viongozi wa dini wakutana na chadema.

Thursday, September 30, 2010
ASKOFU Tomas Laizer wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati (kushoto), akizungumza na mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, Dk. Willibroad Slaa, makao makuu ya chama hicho, Kinondoni Dar es Salaam, baada ya ujumbe wa Kamati ya viongozi wa dini nchini akiwemo askofu Laizer, kufanya mazungumzo na viongozi wa CHADEMA jana, ambapo pamoja na mambo mengine walizungumzia mustakabali utakaowezesha uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, kufanyika kwa amani na kutozusha rabsha baada ya matokeo, kwa kuzingatia mambo kadhaa ikiwemo vyama shiriki kukubali matokeo baada ya uchaguzi. Kulia ni Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, na wa tatu ni mgombea ubunge jimbo la Ubungo kwa tiketi ya Chama hicho, John Myika.
Mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa (katikati) akisalimiana na Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa Salum wakati mgombea huyo alipokutana na viongozi mbalimbali wa dini Dar es Salaam jana. Kushoto ni mgombea mwenza, Said Mzee Said.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

jk akiendeleza kampeni zake uyowa,urambo leo.

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia mkutano wa kampeni Uyowa Wilayani Urambo leo
Wananchi wa Uyowa wakishangilia huku wakiwa wamepunga mikono hewani wakati wakifuatilia hotuba ya Mheshimiwa Kikwete kwenye mkutano wa kampeni Uyowa mjini Urambo.
Umati mkubwa wa watu wakimshangilia Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiingia Uyowa, Ulyankulu Wilayani Urambo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

WAZIRI MASHA AWATAKA POLISI WASIVUNJike MOYO!

NA MAGRETH KINABO NA MARY KWEKA- MAELEZO

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Lawrence Masha amelitaka jeshi la polisi lisivunjike moyo kwa kuongezeka kwa taarifa za uhalifu katika vituo vya polisi bali wachukulie kama changamoto na kujidhatiti kukamirisha mikakati ya kukabiliana na matukio hayo.

Kauli hiyo ilitolewa leo na Waziri Masha wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya wakaguzi wasaidizi wa jeshi hilo, iliyofanyika katika Chuo cha Polisi Dar es Salaam. “Mnao wajibu wa kuwa mstari wa mbele katika kupanga mikakati madhubuti ya kukabiliana na changamoto hizi,” alisema Waziri Masha.Alizitaja sababau za kuongezeka kwa matukio ya uhalifu kuwa ni maendeleo ya Sayansi na teknolojia, ukosefu wa ajira, utandawazi, umasikini, ukuaji wa miji, ongezeko la makazi holela, kuzagaa kwa silaha, imani za kishirikina,ongezeko la pengo baina ya matajiri na masikini pamoja na utumiaji na usafirishaji wa dawa za kulevya.

Waziri Masha alisema kuongezeka kwa taarifa za uhalifu katika vituo vya polisi ni miongoni mwa mafanikio ya jitihada zinazofanywa na jeshi hilo, kuwahamasisha wananchi kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu katika maeneo yao. Hata hivyo Waziri Masha aliongeza kuwa makosa yanayowakera wananchi kama unyanga’nyi na uvunjaji wa majumba na wizi yamepungua.

Alisema takwimu zinaonyesha kuwa mwaka 2008 makosa ya uvunjaji yalikuwa 27,491 na mwaka 2009 yalipungua hadi 26,561 hivyo kupungua kwa asilimia 3.4, wakati makosa ya wizi mwaka 2008 yalikuwa 31,130 na mwaka 2009 yalipungua hadi kufikia 28,427, hivyo yamepungua kwa asilimia 8.7.

Waziri Masha alilipongeza jeshi hilo, kwa kuendelea na mpango wa kuratibu na kusimamia mafunzo ya walinzi wa amani kimataifa ikiwa ni pamoja na kushiriki kwa vitendo shughuli za kulinda amani sehemu mbalimbali duniani.“Serikali inaendelea kuvijengea mazingira mazuri vyombo vya ulinzi na usalama na kutatua matatizo ya makazi na maslahi ya watumishi wake.

