Eve E akiwa amepozi kiaina.
wwwoooooowww..! I cant believe it...Eve..!
Msanii Alpha akitimiza moja ya ndoto zake katika anga ya muziki.
Waratibu na wadhamini wakiwa katika picha pamoja na wanamuziki watakaotumbuiza kwenye tamasha la Tusker All Stars 2011,kwenye viwanja vya Carnivo hapo kesho,tamasha hilo linatarajiwa kuanza mapema mnamo saa nane mchana na kuendelea,aidha ndani ya tamasha hilo mtoto mwenye umri chini ya miaka 18 haruhusiwi.
Pichani kulia ni Mkurugenzi wa masoko wa kampuni ya EABL-Kenya ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha la Tusker All Stars,kupitia kinywaji chao cha Tusker akizungumza na Waandishi wa habari kuhusiana na tamasha hilo ndani ya moja ya ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Serena akiwa na wanamuziki wote ambao watatumbuiza kwenye tamasha hilo,ambalo limekuwa na msisimko mkubwa hapa jijini Nairobi.
Mwanamuziki Shaggy akifafanua jambo mbele ya Wanahabari (hawapo pichani) kuhusiana na tamasha la Tusker All Stars 2011,kulia kwake ni Mkurugenzi wa masoko wa kampuni ya EABL-Kenya ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo kupitia kinywaji chao cha Tusker.
Baadhi ya wasanii watakaoshiriki kwenye tamasha la Tusker All Stars 2011 wakiwa kwenye mkutano na wanahabari ndani ya Serena hotel kuhusiana na tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika kesho kwenye viwanja vya Carnivo,jijini Nairobi.Shoto ni Msanii Amani,Jaguar pamoja na Alpha.
Mmoja wa Wakurugenzi wa Clouds Entertainment,Ruge Mutahaba pichani kulia akizungumza jambo na Shaggy leo mchana nje ya hoteli ya Kimataifa,Serena,jijini Nairobi.
Mwanamuziki kutoka nchini Jamaica,anaefanya kazi zake za kimuziki nchini Marekani,Orville Richard Burrell a.k.a Shaggy akiwa amepozi mara baada ya kutia saini bango lenye tangazo la kampeni mpya ya East African Breweries Ltd, iliozinduliwa hivi karibuni kwa ajili ya kuielimisha jamii kuhusiana na suala la ulevi wa kupindukia ijulikanayo kama "Unywaji pombe kistaarabu" ama " RESPONSIBLE DRINKING CAMPAIGN"
Mwanamuziki nyota kutoka nchini Marekani,Eve Jihan Jeffers a.k.a Eve E akitia saini kwenye bango lenye tangazo la kampeni mpya ya East African Breweries Ltd,iitwayo "Unywaji pombe kistaarabu" ama " RESPONSIBLE DRINKING CAMPAIGN"
Msanii kutoka nchini Angola,Ivon Manuel Lemu a.k.a Cabo Snoop, akitia saini kwenye bango lenye tangazo la kampeni mpya ya East African Breweries Ltd,iitwayo "Unywaji pombe kistaarabu" ama " RESPONSIBLE DRINKING CAMPAIGN"
Msanii mmojawapo wa Tusker All Stars 2011 akitia saini kwenye bango lenye tangazo la kampeni mpya ya East African Breweries Ltd,iitwayo "Unywaji pombe kistaarabu" ama " RESPONSIBLE DRINKING CAMPAIGN"
Paparazi wakiwa kazini kunasa tukio hilo leo mchana,pichani Mwanamuziki akiwa ndani ya Tax.
Baadhi ya wanamuziki waliojitokeza kuunga mkono kampeni mpya ya EABL-Kenya ( RESPONSIBLE DRINKING CAMPAIGN),wakiwa wamepozi picha pamoja kwenye baadhi ya Tax zenye kuhamasisha kampeni hiyo jijini Nairobi,kulia ni Davies,Eve E,Peter Msechu,Cabo Snoop pamoja na Shaggy.
Mmoja wa wafanyakazi wa kampuni ya EABL akitoa maelekezo mafupi kwa Wanaumuziki namna kushiriki ama kuunga mkono kampeni mpya ya kupambana na suala zima la ulevi kupindukia.
Pichani kulia ni Mkurugenzi wa Masoko wa EABL-Kenya,Caroline Ndungu sambamba na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo wakiwa na wanamuziki watakaotumbuiza kesho kwenye tamasha la Tusker All Stars 2011,wakitoka nje ya hoteli ya Serena,iliopo katikati ya jiji la Nairobi,Kenya mapema leo mchana kwa ajili ya kuunga mkono kampeni mpya ya Unywaji pombe kistaarabu " RESPONSIBLE DRINKING CAMPAIGN",ambayo nchini Tanzania ilizinduliwa hivi karibuni (kwa picha ya tukio hilo bofya hapa).