Bibi Kidude lakini wao wakaimba remix.
Mwanadada Linah akiwarusha vilivyo mashabiki wake usiku huu kwenye tamasha la Bongo 50,ikiwemo na kuusubiria mwaka mpya.

Mkali wa mashairi,Simba Mzee a.k.a Uncle Virus Afande Sele akikamua viulivyo usiku huu mbele ya mashabiki wake waliopagawa vilivyo,huku wakiungoja Mwaka mpya kwa hamu kubwa.

Watu walijitokeza kwa wingi usiku huu kwenye tamasha la Bongo 50 lilodhaminiwa na kampuni ya simu za mikononi ya Airtel kupitia huduma yake mpya ya Airtel Money iliyozinfuliwa hivi karibuni jijini Dar.

Uncle Virus,Afande Sele akiwarusha vilivyo mashabiki wake usiku huu.

Wadau,Pichani kulia Sebastian Maganga kutoka Clouds FM na rafiki yake nao walikuwepo kuuaga Mwaka 2011 na kuukaribisha mwaka 2012 ndani ya tamasha la Bongo 50,kwenye viwanja vya Lidaz Club.





Watu mbalimbali wakiuaga mwaka kwa staili yao,mara ilipotimu saa sita kamili kabaaaaa....fataki na mayowe,shangwe kama kawaida.







Msanii mdogo kiumri lakini kipaji cha usanii kimekaa mahali pake,anaitwa Asley anayetamba na wimbo wake Naenda Kusema,akijiachia jukwaani na miondoko ya kiduku huku akiwakuna vilivyo washabiki na wapenzi waliokusanyika usiku huu kwenye viwanja vya lidaz Club,jijini Dar ambako tamasha la Bongo 50 linafanyika kwa udhamini mkubwa wa kampuni ya simu ya mikononi ya Airtel. 
 
Mmoja wa Ma-Dj  Mahiri kutoka Clouds FM,Dj Zero akikamua vilivyo jukwaani na kuwarusha mashabiki kibao waliofika kwenye uwanja wa lidaz club katika mpango mzima wa kuuaga mwaka.
Washabiki wakiendelea kufuatilia makamuzi yanayoendelea jukwaani hivi sasa,wakati huo huo walioko majumbani wanaweza kuangalia onesho hili kupitia Clouds TV.
Wasanii wa kundi la Uswahilini Matola wakitumbuiza jukwaani hivi sasa na wimbo wao wa Kosa la Marehemu
Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar na vitongoji vyake wakiendelea kujitokeza usiku huu kwenye viwanja vya lidaz club,ambako tamasha la Mkusanyiko wa wasanii Bongo 50 concert linafanyika,pia ikiwa ni sehemu ya kuuaga mwaka 2011 na kuukaribisha mwaka mpya.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI MAAMUZI YA KAMATI YA UTANDAJI CUF 30 – 31 Desemba, 2011

*TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI*


Kamati ya Utendaji ya Taifa ya Chama Cha Wananchi (CUF) imefanya kikao
chake cha kawaida cha siku mbili mjini Zanzibar tarehe 30 – 31
Desemba, 2011 chini ya Katibu Mkuu wa Chama, Maalim Seif Sharif Hamad.



Pamoja na kujadili ajenda kadhaa za kawaida kuhusiana na mambo ya
utendaji katika Chama, Kamati ya Utendaji ya Taifa pia ilipata nafasi ya
kupokea taarifa ya kina kuhusu hali ya kisiasa ndani ya Chama kutoka kwenye
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Chama kupitia Kamati yake Ndogo ya Nidhamu na
Maadili. Taarifa hiyo ilijikita zaidi katika njama zinazoendeshwa na
wanachama 14 wakiongozwa na Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed zenye
mwelekeo wa kutaka kukivuruga Chama.



