Duu..! kuna kiboko lakini hii ni kiboko yake.!

Thursday, March 31, 2011
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 4

Rais Kikwete akutana na Waziri Mkuu wa Zimbabwe ikulu leo jijini dar

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu Zimbabwe Morgan Tsvangirai ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi (Freddy Maro).
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

rais wa zanzibar Dr Shein amwapisha Jaji wa Mahakama Kuu na mwanasheria mkuu wa zanzibar leo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akimuapisha Othman Masoud Othman,kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar,awali alikuwa Mkurugenzi wa mashtaka,hafla hiyo iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akimuapisha Othman Masoud Othman,kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar,awali alikuwa Mkurugenzi wa mashtaka,hafla hiyo iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar jana.Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

mjadala wa kikombe Live na clouds FM leo.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

Mbio za Ngorongoro kufanyika Aprili 4 Karatu.


Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo kwa kushirikiana na WellShare International inadhamini mashindano ya mbio za riadha za nusu Marathoni zinazoitwa “Mbio za Ngorongoro” zitakazofanyika april 4 katika Wilaya ya Karatu. Mbio hizi zina lengo la kupiga vita ugonjwa wa Malaria.

Akiongea na waandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam, Afisa Uhusiano wa Tigo Jackson Mmbando (Pichani) alisema kuwa Mbio hizo ambazo zinafanyika kwa mara ya nne mfululizo chini ya udhamini wa Tigo, Mwaka huu mbio hizi zitakuwa kama sehemu ya utangulizi wa kuazimisha siku ya Malaria duniani itakayofanyika april 25 mwaka huu mkoani Arusha.

Alisema kuwa wanariadha mmoja mmoja na kama timu watajumuika na jamii ya watu wa Karatu kushiriki mbio hizo ambazo zitaanzia geti la Ngorongoro Crater na kuishia Karatu Mjini. Mwaka jana mbio hizi zilihudhuriwa na watu zaidi ya 5,000 ambapo wakazi wa wilaya ya Karatu walijifunza mambo mbalimbali yahusuyo magonjwa, zaidi ikiwa ni ugonjwa malaria.

Wadhamini wengine ni Shirika La Maendeleo La Watu wa Marekani (USAID), Kampuni ya utalii ya ZARA, A to Z Textiles/Olyset Nets, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Halmashauri ya Wilaya ya Karatu. Halikadhalika wafanyabiashara mbalimbali wa Karatu wakiwemo Jubilee Tyres, Karatu Quality Garage, Bougainvillea Lodge na Octagon Lodge, Happy Days Pub, Karatu Bakery, Shagri-La Estates, pamoja Exim Bank.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

kumekucha maonyesho ya harusi 2011.


UKUMBI WA DIAMOND WAANDALIWA TAYARI KWA MAONYESHO YA HARUSI 2011 YANAYOTARAJIWA KUANZA KESHO TAREHE 1 MPAKA 3 MWEZI APRIL.


Maandalizi motomoto ya Maonyesho harusi kwa mwaka 2011 yanaendelea mchana huu ndani ya ukumbi wa Diamond , huku washiriki wakimiminika ukumbini hapo ili kuhakikisha mabanda yao, na kila kitu kiko sawa.


Hatua za mwisho za maandalizi ya ukumbi huo uliopambwa kwa mabanda ya rangi nyeupe na mazulia mazuri ya kibuluu, inaufanya ukumbi huo kung'aa na kuuweka tayari kwa maonyesho hayo yanayoanza kesho tarehe 1 hadi 3 mwezi April.

Haya ni maonyesho ya aina yake, yanayochukua sura ya kimataifa huku yakitarajiwa kutembelewa na viongozi mbalimbali toka serikalini na sekta binafsi.


Kwa kweli si maonyesho ya kukosa kwa wadau na wale wote wanaotarajia kufunga ndoa hivi karibuni.

Baadhi ya washiriki wa maonyesho wa mwaka huu ni: Lotus Creative Concepts, Nadd House Events Hire, Zanzibar Weddings, Fannina Investments, Endepha Events Planners,Luxe Papers, Paper Designs, Vayle Springs, Upper Zonal Trading, River Blues Tanzania Ltd, MH Gallery,Kinara Mobile Studio, Dar City, Slice of Wedding,Markham Executive Suites,The Flying Chefs, Mustafa Hassanali Wedding, Malaika Event Designs & Rentals, GRM Production, Bluecheriemoe, DIA’s, Metro Fashion, Rose Fashion Designer, TANZANIA HAIR INDUSTRY, NORBROS Collection, Manju Msitta, Caros Cakes& Hot Brades, Moevenpick Royal Palm Hotel, Sheer Illusion and Daily News, nk.


