Tanzania receives ALMA award of Excellence in Addis Ababa.

Monday, January 31, 2011
Tanzania yesterday received the First African Leaders Malaria Alliance award of excellence for its efforts in combating Malaria in the country.In the picture The United Nations Secretary General Ban-ki-Moon hands over the award to President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete in Addis Ababa Ethiopia while the chairman of the AU Commission Jena Ping(centre) looks on.(Photo by Freddy Maro).
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, January 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

nakupa siku tano anza kubomoa ofisi yako,iwe mfano kwa raia wengine-Magufuli.

Waziri wa Miundombinu, John Magufuli, akizungumza jambo na Mthamni Mwandamizi wa Wilaya ya Kinondoni, Einhard Chidaga, wakati alipokuwa katika ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Barabara ya Ubungo Maziwa, inayotokea Kigogo, wakati wa ziara hiyo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam, wakati huo huo Waziri huyo ametoa siku tano kwa Meneja wa Mkoa kubomoa ofisi yake iliyopo Ubungo, ili iwe mfano kwa raia wengine wanaotakiwa kupitiwa na zoezi hilo la ubomoaji ili kupisha upanuzi wa Barabara na mradi wa Magari yaendayo kasi.picha kwa hisani ya Muhidin Sufian.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, January 31, 2011 | | Permalink | Maoni 2

unyama uliokithiri..!yametokea leo huko mwananyamala kwa kopa,jijini Dar.

Vichanga hivyo vikiwa tayari vimeondolewa kwenye shimo kando kando ya jirani ya nyumba ya mkazi mmoja wa eneo la Makaburi Mwananyamala kwa kopa..
Kijishimo hiki ndicho vilikotupwa vichanga hivyo.
Eneo ambalo vimekutwa vichanga hivyo mchana wa leo
Wakazi mbalimbali wa eneo la jirani na makaburi ya Mwananyamala kwa Kopa, wakiwa katika simanzi kubwa baada ya kuliona tukio la vichanga wale wasio na hatia yoyote,wakiwa wametupwa kwenye shimo.

======= ===== ===== =====
Katika hali ya kustaajabisha, ya kishenzi na ya kinyama kabisa,maiti za watoto wachanga wanaokadiriwa kuwa na umri wa siku moja au zaidi, zinazofikia idadi ya 11, zimefukuliwa katika shimo moja, jirani na maeneo ya makaburi ya Mwananyamala kwa Kopa mchana wa leo!!. Tukio hilo limevuta hisia za watu wengi na kuwaacha midomo wazi wakazi wengi wa eneo hilo . Hadi sasa haijajulikana maiti hizo ziliwekwa pale na nani na kwa minajili gani ?
Msikilize shuhuda huyu aliyeshuhudia tukio hilo la kusikitisha kabisa.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, January 31, 2011 | | Permalink | Maoni 7

lady in red kumekucha

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, January 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

serikali yaadhimia kuielimisha jamii nzima kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Bw Richard Muyungi Akizungumzia suala la athari ya mabadiliko ya tabia nchi na changamoto zake wakati wa ufunguzi wa Warsha ya wadau wa mikoa ya Lindi na mtwara Mjini Mtwara Leo, kushoto ni mwakilishi wa RAS Mtwara,Bw Smythies Pangisa (Picha na Evelyn Mkokoi wa Ofisi ya Makamu wa Rais).
Washiriki wa warsha ya wadau wakifuatilia kwa makini mada ya dhana nzima ya masuala ya mabadiliko ya tabia nchi ilipokuwa ikiwasilishwa mjini Mtwara leo CPicha na Evelyn Mkokoi wa Ofisi ya Makamu wa Rais).

====== ====== ====== ====

Serikali imedhamiria kuelimisha jamii nzima ya watanzania juu ya athari na namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, kupitia wa kwa wadau wa sekta mbali mbali.

Hayo yameeleezwa leo na Mkurugenzi msaidizi wa Idara ya Mazingira kutoka ofisi ya makamu wa Rais Bw Richard Muyungi, katika warsha ya wadau wa kanda ya kusini ilofanyika mkoni Mtwara.

Bwana Muyungi ameeleza kuwa Nchi zinaoendelea ikiwemo Tanzani inakabiliwa na changamoto mbali mbali zitokanazo na mabadiliko ya Tabia nchi ikiwa ni pamoja na mafuriko akitolea mfano mafuriko ya Kilosa, ongezeko la magonjwa kama vile malaria zaidi katika maeneo ambayo awali maralia haikuwa tishio kama vile Lushoto, kituro Rungwe na Njombe.

Bw. Muyungi ameainisha kuwa, kuna kila sababu ya jamii kuelewa kuhusu mabadiliko ya tabia nchi umuhimu wake na changamoto zake ikiwa ni pamoja na umaskini.