Kamati ya Utendaji ya Taifa imeridhika kwamba kuna hoja za msingi na
ushahidi wa kutosha dhidi ya wanachama hao 14 unaoonesha kuhusika kwao
na njama hizo. Wanachama hao ni:



1. Hamad Rashid Mohamed2. Doyo Hassan Doyo
3. Shoka Khamis Juma
4. Juma Said Saanani
5. Yasin Mrotwa
6. Mohamed Albadawi
7. Mohamed Masaga
8. Doni Waziri
9. Yusuf Mungiro
10. Nanjase
11. Ahmed Issa
12. Tamim Omar
13. Amir Kirungi
14. Ayubu Kimangale



Kwa mujibu wa Katiba ya Chama, kifungu cha 63 kinachozungumzia Wajibu
wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa, kifungu cha 63 (1) (d) kinafafanua
wajibu huo kuwa ni “kulinda na kuendeleza heshima ya Chama na Serikali zote
halali za nchi.” Kifungu cha 63 (1) (j) kinaelezea wajibu mwengine kuwa ni
“kuwachukulia hatua za nidhamu viongozi na wanachama wanaoshutumiwa
kwa makosa mbali mbali kwa kufuata masharti ya Katiba hii na kanuni
zitakazotungwa mara kwa mara kwa mujibu wa katiba hii.”



Kwa kuzingatia hali hiyo, Kamati ya Utendaji ya Taifa imeridhika
kwamba kuna haja ya kutumia uwezo iliopewa chini ya kifungu cha 62 (1) cha
Katiba ya Chama kuitisha kikao cha dharura cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa
la Chama ili kutafakari hali hiyo, kusikiliza tuhuma zinazowakabili
wanachama hao, kuwapa nafasi ya kuwasiliza na kujitetea na kisha kuchukua hatua
kama litakavyoona inafaa.



Kikao hicho cha Baraza kuu la Uongozi la Taifa kitafanyika Zanzibar,
tarehe 04/01/2012 katika ukumbi wa hoteli ya Mazson.



Kamati ya Utendaji ya Taifa inawaomba wanachama na wapenzi wote wa CUF
kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hiki na kutoa nafasi kwa vikao
vya Chama kutekeleza wajibu wake kwa mujibu wa Katiba ya Chama.



HAKI SAWA KWA WOTE
 Imetolewa na;



JULIUS MTATIRO,
NAIBU KATIBU MKUU (TANZANIA BARA),
KATIBU WA KAMATI YA UTENDAJI TA TAIFA (CUF NATIONAL CENTRAL
COMMITTEE).
31 Disemba 2011,
ZANZIBAR.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

tamasha la bongo 50 kwenda live clouds tv jioni ya leo.!

Meneja Uhusiano wa kampuni ya simu ya mikononi ya Airtel,Jackson Mmbando akiwa na baadhi ya waandaaji wa tamasha la kufunga mwaka la bongo 50 wakigawa CD zenye nyimbo za wasanii mbalimbali wanaounda umoja wa BONGO 50. wateja 2000 wa kwanza kuingia kwenye uwanja wa liders wanapatiwa CD 1 ya BONGO 50 kama zawadi  
Gari mpya ya kurushia matangazo ya LIVE ya Clouds TV (OB-VAN) ikiwa imepaki katika maeneo ya viwanja vya Lidaz Club Kinondoni jijini Dar,Gari hiyo itatumika kurushia shamra shamra zote zitakazokuwa zikifanyika kwenye viwanja hivi jioni ya leo ,ambapo tamasha la mkusanyiko wa wasaniii Bongo 50 Concert litakuwa likifanyika kwa udhamini mkubwa wa kampuni ya simu ya mikononi ya Airtel kupitia huduma yake mpya ya Airtel Money iliozinduliwa hivi karibuni jijini Dar.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

rais dr shein atoa SALAMU ZA MWAKA MPYA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza ola Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akitoa salamu za kuukaribisha mwaka mpya wa 2012  Biladiya,  kwa wananchi wa Zanzibar na Watanzania kwa ujumla,na  kuwatakia amani na utulivu pia amewataka wananchi kuiunga mkono Serikali yao kwa michango mbali mbali kuliletea maendeleo ya Taifa letu. Picha na Ramadhan Othman IKULU.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

serikali ya zanzibar yaahidi kuendelea kuimarisha miundombinu na uborawa huduma za jamii