Maonyesho ya Harusi kwa mwaka huu yamedhaminiwa na Clouds FM, Daily News, Habari Leo, Global Outdoor Systems, Image Masters, Ultimate Security, Vayle Springs, Eventlites na 361 degrees.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

NAIBU WAZIRI ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA ZANTEL jijini dar leo.

Ofisa Mkuu wa Tekenorojia Kampuni ya Zantel Bw. Moncef Mettiji wa pili (kulia) akimuonesha moja ya mitambo ya mawasiliano ya Kampuni hiyo, Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Bw. Charles Kitwanga alipotembelea kampuni hiyo Dar es salaam leo kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu Ali Bin Jarsh na kushoto ni Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa wa Zantel, Norman Moyo.(PICHA NA MPIGAPICHA WETU).
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

Matokeo: Maoni ya watu kuhusu tiba ya Babu Loliondo


Habari Bro Michuzi Jr .

Tunashukuru sana kwa kuwekea tafiti yetu kwenye blog yako. Leo ndio ile siku ya kutangaza matokeo. Chini ni ujumbe unaoambatana na link ya kwenye maoni. Pia tumeattach picha ambayo unaweza kuambatanoisha na hii post. Tunatanguliza shukrani mkuu.

.........................................................................................................

MATOKEO : MAONI YA WATU KUHUSU TIBA YA BABU LOLIONDO

Kwa niaba ya Bongo Promotions tunapenda kutoa shukrani zetu kwa wale wote walioshiriki katika survey tuliyoitangaza siku ya jumatatu (28.03.11). Lengo la kufanya huu utafiti mdogo ni kuangalia mitizamo ya wananchi kuhusu tiba ya babu Loliondo.


Tumepata maoni mengi sana kutoka kwa watu zaidi ya 180. Takwimu zinaonyesha wengi wamependekeza kwamba taratibu za kitaalam zifanyike kuthibitisha kama dawa inatibu, wengine wanasema kuwa hili ni suala la imani zaidi. Wapo walio fedheheshwa na juhudi za vingozi kutokuwa za kuridhisha katika kufuatilia suala hili na badala yake wao kuwa ni miongoni wa wanaojitokeza kwenda kupata kikombe. Unaweza kupata maelezo zaidi na report kamili ya hii tafiti ndogo kupitia link hiyo hapo chini.


https://spreadsheets0.google.com/viewform?formkey=dEswRHpxZ3RJSzAzalBDYkVZMEs5N1E6MQ


Tunashukuru kwa ushirikiano wako

BONGO PROMOTIONS Team

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

TAARIFA KWA UMMA

SIKU YA TAIFA YA KUPANDA MITI APRILI MOSI 2011

Tarehe Mosi Aprili kila mwaka ni SIKU YA TAIFA YA KUPANDA MITI. Maadhimisho ya Siku ya Taifa ya Kupanda Miti yalifanyika kwa mara ya kwanza tarehe Mosi Januari mwaka 2001 kutokana na Waraka wa Waziri Mkuu Namba 1 wa mwaka 2000 uliomtaka kila mwananchi kupanda miti kwa manufaa yake.

Kutokana na kiwango cha uponaji wa miti iliyopandwa kuwa kidogo, yaani kati ya asilimia 50 na 60 hasa kwenye maeneo kame kinachosababishwa na kupungua kwa mvua na athari za tabianchi, Waziri Mkuu alitoa Waraka mwingine Namba 1 wa Mwaka 2009, uliobadilisha Siku ya Taifa ya Kupanda Miti kuwa tarehe Mosi Aprili kila mwaka badala ya Januari Mosi. Mwezi Aprili ni mwezi ambao sehemu nyingi nchini zinapata mvua, hivyo ni wakati muafaka wa upandaji miti.

Mwaka jana Siku ya Taifa ya Kupanda Miti iliadhimishwa kitaifa Aprili Mosi kwa mara ya kwanza mkoani Shinyanga. Mwaka huu maadhimisho haya yatafanyika katika ngazi za mikoa yote nchini.