Awali akifuangua warsha hiyo mwakilishi wa Afisa tawala wa Mkoa wa Mtwara Bw.Smythies Pangisa alisema athari zaidi ya mabadiliko ya tabia nchi katika vizazi vijavyo ni ukosefu wa maji safi, kuongezeka kwa hali ya ujangwa katika baadhi ya maeneo na viumbe kutoweka.

Warsha hiyo ya siku mbili iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira imehusisha mada ya mabadiliko ya Tabia nchi na Sera ya Taifa ya Mazingira, sheria ya usimamizi wa mazingira na utekeleazaji wake, imeudhuriwa na wadau mbali mbali wakiwemo maafisa maliasili na mazingira, mahakimu, wadau kutoka katika asasi za kiraia, Ngo’s, na wanahabari.

Habari kwa hisani ya

Evelyn Mkokoi

Afisa Habari Ofisi ya Makamu wa Rais

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, January 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

RATIBA YA TOUR YA LADY JAY DEE IN EUROPE.

These are the booked dates for Lady JAY DEE”s european Tour

1. 21/04 BERGEN NORWAY ( CHIKU ALLY )
2. 22/04 OSLO NORWAY ( HASSAN NGANZO )
3. 23/04 AMSTERDAM HOLLAND ( EDDIE BUKENYA )
4. 24/04 ESSEN GERMAN ( NASHE MVUNGI )
5. 29/04 ZURICH SWISS (Dalla Silk )
6. 30/04 STOCKHOLM SWEDEN ( FREDY NICE )
She’s only doing two weekends. NO MORE BOOKINGS NEEDED.

Hassan Ngazo.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, January 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

gazeti lako makini la dira leo liko mtaani kwa sh 500 tu.




 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, January 31, 2011 | | Permalink | Maoni 0

hatimaye Michael Nkya na Caroline waingia kwenye kurasa mpya ya maisha,jiachie inawatakia kila lakheri katika maisha yao.

Maharusi wakiwaaga wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye mnuso huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Kilamuho-Mbezi beach jijini dar,usiku wa kuamkia leo.
.Maharusi wakicheza taratiibu kwa rahaa zao
Ulifika muda ya kujiachia.
Mkurugenzi Mwandamizi wa kituo cha THT Ruge Mutahaba akipewa zawadi ya heshima kutoka kwa maharusi
Maharusi wakitoa shukurani za dhati kabisa kwa MC aliyeiongoza harusi hiyo mwanzo mwisho,Haris Kapiga ambaye pia ni mmoja wa watangazaji wa Clouds FM.
Vijana wa THT wakitoa heshima ya kipekee kabisa kwa maharusi.
Boss wa masoko wa kampuni ya bia ya TBL,Bwa.David Minja akiwa na mkewe wakifurahia namna vijana wa THT wakionesha ubunifu wao kwa mfanyakazi ambaye ni mwalimu wao wakati wa kutoa heshima kwa maharusi hao.
Mmoja wa viongozi wa waandamizi wa THT,Ruge Mutaha pichani kulia akiwa na viongozi wengine wa THT wakifurahia jambo kwa pamoja,kwamba kijana wao ambaye ni mfanyakazi katika kituo hicho ,anauaga ukapera.
Baadhi ya wasanii kutoka THT wakiwatumbuiza maharusi na wageni waalikwa usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Kilamuho,Mbezi Beach jijini Dar.
wakati wa kitu ndafu.
Lisha nikulishe ndio furaha ya pendo
Michael Nkya akimlisha keki mkewe Bi.Caroline huku wakitabasamu safi kabisa.
Maharusi wakikata keki yao ya upendo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kuishuhudia siku hiyo adhimu kabisa kwa maharusi hao,iliyofanyika katika ukumbi wa Kilamuho,tangibovu-Mbezi beach,jijini dar.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, January 31, 2011 | | Permalink | Maoni 6

President Dr. Kikwete in Addis for the African Union Summit

President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete shake hands with President Dr.Bingu wa Mutharika of Malawi shortly after the opening of the 16th ordinary Session of the Assembly of the African Union at Addis Abba Ethiopia this afternoon. President Kikwete flew in Addis last night from Davos Switzerland after attending the World Economic Forum (WEF)2011 where he launched a strategy to significantly increase food production while conserving environmental resources and spurring economic growth in Tanzania. Others in the picture are from left front row Liberia’s President Sirleaf Johnson, The Chairman of the AU Commission Jean Ping and right is the United Nations Secretary General Ban-ki-Moon(Photo by Freddy Maro).
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, January 31, 2011 | | Permalink | Maoni 9

warembo wanaowania taji la kisura wa tanzania 2011 waingia kambini leo.