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
     Zanzibar                                                                                           
   31.12.2011
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar katika mwaka 2012 itaendelea kuimarisha miundombinu na ubora wa huduma za jamii zikiwemo elimu, afya na maji safi na salama ili kwa pamoja visaidie kufikia lengo la kukuza uchumi na kupunguza umasikini, bila ya kuisahau dhamira kuu ya Mapinduzi ya Kilimo.
 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein aliyasema hayo leo  Ikulu mjini Zanzibar, katika risala aliyoitoa ya kuukaribisha mwaka mpya wa 2012, AD na mwaka 1433 AH kwa wananchi wa Zanzibar na Watanzania wote kwa jumla.
 
Katika risala yake hiyo, Dk. Shein alieleza kuwa katika mwa 2012, Serikali itaongeza ushirikiano na sekta binafsi katika kuchangia ukuaji wa uchumi na huduma za jamii.
 
Alieleza kuwa katika kukabiliana na athari za uchumi wa dunia hususan ongezeko la bei ya chakula, Serikali imejidhatiti kukabiliana na tatizo hilo kwa kuimarisha sekta ya kilimo ili kuongeza uzalishaji na tija kwa wakulima.
 
Akieleza mipango ya kiuchumi kwa mwaka 2012 Dk. Shein alisema kuwa Serikali inaazimia kuzidi kuongeza ukusanyaji wa kodi na kuimarisha mazingira ya uwekezaji ili kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.
 
“Serikali yenu inapanga mipango bora zaidi ya kuiendeleza sekta ya Utalii ili kuhakikisha kuwa kila mmoja wetu anafaidika na sekta hii, huku tukiwa makini juu ya athari zake, na kwa hivyo kuulinda utamaduni, mila na silka zetu”alisema Dk. Shein. Alisema kuwa mazingira ya Utumishi bora katika kuwatumikia wananchi yatazidi kuimarishwa ili iwe chachu ya maendeleo ya haraka na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. 
 
Alieleza kuwa masuala mengine yanayopaswa kukubushwa na kuyazingatia ni matukio makubwa ya Kitaifa likiwemo mchakato wa Katiba mpya ambapo ushiriki wa kila mmoja unahitajika na kuwanasihi wananchi wote kujitokeza kwa wingi katika kutoa maoni yao wakati utakapofika.
 
Aidha, alieleza jambo jengine la pili ni Sensa ya Taifa ya Watu na Makaazi, ambalo nalo ni tukio muhimu nchini kwani inapojulikana idadi ya watu ndipo upangaji bora wa huduma za uchumi na jamii unavyofanyika kwa ufanisi.
 
Kutokana na umuhimu huo wa Sensa, alitoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano katika zoezi hilo muhimu na kuwataka kuondoa hofu katika kujibu maswali watakayoulizwa na maafisa wa Sensa katika zoezi hilo litakalofanyika tarehe 26 Agosti, 2012.
 
Dk. Shein alisisitiza kuwa katika kuelekea mwaka 2012 kuna mambo muhimu ya kuyazingatia na kuyatekeleza ipasavyo kwa ustawi wa maendeleo ya nchi ikiwa ni pamoja na kuimarisha amani na utulivu. Jambo jengine ambalo Dk. Shein alilitaja ni kuongeza jitihada katika kukabiliana na vitendo vinavyosababisha uharibifu wa mazingira na kushusha hadhi na haiba ya mji.
 
Kutokana na hali hiyo Dk. Shein aliwataka wananchi wote kushirikiana na viongozi, taasisi za serikali na zisizo za Kiserikali katika kuondoa taka, kuzuwia uchimbaji ovyo wa mchana, uzururaji wa wanayama mijini na kuimarisha upandaji miti. Pia, alisisitiza kuondoa kabisa vitendo vya uzalilishaji wa kijinsia hasa ubakaji na kueleza kuwa tatizo hilo linafedhehesha sana na ni kinyume cha maadili ya Kizanzibari.
 