Kiutaratibu tarehe Mosi Aprili ni siku ya uhamasishaji pamoja na kupanda miti michache kama sehemu husika haitakuwa na mvua za kutosha. Kama kawaida, kila Mkoa umepanga siku maalum ya kupanda miti mingi zaidi kufuatana na majira ya mvua kwenye Mkoa husika.

Kwa mfano, Mkoa wa Pwani umepanga kupanda miti tarehe 15 Aprili, 2011. Watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii Makao Makuu watajiunga na wananchi wa Mkoa huo wakati watakapokuwa wanapanda miti katika msitu wa Kazimzumbwi Wilayani Kisarawe.

Maadhimisho ya mwaka huu ni ya pekee kwa maana ni mwaka ambao umetangazwa na Umoja wa Mataifa kama Mwaka wa Kimataifa wa Misitu. Ni mwaka wa kutafakari mchango wa watu wa mataifa yote katika kuilinda misitu na kuitumia kiuendelevu. Ni mwaka wa kuhamasishana kuendeleza uhifadhi na kupanda miti ili misitu iwanufaishe watu wa kizazi hiki na vizazi vijavyo. Kwa hiyo, mwaka huu tutaitumia tarehe Mosi Aprili kuadhimisha Siku ya Taifa ya Kupanda Miti, pamoja na Mwaka wa Kimataifa wa Misitu.

Tukumbuke pia kuwa huu ni mwaka wa kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara. Hivyo, tutaadhimisha siku hii kwa kutathmini tulikotoka, tulipo na tunapokwenda kuhusiana na hali ya misitu. Kila mmoja wetu anatakiwa atathmini athari anazopata kutokana na ufyekaji na uharibifu wa misitu na kuamua kwa dhati kuhifadhi misitu, miti iliyopo nje ya misitu na kuongeza jitihada za kupanda kwa wingi miti ya asili na ya kigeni.

Sera ya Taifa ya Misitu imeweka umuhimu mkubwa katika kuhifadhi na kulinda misitu. Sera hii inahimiza ushiriki wa wananchi na wadau wengine kuihifadhi misitu iliyopo na kupanda miti na kuitunza.Nachuku fursa hii kuwapongeza wananchi ambao wanastawisha miche ya miti bila kutegemea ile inayostawishwa katika bustani za serikali. Kwa sasa asilimia 70 ya miche ya miti yote inayopandwa inatokana na juhudi za wananchi wenyewe wanaoanzisha bustani ndogo zinazomilikiwa na vikundi vya kinamama, vijana, asasi zisizo za serikali, shule, na watu binafsi.

Ili kufanikisha upandaji mti nchini napenda kutumia fursa hii kutoa wito kuwa kila familia ianzishe bustani ndogo yenye miche angalau inayolingana na idadi ya wanafamilia. Kwa kufanya hivyo, ni rahisi kuitunza miche hiyo kwa kutumia maji yanayotumika nyumbani. Na pale inapowezekana, ni vema familia zianzishe bustani kubwa kwa ajili ya biashara hivyo kuwawezesha wananchi wengi kupanda miti.

Wakati mwingine siyo lazima miche yote inayopandwa itoke bustanini. Njia nyingine ya kustawisha miti ni kutumia miche inayojiotea yenyewe ardhini kama maotea. Miche hiyo inapandwa katika sehemu zilizokusudiwa ikiwa bado midogo. Njia hii inatumika hasa kwenye sehemu zenye mvua nyingi na udongo tifutifu.

Njia nyingine ya kuongeza kiwango cha upandaji miti ni kupanda mbegu moja kwa moja ardhini kwa baadhi ya miti. Njia hii inatumika sana katika mikoa iliyoko katika nyanda za juu hapa nchini. Kwa mfano wakulima wa miwati katika mikoa ya Tanga na Iringa wanapanda mbegu moja kwa moja ardhini. Aidha, mikaratusi pia inaweza kupandwa kwa njia hii.

Aina nyingine ya kustawisha misitu ni kutenga na kulinda eneo kutokana na uharibifu wa kimazingira ili mbegu ziote zenyewe (yaani natural regeneration). Njia hii imefanikisha shughuli za kustawisha misitu na malisho ya mifugo mkoani Shinyanga. Wananchi wa Shinyanga wanatumia utaalam wao wa jadi unaojulikana kwa jina la Ngitili wa kutenga maeneo na kuyapumzisha ili mbegu zijiotee zenyewe. Matokeo yake ni eneo husika kubadilika na kuwa msitu.