Sunday, January 30, 2011


WAREMBO wanaowania taji la Kisura wa Tanzania 2010/11, wameingia kambini leo katika Hoteli ya Kiromo View Resort, iliyopo nje kidogo ya Mji wa Bagamoyo,Pwani, tayari kwa fainali zitakazofanyika Machi 12, mwaka huu. Kambi hiyo itahusisha wasichana 25 kutoka mikoa mbalimbali nchini, waliofanikiwakutinga katika hatua ya fainali za shindano hilo, baada ya mchujo uliofanyika kwa miezi miwili.

Mchakato wa kuwapata wasichana hao, ulianza Desemba 11, mwaka jana, na kumalizika mapema mwezi wa kwanza, ukihusisha warembo kutoka mikoa ya Mwanza,Mara, Kagera, Shinyanga, Tabora, Dar es Salaam, Arusha, Manyara, Dodoma, Iringa,Mbeya na Ruvuma.

Akizungumza wakati wa kuwatambulisha warembo hao katika Hoteli ya Kiromo ViewResort, Mwenyekiti na Mwanzilishi wa mradi wa Kisura wa Tanzania, Juliana Urio kutoka kampuni ya Beautiful Tanzanie Agency (BTA), alisema kuwa warembo walioingia kambini, ni wale waliopita katika mchujo baada ya kukidhi vigezovinavyotakiwa.

Vigezo hivyo urefu wa sentimita174, mapaja 36, kiuno 25, kifua 36 na umri ni kati ya miaka 18-27, bila kujali kama mshiriki ameolewa, kuzaa au la.“Mwaka huu idadi ya warembo walioingia kambini imeongezeka, kutoka 20 kama ilivyokuwa awali hadi 25, hii ikitokana na mdhamini wetu Kiromo View Resort kutupa nafasi ya pekee ya kuongeza wasichana watano zaidi,” alisema.Urio aliwataja warembo walioingia kambini kuwa ni Neema Methew na Silipa Swai kutoka Mwanza, Lilian Bussa na Gaudencia Joseph (Mara), Beatrice James (Kagera),

Monica Fikiri na Angella Mombeki (Tabora).Wengine ni Suzana Manoko, Winnfrida Sabega, Rita Swai, Lethina Christoper, Joyce Joseph, Happiness Salimenya, Grace David (Dar es salaam), Dotinata Soro, Neema Kilango, Neema Seley (Arusha), Kipoyane Laibon (Manyara), Mariam-Kissa Isaack, Asha Hamisi, Flavian Makungwa, Lucy John (Dodoma) na Queen Kabisama (Ruvuma).

Alisema kuwa wakiwa kambini, warembo hao watapewa mafunzo mbalimbali kuhusiana na maisha yao binafsi na jinsi ya kukabiliana na changamoto zinazowazunguka katika maisha yao ya kila siku, ikiwa ni pamoja na kutembelea maeneo tofauti. Urio aliwapongeza warembo waliopata bahati ya kutinga fainali za shindano hilo,ikiwa ni pamoja na kuwashukuru wazazi waliowaruhusu watoto wao kujiunga shindano hilo, akiwaahidi ‘kuwapika’ vilivyo warembo hao ili waweze kuwa mfano wa kuigwa kwa jamii ya kitanzania kutokana na matendo yao.

Mdhamini mkuu wa shindano hilo ambalo linafanyika kwa mara ya tatu sasa, ni Family Health International (FHI), wakati wadhamini wengine ni TBC1, Kiromo View Resort, TanFoam (Arusha), SBC Limited, Flare Magazine, Hugo Domingo, BASATA, GRM Production, Clouds FM, ATCL na MJ Records.Pia napenda kutoa shukurani zangu za dhati kwa kupata wadhamini wapya, TBL kupitia kinywaji chao cha REDDS na i-View
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, January 30, 2011 | | Permalink | Maoni 1

maharusi Michael Nkya na mkewe wakiwa na marafiki mbalimbali mara baada ya kufunga ndoa leo.







 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, January 30, 2011 | | Permalink | Maoni 2

Michael na caroline walivyomeremeta azania front leo mchana.

Caroline akiwa ametulia tulii wa raha zake.
Bibi harusi Caroline akiwa amepozi na ua lake mara baada ya kufunga ndo leo mchana katika kanisa la Azania Front,jijini Dar.
Bwana harusi Michael Nkya kwa raha zake akimfunua shella mkewe mara baada ya kuvalishana pete ya ndoa na kuanza kurasa mpya ya maisha yao.
Waoooo....!
Maharusi wakiwa wameambatana na wapambe wao wakielekea kanisani,kwa maana kwamba wakati umewadia wa kutimiza ndodo zao kati ya Dada Caroline na Kaka Michael Nkya na hatimaye kuhalalishwa kuwa mwili mmoja ndani ya kanisa l a Azania Front,jijini Dar mchana wa leo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, January 30, 2011 | | Permalink | Maoni 3

teacher michael nkya akimeremeta na mkewe Carolina mchana huu.