Sambamba na hayo, alisema kuwa licha ya kuwepo changamoto mbali mbali katika ukuaji wa uchumi nchini na kupanda kwa bei ya bidhaa duniani mafanikio makubwa yamepatikana katika ujenzi wa skuli maalum za Sekondari za Wilaya Unguja na Pemba ambazo zimejengwa kwa kipindi cha mwaka mmoja badala ya miaka mitano.
 
Pia, alisema kuwa serikali imekamilisha ujenzi wa barabara kadhaa Unguja na Pemba pamoja na kuwapatia pembejeo za kilimo, mbolea,dawa na huduma za mashambani wakulima kwa bei nafuu zaidi. Dk. Shein alisema kuwa huu ni wakati wa kutafakari matukio ya mwaka unaomalizika na kasha kupanga mikakati ya kuimarisha mafanikio yaliopatikana na kuibua mbinu mpya za kukabiliana na changamoto zilizopo.  “Tutajifunza kuwa papo kwa papo kamba hukata jiwe, hivyo tunapaswa kujipanga upya ili tufanye vizuri zaidi mwaka unaokuja”,alisisitiza Dk. Shein.
 
Dk. Shein pia, alitumia fursa hiyo kutoa shukurani kwa wakulima wa karafuu kwa kuziuza katika vituo vya Shirika la Biashara la Taifa (ZST) pamoja na kutoa pongezi kwa Kikosi Kazi kinachosimamia karafuu chini ya uongozi wa Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko, Wakuu wa Mikoa na Makamanda wa vikosi vya SMZ na SMT.
 
Pia, alieleza imani yake kuwa kasi  ya mabadiliko ya maendeleo itakuwa maradufu katika mwaka mpya wa 2012.
 
Rajab Mkasaba,Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

jiachie na tmtv kwa raha zako.


Watch TMTV Tanzania Music Television Everyday Via Our site by following the Link Below http://www.eastafricanhit.com/TMTV Or you can Click On our Home page where you see a banner says TMTV . Much Thanks. Share with you Friends .  

 
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

RAIS KIKWETE, LEO AMUAPISHA BALOZI SEFUE KUWA KATIBU MKUU KIONGOZI, BADALA YA LUHANJO

Rais Jakaya Kikwete, Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue, wakipiga picha ya pamoja na Makatibu wakuu, baada ya hafla hiyo ya kumuapisha Katibu Mkuu Kiongozi iliyofanyika leo Ikulu Dar es Salaam.
  Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue, wakipiga picha ya pamoja baada ya hafla ya kuapishwa rasmi kwa katibu huyo leo Ikulu Dar es Salaam
 Rais Jakaya Kikwete, akimkabidhi Nyaraka za Serikali, Katibu Mkuu Kiongozi mpya Balozi Ombeni Yohana Sefue, mara baada ya kumuapisha rasmi, leo Ikulu Dar es Salaam.


Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha rasmi, Balozi Ombeni Yohana Sefue, kuwa Katibu Mkuu Kiongozi badala ya Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Phillemon Luhanjo, aliyemaliza muda wake. Hafla hiyo ya kumuapisha Balozi Sefue, imefanyika leo Ikulu Dar es Salaam. Wa pili (kushoto) kwa Rais ni Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Phllemon Luhanjo, akisimamia zoezi hilo.
Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Phillemon Luhanjo (kushoto) akimkabidhi nyaraka za serikali maalum kwa kuapishiwa na Biblia, Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue, ili kuanza kuapishwa rasmi na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu Dar es Salam leo.
Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue (kushoto) akifurahia jambo na Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Phillemon Luhanjo, wakati wa hafla hiyo ya kuapishwa katibu Mkuu kiongozi Ikulu Dar es Salaam leo
Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Phillemon Luhanjo, akihojiwa na waandishi wa habari, mara baada ya kumalizika kwa hafla hiyo ya kumuapisha Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue Ikulu Dr es Salaam leo.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue na Balozi Kiongozi Mstaafu, Phillemon Luhanjo, wakizungumza jambo baada ya hafla ya kuapishwa rasmi kwa katibu huyo leo Ikulu Dar es Salaam.
Balozi Ombeni Yohana Sefue, akiwa ukumbini wakati akisubiri kuapishwa rasmi kushika madaraka ya Katibu Mkuu Kiongozi badala ya Phillemon Luhanjo, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika leo Ikulu Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiingia katika ukumbi wakati wa hafla fupi ya kumuapisha Katibu Mkuu Kiongozi mpya, Balozi Ombeni Yohana Sefue, aliyeapishwa  na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu Dar es Salaam leo. Picha Ikulu na Muhidin Sufiani-OMR
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

Happy birthday mdau babu tale.

Mdau Babu Tale, leo anatimiza miaka kadhaa tangu kuzaliwa kwake,ambapo bia anasubiria masaa tu kuuaga mwaka 2011 na kuukaribisha mwaka 2012.Blogu ya Jiachie inamtamkia afya njema na  kila lakheri katika kuuaga mwaka 2011.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

RAIS KIKWETE AKIWA NA KATIBU MKUU KIONGOZI MSTAAFU NA MPYA


Rais Jakaya Kikwete akiongea na Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu Mh Philemon Luhanjo (kulia) na Katibu Mkuu kiongozi mteule Balozi Ombeni Sefue ofisini kwake Ikulu Dar es salaam (jana) Ijumaa usiku mara baada ya kufanya uteuzi huo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

gazeti la michezo heka heka uwanjani liko sokoni leo kwa sh 400/= tu.



 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

kibanda ajiuzuru kuwa mjumbe wa kamati ya taifa ya mchakato wa kupata vazi la taifa.



KUJIUZURU KWA BW. ABSALOM KIBANDA KAMA MJUMBE WA KAMATI YA TAIFA YA MCHAKATO WA KUPATA VAZI LA TAIFA.

Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo imepokea kwa masikitiko taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya Habari na Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Free Media Bw. Absalom Kibanda ya kujitoa kwenye Kamati ya Taifa ya kukamilisha mchakato wa kupata vazi la Taifa, Wizara haina pingamizi na uamuzi wake huo. 

Wizara imesikitishwa na sehemu ya tamko lake kudai kuwa namnukuu,
“Nimelazimika kufikia uamuzi huu, baada ya kujiridhisha pasipo shaka kwamba mchakato mzima uliohusisha sakata langu kama Mhariri Mtendaji kuhojiwa na kufunguliwa mashitaka na Polisi na hatimaye kufikishwa kwangu Mahakamani usingeweza kufikiwa pasipo kuishirikisha Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo inayoongozwa na Waziri Nchimbi”, mwisho wa nukuu. 



Kwa taarifa hii Wizara inapenda kuutarifu umma kuwa Habari hiyo ni uzushi usio na mashiko wenye nia ya kuharibu uhusiano mzuri uliopo kati ya Wizara na wadau wa  Habari nchini.

Kwa mujibu wa majukumu ya Wizara, si sehemu ya kazi za wizara hii kushauri, kuchunguza au kuandaa tuhuma za makosa ya jinai. Ni vema iwe wazi kuwa Wizara hii, viongozi , watendaji,  na watumishi wake hawajashiriki, hawajashirikishwa na hawajajishirikisha na hawajashauri wala kushauriwa juu ya tuhuma na mashitaka dhidi ya Bw. Kibanda.

Wizara inavisihi vyombo vya Habari kuendelea kuzingatia weledi, mila na desturi zetu katika kutekeleza majukumu yake.