Ustawishaji misitu kwa kutumia njia ya Ngitili umewawezesha wananchi wa mkoa wa Shinyanga kuongoa zaidi ya hekta 500,000 za ardhi ambayo ilikuwa imeharibika kabisa hapo awali. Kutokana na uzoefu huo, nawaasa wananchi kutumia njia zao za jadi za kustawisha misitu na miti kwenye maeneo yao.

Napenda kuwakumbusha na kuwahimiza kuwa kila mmoja wetu aitunze miti atakayoipanda kwa kuilinda dhidi ya uharibifu wa aina yoyote. Aidha, napenda kuchukua fursa hii kumhimiza kila mwananchi ajenge utamaduni wa kuitumia rasilimali ya misitu kwa njia endelevu kwa kufuata taratibu zilizowekwa kisheria za kuvuna mazao mbalimbali ya misitu.

Baada ya kusema hayo, nawatakia wananchi wote maadhimisho mema ya Siku ya Taifa yaKupanda Miti mwaka 2011
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

Rais wa Zanzibar,Dk Shein na Balozi wa Brazil,Fransisco wakutana ikulu zanzibar leo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akizungumza na Balozi wa Brazil Nchini Tanzania,Fransisco Carlos,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Brazil Nchini Tanzania,Fransisco Carlos,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

Audio ya Njia Panda kuhusu 'uponyaji' wa Loliondo

Kipindi cha Njia Panda kilichorushwa na redio Clouds FM siku ya Jumapili, Machi 27, 2011 kilihusu 'uponyaji' wa Loliondo. Studioni alikuwepo Dada aliyejielezea baada ya kunywa dawa, walikuwemo pia Wachungaji wawili toka madhehebu tofauti ya Kikristo, pamoja na Wataalamu wa Afya, bila kusahau wauliza maswali.

Yeyote aliyekosa kusikia, au anayetaka kujikumbusha, anaweza kukisikia tena mtandaoni.
Linki ni : http://bit.ly/NjiaPandaLoliondo.
Subi.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

SHEAR HAIR & BEAUTY ISSUE 10 OUT NOW!


Je, unamjua Amanda Annan? Amanda ni British Super Model na katika ulimwengu wa ulimbwende anajulikana kama ‘Rebel Niece’, kwa sababu yeye Amanda (Kofi Atta Annan (baba mdogo wa Amanda) ni mdiplomasia toka Ghana ambaye ni mtu wa 7 kuitumikia cheo cha Secretary-General wa United Nations kuanzia 1 January 1997 mpaka 31 December 2006.) amezaliwa kwenye familia ya wasomi, wanasiasa na madiplomasia, lakini alipotimiza umri mdogo wa miaka 17 akajikita kwenye fani ya mitindo, uigizaji na ulimbwende tofauti na matarajio ya wazee wake.

Amanda aliliona jarida la Shear Magazine akiwa matembezini Marekani kwa rafiki yake ambaye in dada yetu wa Kibongo aitwaye Pendo Nyonyi anayeishi Los Angeles. Agent/manager wake akapenda wazo la Amanda kutupatia nasi historia yake kwa ufupi na kuwapa moyo kina dada wa Kibongo mbinu za kujikita katika ulimbwende na kutokukata tamaa katika kufanya kile kitu ambacho moyo unapenda, na pia anaeleza kwa kina kuwa mafanikio hayaji bila kujituma, uvumilivu na ujuzi pia.

Pata nakala yako ya Toleo jipya la Kumi maana liko mitaani sasa uweze kusoma story ya kusisimua ya Amanda, kazi zake alizofanya za kuisaidia jamii ya wanawake Afrika, siri zake za urembo, utunzaji wa mwili, ngozi na nywele. Pia ndani ya toleo hili, utapata kujua historia fupi ya 'Legend' Issa Michuzi katika page maalum ya brothers, mahojiano na Ankal Michuzi amewapa wasomaji historia yake ambayo watu wengi hawaijui na yeye binafsi hajazitoa katika blog yake. Nunua nakala yako sasa kwa TSh.5,000 tu!

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

Vijana FM interviews Twaweza's Rakesh.

Yesterday, we got the opportunity to interview a special friend of our organization, and someone who has inspired a lot of our current projects. Meet Rakesh Rajani, currently the head of Twaweza, which aims to facilitate large-scale, citizen-driven change in Tanzania and greater East Africa. Before founding Twaweza, Rakesh initiated and ran Haki Elimu, a group focused on democratizing education in Tanzania, for more than 6 years.