Pichani maharusi watarajiwa wakiwa katika chumba cha matayarisho kabla ya kuingia ndani ya kanisa la Azania Front mchana huu kwa ajili ya kuitimiza ndoto yao ya kuishi pamoja.
Maharusi watarajiwa wakiwa wamepozi na wapambe wao kwenye chumba cha maandalizi kabla ya kufunga ndoa mchana huu ndani ya kanisa la Azania Front jijini Dar.
Wapambe wa maharusi wakiwa katika picha ya pamoja mchana huu.
Dada Carolina akiwa na mpambe wake wakiwasili katika kanisa la Azania Front ,jijini Dar mchana huu kwa ajili ya kufunga ndoa takatifu na mpendwa wake Michael Nkya.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, January 30, 2011 | | Permalink | Maoni 1

waandishi wa habari wadaiwa kuvamia mikutano na kudai posho,wapiga picha wa tv na maripota wadaiwa kuwa matawi ya juu..!

Saturday, January 29, 2011
Imeelezwa katika mkutano wa wadau na waandishi wa habari uliofanyika ukumbi wa majengo ya makumbusho ya Azimio la arusha Januari 28 kuwa baadhi ya waandishi wamekuwa wakivamia mikutano na kudai posho kwa nguvu na wanapokosa hela wanaporomosha matusi.

Waandishi wamekuwa wakijifanya askari kanzu kuchunguza habari za watu na kuwadai fedha kwa nguvu.

Hapa Arusha waandishi wa habari wa kike wamebatizwa jina na kuitwa watoza ushuru,ushuru huo ama uwe wa habari au wa ngo..! kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Isdori Shirima.

Abubakari Karisan amewashutumu wamiliki wa vyombo vya habari kushindwa kuwalipa bwaandishi wao wa mikoani na kusababisha kufanya kazi katika mazingira magumu.

Hata hivyo ametoa wito wa Asasi za kiraia kuangalia namna bora ya kuwasaidia waandishi wafanye kazi kwa kuzingatia miiko ya uandishi wa habari.

Viongozi wa vyama vya Siasa wameonywa kuacha kuwagawa waandishi kwa pesa na badala yake watoe nafasi wafanaye kazi zao kwa uhuru.

Pia tabia ya Viongozi wa Serikali,Wanasiasa n.k kupendelea TV na Redio iachwe kwani inadumaza waandishi wa habari wa magazeti,na hata mwingine Waziri,Kongozi wanapokuwa na mkutano unaweza kuchelewa kuanza kisa mtu wa Tv hajafika.

Na hali imesababisha wapiga picha wa TV na ripota kujiona wako matawi ya juu na kutaka walipwe pesa nyingi.

habari hii imetumwa na Fortunatus.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, January 29, 2011 | | Permalink | Maoni 1

skia hii kutoka kwa jeneral Ulimwengu

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, January 29, 2011 | | Permalink | Maoni 7

afumaniwa live..!

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, January 29, 2011 | | Permalink | Maoni 36

WARSHA YA WAHARIRI KUHUSU NAFASI YA VYOMBO VYA HABARI KATIKA MCHAKATO WA KATIBA MPYA YAFANYIKA DAR ES SALAAM

Friday, January 28, 2011

JENERALI Umlimwengu akizungumza katika warsha ya wahariri kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika mchakato wa Katiba mpya, iliyofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Profesa Issa Shivji.picha kwa hisani ya Chachandudaily.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, January 28, 2011 | | Permalink | Maoni 0

washiriki wa exchange programme ya tamwa wakutana

Anna Nkinda (katikati) akielezea yale ambayo amejifunza nchini Kenya.
Wanachama wa Tamwa pamoja na Mkurugenzi wa TAMWA mama Ananilea Nkya wa pili kushoto wakiwapongeza Amina Mollel wa Shirika la Habari la Utangazaji la Taifa (TBC 1) wa nne kushoto na Anna Nkinda wa Idara ya Habari Maelezo wa nne kulia baada ya kumaliza kozi yao ya kubadilishana kazi (Exchange Programme) kwenye Nchi za Kenya na Nepal wakiwa kwenye picha ya pamoja kwenye ofisi za Tamwa zilizoko Kijitonyama mjini Dar es Salaam leo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Friday, January 28, 2011 | | Permalink | Maoni 1
Idadi ya watu