Imetolewa na,
Msemaji wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Tarehe 29/12/2011.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, December 31, 2011 | | Permalink | Maoni 1

rais kikwete amteua balozi Ombeni sefue kuwa katibu mkuu kiongozi,kuapishwa kesho.

Friday, December 30, 2011
 UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116539
E-mail: press@ikulu.go.tz
Website: www.mawasilianoikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Balozi Ombeni Yohana Sefue kuwa Katibu Mkuu Kiongozi.

Balozi Sefue anachukua nafasi inayoachwa wazi na Bwana Phillemon Luhanjo ambaye anahitimisha mkataba wake wa utumishi wa umma kesho, Jumamosi, Desemba 31, 2011.

Kabla ya uteuzi wake, Balozi Sefue alikuwa Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York, Marekani. Kabla ya hapo, Balozi Sefue alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani na kabla ya hapo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Canada tokea Oktoba 2005.

Balozi Sefue ataapishwa kesho, Jumamosi, Desemba 31, 2011 saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

30 Desemba, 2011
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 30, 2011 | | Permalink | Maoni 0

TAARIFA MUHIMU KWA WATEJA WA DAWA YA KUKATA TUMBO WALIOPO JIJINI DAR ES SALAAM.


TAARIFA  MUHIMU  KWA  WATEJA  WETU  WA  
DAWA  YA   KUKATA  TUMBO ( KITAMBI )  WALIOPO  JIJINI  DAR  ES  SALAAM

NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOOD  CLINIC , WAUZAJI  WA  DAWA   SAFI  YA  ASILI  YA  KUKATA  TUMBO,  TUNAPENDA  KUWATAARIFU  WATEJA  WETU  WAPENDWA  KUWA  KWA  SASA TUMESOGEZA  HUDUMA  YETU  KARIBU  ZAIDI  NA  WATEJA  WETU  KWANI  KUANZIA  TAREHE  27/12/2011 . TUNAPATIKANA  KATIKA  HOTELI  YA  ROMBO  GREEN  VIEW  HOTEL  ILIYOPO  KATIKA  ENEO  LA  SHEKILANGO. SIKU  ZA  KAZI  NI  JUMATATU  HADI  JUMAOSI  KUANZIA  SAA  MBILI  KAMILI  ZA  ASUBUHI  HADI  HADI  SAA   MBILI  KAMILI  ZA  USIKU.

Kwa  maelezo  zaidi wasiliana  nasi  kwa  SIMU: 0767010756  au   tutembelee  katika  blogu  yetuhttp://www.neemaherbalist.blogspot.com//
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 30, 2011 | | Permalink | Maoni 4

NGOMA AFRICA BAND AKA FFU YATOA SALAM ZA HERI YA MWAKA MPYA 2012


NGOMA AFRICA BAND AKA FFU
YATOA SALAM ZA HERI YA MWAKA MPYA 2012    

Kwa Wadau wote! Happy New year               

Bendi ya muziki wa dansi Ngoma Africa band aka FFU yenye makao yake Ujerumani, Inatoa salam za heri ya mwaka mpya 2012 kwa wadau wote,mabibi na mabwana,wakubwa na watoto popote pale duniani. Tuna watakia kila la heri na baraka za mwaka mpya 2012 ,afya njema,maisha bora,furaha, amani,upendo na mshikamano.
Happy New Year 2012
 
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 30, 2011 | | Permalink | Maoni 0

VODACOM KUWAKUMBUKA MCHUKA NA NGAHYOMA

Vodacom yatoa pole vifo vya wanahabari Marehemu Halima Mchuka na John Ngahyoma.

Dar es salaam Disemba 30, 2011. Kampuni ya simu ya mawasiliano ya Vodacom imepokea kwa mshtuko na huzuni kubwa taarifa za vifo vya wanahabari nguli nchini Bi. Halima Mchuka na Bw. John Ngahyoma.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana, wanahabari hao wamefariki kwa siku tofauti akianza Halima juzi na baadae Ngahyoma aliyefariki asubuhi ya leo wote jijini Dar es salaam.