In general, Rakesh’s experience is extensive in the East African development sphere, ranging from progressive and community-driven media and telecommunications campaigns, to the assessment of learning across public schools. It is therefore with deep enthusiasm and interest that we, at Vijana FM, took this opportunity to interview Rakesh.

The full interview can be found here (click) both in audio and print.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

taarifa ya arobaini ya mzee Alhaji Juma Sindano !

Marehemu Alhaji Juma Sindano enzi za uhai wake.

Shukrani

Famili ya marehemu Alhaji Juma Sindano wa Makumbusho Dar es Salaam. Inatoa shukrani kwa wote walishirikiana nasi kwa namna moja au nyingine kutoka ugonjwa hadi kifo chake shukrani za pekee ziwaendee Prof Mgonda wa Muhimbili Hospitali, Hospitali ya Agha Khan, Dr, Kanabal wa Regency Hospital, kwa kutaka kuokoa maisha ya marehemu baba yetu mpendwa, Mh. Rais Jakaya Kikwete, viongozi wote wa chama na Serikali, wafanyakazi wa Gapco Tanzania Ltd, Wafanyakazi wa MGS Ltd, Wafanyakazi wa Riki Hill Hotel, Wafanyakazi wa Wizara ya Afya Kitengo cha Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua kikuu na Ukoma,Majirani zetu wa makumbusho, ndugu jamaa na marafiki si rahisi kumshuru kila mtu mmoja mmoja tunaomba shukurani zetu za dhati wote mlioshirikiana nasi katika kipindi hiki kigumu.

Hatuna cha kuwalipa mwenyezi mungu ndie atakae walipa

Wainnalilah Rajuhuni

Arobaini ya marehemu itafanyika tarehe 2/04/2011 saa 7 mchana nyumbani kwake Makumbusho Dar es Salaam.

Wote mnakaribishwa.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

funguka na mjadala wa kusaka jibu kuhusiana na kikombe.!

Mwandishi na mtafiti wa masuala ya kijamii Bwa.Chambi Chachage akizungumza na Dr Emmanuel Kandusi mapema leo mara baada ya kumaliza kuzungumza mjadala wa kusaka jibu kuhusiana na mambo mbalimbali ambayo yamekuwa yakiibuka hivi karibuni ikiwemo masuala ya “KIKOMBE”.
Kipindi cha PB kilipokuwa kikiruka LIVE leo asubuhi .

Kipindi cha Power Breakfast leo asubuhi kimeendesha live, mjadala wa kusaka jibu kuhusiana na mambo mbalimbali ambayo yamekuwa yakiibuka hivi karibuni ikiwemo masuala ya “KIKOMBE”.Mjadala huo umefanyika ndani ya hoteli ya Kilimanjaro Kempinsk,jijini Dar.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 2

Job opportunity at Sikika.


Receptionist Opportunity.

Join us in advocating for quality health services for all Tanzanians

Introduction.

Sikika is a Non Governmental Organization that advocates for quality health services for all Tanzanians. The organization works to ensure equitable and affordable quality health care services through social accountability monitoring of health systems at all government levels. For more information please visit us at www.sikika.or.tz.
Sikika seeks to recruit a Receptionist with immediate effect:
Responsibilities;

• Manage front desk, telephone and faxes
• Provide Secretarial and administrative support to logistics
• Track and organize all official correspondences
• Ensure that the office runs smoothly, specifically make timely purchases of drinking water & stationery supplies in liaison with the Office Attendant
• Coordinate printing & photocopying
• Make travel, meeting and other arrangements for Staff
• Assist in processing basic financial documents
• Collaboration with other Staff to ensure implementation of program strategy
• Implement & adhere to lawful instructions by HR & Admin Manager and Executive Director.
Key competencies: (a) Minimum of Diploma in Business Administration/Office Management/Front Office Management/Secretarial. (b) At least three years experience in areas related to your responsibilities. (c) Excellent writing and communication skills. (d) Proficiency in using Microsoft Office (e) Experience working in an NGO will be an added advantage

Remuneration:

An attractive package will be offered to successful candidates.
If you believe you satisfy the above requirements you are encouraged to send: (a) a cover letter explaining why your competencies and experiences are suitable for the job, (b) an updated CV which includes your contact details and (c) the full names and addresses of 3 references.

Send your application papers to:
The Executive Director,
Sikika, P.O Box 12183,
Dar es Salaam, Tanzania
or by e-mail to jobs@sikika.or.tz.
Application Deadline: 14 April 2011.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 1

WAZAMBIA WAZUNGUMZIA LOLIONO KUTOA USHUHUDA NA USHIRIKIANO WA TANZANIA NA ZAMBIA


Kwa hisani ya Mbeya yetu blog.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

Happy birthday sweet husband wake.!

"You walked into my world,and took residence in my soul, You make my heart flutter, With what ever you do and every word you say, I will tell you this from the bottom of my heart, Y ou mean everything to me,you are everything to me, I will forever keep loving you Happy birthday sweet husband
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 4

Mkono mmoja haunizuii 'kukuna' mashabiki Pasaka


Mukubwa ni mlemavu wa mkono mmoja wa kushoto anaodai umekuwa katika hali hiyo kutokana na kudhuriwa kwa uchawi na mama yake wa kambo alipokuwa na umri mdogo.

Anasema akiwa na miaka 12 alipata matatizo hayo kwa kutokea uvimbe wa ajabu na hakuna aliyejua tatizo lilikuwa nini, lakini walibaini kuwa ni mama yake wa kambo ndiye alimroga kutokana na wivu.

Mukubwa anayetamba na wimbo wa 'Mfalme wa Amani', anabainisha kwamba aliugua kwa miaka mitatu na alihaha huku na huko hospitalini hadi kwa waganga wa kienyeji kusaka tiba, lakini hakufanikiwa.Kwa mantiki hiyo, alifikia uamuzi wa kukatwa mkono kwa vile ulikuwa umeharibika.Mukubwa ametoa albamu mbili ambazo ni 'Sijaona Rafiki' na 'Mungu Mwenye Nguvu'.

Mukubwa anasema mama yake huyo wa kambo alikiri kumroga baada ya kuokoka, hivyo amemsamehe. Anasema mkono huop aliokatwa haumzuii kumuimbia Mungu.Mukubwa anasema alihamia Kenya kutokana na msaada wa mwimbaji wa nyimbo za Injili, marehemu Angela Chibalonza, aliyekuwa mshauri wake.

Mukubwa amezaliwa kwenye familia ya watoto tisa, wanaume saba na wanawake wawili, yeye akiwa wa kwanza, ameoa kwa kufunga ndoa na Betty Japhet, Machi mwaka jana.

Wengine watakaoshiriki

Mbali na Mukubwa, wengine watakaoshiriki tamasha la Pasaka mwaka huu ni mwimbaji
wa muziki wa Injili kutoka Zambia, Ephraim Sekeleti. Mgeni rasmi atakuwa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete.

Kiingilio katika tamasha hilo kitakuwa sh. 4,000 kwa viti vya kawaida, viti vya maalumu (B) sh. 10,000 na viti maalumu (A) sh. 20,000. Tiketi za kategoria hiyo hazitauzwa mlangoni. Msama alisema tiketi za viti maalumu vya VIP A zitakazokuwa kama meza za familia, watakaohitaji watalazimika kupiga simu selula 0713 383838, 0786 383838 na 0786 373737 ili kupata tiketi na maelezo kinagaubaga.

Mbali na Sekeleti, wasanii wengine wa nyimbo za Injili watakaopamba tamasha hilo ni Rose Muhando, Upendo Nkone, Bony Mwaitege na wanamuziki kutoka Kenya, Anastazia Mukabwa na Pamela Wanderwa.

Tamasha la Pasaka la mwaka huu litashirikisha waimbaji wa nyimbo za Injili kutoka nchi sita ambazo ni Kenya, Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Afrika Kusini na Zambia. Pia kutakuwa na kwaya mbili kutoka katika nchi hizo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

Tangazo la Ibada ya Kiswahili itakayofanyika April 3rd 2011

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 4

VIDEO YA SITAKI KUUMIZWA (SAJNA FT. LINAH)

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, March 31, 2011 | | Permalink | Maoni 4

EU for more trade and investment in Tanzania, East Africa

Wednesday, March 30, 2011

THE Head of the European Union Delegation to Tanzania, Ambassador Tim Clarke, has called upon European business community to tap the increasing trade and investment opportunities resulting from the East African regional integration.