“Tunatoa mkono wa pole kwa familia za marehemu, waajiri wao na kipekee familia ya wanahabari nchini kwa kuondokewa na wapendwa wetu ambao walikuwa sehemu muhimu ya ujenzi wa tasnia ya habari na utangazaji nchini.”Alisema Ofisa Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Bi. Mwamvita Makamba.

Marehemu Bi. Halima Mchuka alikuwa mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania – TBC na Marehemu Bw. John Ngahyoma hadi umauti unamkuta alikuwa ni mwanahabari wa Shirika la Utangazaji la Uingereza – BBC Ofisi ya Tanzania.

Marehemu wote wawili watakumbukwa kwa jinsi ambavyo walikuwa mahiri katika tasnia ya habari na utangazaji kwamba mchango wao utaendelea kuwa chachu hasa kwa vizazi vijavyo vya wanahabari chipukizi nchini.

“Tutamkumbuka sana Marehemu Halima ambae rekodi zinaonyesha kuwa ni mtangazaji wa kwanza mwanamke kutangaza mpira. Marehemu Ngahyoma kwa upande wake ni sehemu ya watangazaji wa awali kabisa wa televisheni Tanzania Bara mwanzoni mwa miaka ya tisini”Alisema Mwamvita.

Mwamvita amesema kampuni ya Vodacom daima ina thamini na kuheshimu mchango wa wanahabari katika maendeleo ya taifa na ushamirishaji ustawi wa jamii

Mungu azilaze roho za Marehemu Bi Halima Mchuka na Bw. John Ngahyoma mahali pema peponi - Amen
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 30, 2011 | | Permalink | Maoni 0

WASANII WA AIRTEL BONGO 50 NA AIRTEL WATOA POLE NA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO DAR LEO

Meneja Mawasiliano wa kampuni ya simuya Airtel ,Jackson Mmbando akizungumza kuhusiana na utoaji wa msaada uliotolewa na kampuni hiyo kwa kushirikiana pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-,pichani kati ni Meneja Masoko wa Airtel,Rahma Mwapachu.
Msaani wa filamu/muziki ajulikanae kwa jina kisanii Shilole akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-
Wasanii wa muziki wa kizazi kipya   ‘Bongo Flava’ wa Kundi la Wanaume Halisi wakiongozwa na mkali Juma Nature na  wakikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko jijini Dar es salaam waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-
Meneja Masoko wa Airtel,Rahma Mwapaju akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-
Ofisa Rasilimalii Watu wa Airtel,Dada Doris Kibasa aliyeongozana na wafanyakazi wengine wa Airtel  na wasanii muziki wa Bongo Flava akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-
Msanii  mkongwe nchini katika muziki wa Bongo Flava Jafarai akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-
Ofisa Rasilimalii Watu wa Airtel, Dada Doris Kibasa aliyeongozana na wafanyakazi wengine wa Airtel  na wasanii muziki wa Bongo Flava akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-  
Kiongozi wa bendi ya Muziki wa dansi,Ally Choki akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-
Mtayarishaji wa Muziki (Producer) wa Bongo Flava mkongwe P Funk akikabidhi sehemu ya msaada pamoja na umoja wa wasanii wa Airtel Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-
Msanii chipukizi nchini katika muziki wa Bongo Flava maarufu Asley akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-
Msanii  mkongwe nchini katika muziki wa Bongo Flava maarufu Q Chif akikabidhi sehemu ya msaada uliotolewa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel pamoja na umoja wa wasanii wa Bongo 50 kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Lugimbana maalum kwa waathirika wa mafuriko waliokusanyika katika kituo cha Hananasifu kilichopo Kinondoni, Wasanii hao pamoja na Airtel wametoa msaada huo leo vikiwemo vifaa vya nyumbani zikiwemo nguo na vyakula vyote vinathamani ya Shilingi milioni 10/-
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, December 30, 2011 | | Permalink | Maoni 0
Idadi ya watu