Speaking at a Business Networking meeting in Dar es Salaam yesterday, Ambassador Clarke said that given its geographic location Tanzania has potential to serve as a gateway to the East African region.

He therefore urged European businesses to see to it that they fully utilize the opportunity for their benefit and that of the country and the EA region as a whole."Implementation of the EAC Common Market, as it evolves, will bring increasing trade and investment opportunities for EU businesses," he said.

The EU, with its Member States, is not only the largest development partner of Tanzania, but EU companies also bring significant investment to Tanzania, Ambassador Clarke said.The Business Networking meeting, which aimed to provide a platform for European business representatives to meet and exchange views on challenges and opportunities of doing business in Tanzania, was organised by the EU Delegation and EU Member States present in Tanzania.

Enlisting achievements made so far, Ambassador Clarke said that institutionally the EU was engaged in several processes aimed at facilitating EAC integration including Economic Partnership Agreement (EPA) negotiations and support programmes to EAC integration.

"In future," he said, "we are seeking to be in more active communication with the business community in East Africa-through the East African Business Council, and at a country level."The EU Head of Delegation also said that EU had initiated a dialogue with the Tanzania Revenue Authority where they had agreed on 13 points of action relating to clarity and transparency of tax regulations such as audit process and the open-ended nature of the TRA interventions.

As a result of the dialogue, Ambassador Clarke revealed, TRA has agreed to invite EU business representative to become a member of their stakeholder consultative meeting which until now has been including only sectoral and national representation. The EU business community is keen to contribute to the policy and regulatory debate and to provide feedback on the ongoing reform process.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, March 30, 2011 | | Permalink | Maoni 0

Rais wa Zanzibar,Dk Ali Mohamed Shein akutana na Msaidizi Mkuu wa mambo ya Afrika wa marekani Kori Wycoff.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,li Mohamed Shein ALi Mohamed Shein,akizungumza na Naibu Msaidizi Mkuu wa Mambo ya Afrika wa Marekani,Kori E.Wycoff,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,li Mohamed Shein ALi Mohamed Shein,akisalimiana na Naibu Msaidizi Mkuu wa Mambo ya Afrika wa Marekani,Kori E.Wycoff,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo.Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, March 30, 2011 | | Permalink | Maoni 0

At the prestigious Kilimanjaro Kempinski Hotel Dar es Salaam, Johnnie Walker takes us through the world of BLACK, RED, GOLD and BLUE label.

Serengeti Breweries Limited (SBL), through its iconic premium Scotch whisky Johnnie Walker conducted the second Johnnie Walker Mentorship Program today. The Johnnie Walker Mentorship mentoring and tasting session is an opportunity to immerse the guests into the unique and sophisticated world of the Johnnie Walker and give them an appreciation of what each of the different variants of the brand is made from, how it is made, how to drink it and in what occasions. This unique journey was seen in the last two sessions, and will be seen through by two trained Johnnie Walker mentors Gerald Hando and Dennis Ssebo. They took the invited guests through the journey of taste in the cool and classic environment of the Kibo ball room Kilimanjaro Kempinski-Dar Es Salaam.

According to the Spirits manager at SBL, Benjamin Mariki, “Johnnie Walker has become more than just a drink. It is something we can all relate to in terms of how far we each have come in our lives; in business, socially and at our jobs, today we come together to celebrate personal achievement and progression.’

The mentorship took guests through Johnnie Walker’s journey right from the brewery to one’s glass, a process that has been appreciated for more than 150 years. The Marketing Director of SBL, Ms. Caroline Ndungu said “As part of Diageo Inc, Serengeti Breweries (SBL) is now the official distributor of the whole range of the House of Walker brands,”

The Johnnie Walker Mentorship Program commenced on the 10th of March at Mlimani City Conference centre and will continue all through till the end of June. In the coming months, the striding man will be paying visits to different cities around Tanzania including; Arusha, Mwanza and Tanga to share the Johnnie Walker experience with a few of the lucky invites in their respective cities.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, March 30, 2011 | | Permalink | Maoni 0

tamasha la Harusi Trade Fair 2011 kufanyika april 3 diamond

Mustafa Hassanali, briefs journalists about the upcoming event of Harusi Trade Fair 2011 which will be held at Diamond Jubilee starting on 1st to 3rd April this year. Left is Markerting Manager of Mustafa Hassanali, Hamis Omary.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, March 30, 2011 | | Permalink | Maoni 0

Bendi ya Mashujaa kuwasha moto Aprili Mosi ndani ya Kijiji Cha Makumbusho.

Kiongozi wa bendi ya Mashujaa Edward Antony a.k.a Jadoh FFU akiongea na waandishi wa habari katika mkutano wao walioufanya leo jijini Dar es Salaam. Pembeni yake ni Meneja wa bendi hiyo Mujibu Khamisi pamoja na Yanick-Sauti ya Radi.
Baadhi ya wanenguaji wa bendi ya Mashujaa wakitoa show kidogo mbele ya waandishi wa habari.
--------
Bendi ya Mashujaa kuwasha moto Aprili Mosi ndani ya Kijiji Cha Makumbusho.

Bendi ya Mashujaa inatarajia kufanya onyesho lake katika kijiji cha Makumbusho jijini Dar es Salaam ifikapo Aprili mosi.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa Habari uliofanyika jijini Dar es Salaam kiongozi wa bendi hiyo Edward Antony almaafu kwa jina la Jadoh FFU kuwa wanatarajia kufanya onyesho lao katika kijiji cha Makumbusho kwa kushirikiana na Kundi la Mapacha Watatu.

"Nawakaribisha sana ndugu zetu wote waje watuunge mkono maana tutafanya onyesho zuri sana ambalo wao wenyewe wanadhihirisha sisi ni wakali, Alisema kiongozi wa kundi hilo.

Onyesho hilo ambalo litaendana na utambulisho wa wasanii wao wapya ambao wanatarajia kutambulisha wapatao saba na kiingilio kitakuwa ni tshs.7,000/=

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, March 30, 2011 | | Permalink | Maoni 1

Tafakuri Yangu Ya Leo; Jenerali Ulimwengu Bakora Ya Watawala Acha Iwaadabishe Tu.


……W’re polite and progressive by day, more tibalist than even the Kenyans by night…..


Ukweli kama huu anaoweza kuusema Jenerali Ulimwengu ndio umewafanya watawala wengi kumwogopa mwanaharakati huyu kushinda hata UKIMWI, nani nchi hii asiyemfahamu Jenerali Ulimwengu? Licha ya mwandishi huyu kukumbwa na misukosuko hata ya kutaka kunyang’anywa uraia aah wapi Bwana! Jenerali Ulimwengu hana mpinzani kwa jinsi anavyosimamia ukweli.


Pengine kwa waandishi wachanga wenye lengo la kufika alipofika Jenerali waanze mapema kukataa rushwa ambazo huwafanya kutumia kalamu zao kusifia uharamia kuliko kukosoa utawala mbovu, Alleluya Mungu Mwenyezi kwa kutupatia Jenerali Ulimwengu mwenye uwezo wa kuwasemea masikini wan chi hii, mwenye uwezo wa kukemea udini na ukabila , mwenye uwezo wa kumhoji hata rais bila uwoga nani kama Jenerali?

Naam Jenerali Ulimwengu ni bakora ya watawala acha iwachape tu!

Nani kama jenerali, Ulimwengu tumwone

Nani anayetujali, yu wapi tusemezane

Nani tumpe kibali, ukweli akawachane

Jenerali Ulimwengu, kiboko ya watawala.

Wamesuka njama nyingi, zote zimegonga mwamba

Jenerali ndio kingi, wanyonge tunampamba

Wanaoweka vigingi, hao wote ni mafamba

Jenerali Ulimwengu, bakora ya watawala

Nani asiyefahamu, Jenerali ni shujaa

Yu wapi tumuhukumu, kwa kuzidi kuzubaa

Jenerali ni muhimu, Arusha hata kondoa

Jenerali Ulimwengu, sindano ya mabwenyenye

Wakiwa maofisini, watawala wanalia

Wakisoma gazetini , hofu inawaingia

Kwa Jenerali makini, Mwema Raia sikia

Jenerali Ulimwengu, msome Raia Mwema

Beti tano nakomea, mengi nimeongelea

Ulimwengu endelea, uovu kuufunua

Ukweli tunaujua, wewe unatutetea

Jenerali Ulimwengu, mtetezi wa wanyonge.


Nova Kambota Mwanaharakati,

0717-709618 au 0766-730256

novakambota@gmail.com

www.novatzdream.blog.com

Tanzania, East Africa

Jumatano 29 March 2011.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, March 30, 2011 | | Permalink | Maoni 1
Idadi ya watu