Serikali kupitia Mfuko wa Hifadhi ya Jamii(NSSF) katika mwaka huu wa fedha inaendelea na awamu ya pili ya ujenzi wa nyumba za askari kwa kujenga maghorofa 30 kambi ya polisi barabara ya Kilwa, sita kambi ya Mabatini Mwanza, sita Musoma , Mara, Tatu Byekera ,Bukoba, 12 Ludewa Iringa, nane Kiwanja cha ndege Arusha, mbili Unguja Kuu Unguja na mbili Finya Kaskazini, Pemba.

Naye Mkuu wa chuo hicho, Elice Mapunda alisema kitaanza kutoa diploma ya sayansi ya polisi kuanzia mwaka 2010/2011 ikiwa ni jitihada za kukipandisha hadhi.Alisema jumla ya wanafuzi walioripoti katika mafunzo hayo walikuwa 356 na wote wamefaulu, lakini wawili kati yao walishindwa kushiriki kikamilifu baada ya kuumia wakiwa chuoni.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

KCB Tanzania yajitolea kulea watoto yatima wapatao 11.

Baadhi ya wfanyakazi wa KCB Tanzania wakiwa wamewabeba watoto wa kituo cha yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu cha Amani Orphanage Center cha Boko wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kufundishia vyenye thamani ya milioni 2/-kwenyer hafla iliyofanyika shuleni hapo leo jijini Dar es SalaamMeneja Uhusiano wa KCB Tanzania , Austin Makani akigawa vinywaji kwa wanafunzi wa kituo cha Amani Orphanage Center wakati wafanyakazi wa benki hiyo walipotembelea kituo hicho na kutoa msaada vifaa vya kufundishia vyenye thamani ya shilingi milioni 2/- jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa K CB Tanzania ,Christina Manyenye akikabidhi vifaa vya kufundishia vyenye thamani ya milioni 2/- kwa watoto wa kituo cha Amani Orphanage Center cha Boko kinachohudumia watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu wakati wa hafla liyofanyika shuleni hapo jijini Dar es Salaam leo.Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa KCB Tanzania, Christina Manyenye (kushoto) na Mkurugenzi wa kituo cha Amani Orphanage Center , Margareth Mwegalawa wakiwasaidia kufungua maboksi yenye vitabu vilivyotolewa na benki hiyo wakati wafanyakazi wa benki hiyo walipotembelea kituo hicho na kutoa msaada wenye thamani ya shilingi milioni2/- jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa kituo cha Amani Orphanage Center Margareth Mwegalawa akipokea msaada wa vifaa vya kufundishia vyenye thamani ya milioni 2/- kutoka kwa Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa KCB Tanzania ,Christina Manyenye wakati wa hafla iliyofanyika kwenye kituo hicho kinachohudumia watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu jijini Dasr es Salaam leo.

======= = ===== ===== ===== ==== ====

KCB Tanzania yajitolea kulea watoto yatima

Na Mwandishi Wetu

BENKI ya KCB Tanzania imeamua kubeba jukumu la kuwalea watoto 11 wa kituo cha watoto yatima cha Amani Orphanage Centre kwa kukikisaidia na kukihudumia kwa mahitaji ya vifaa muhimu vya shule kwa watoto hao kilichopo Boko jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali wenye thamani ya zaidi milioni 2/- kwa ajili ya takribani watoto 45 wa shule hiyo,Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo Christina Manyenye alisema kwa kuanzia wametoa vifaa hivyo ili viwasaidie kwanza yatima.

Akifafanua alisema kutokana na kuguswa na watoto wa kituo hicho kilicho chini ya Shirika la Empowering Children and Community Organization kilichoanzishwa kusaidia watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu wameona wakisaidie kutokana na kuona kwamba ndoto za watoto hao ni sawa na za wanaotoka katika familia zinazojimudu kimaisha.

“Hivyo basi hatuna budi kuwasaidia watoto hawa na tunaahidi kuendelea kuwasaidia ili kukipunguzia mzigo kituo cha Amani jukumu la kuwalea watoto kituo hiki cha Amani ikiwa ni pamoja na kuwawezesha kusoma. Ni wachache sana wanaoweza kufanya ubinadamu huu,” alisema Manyeye.

Hata hivyo aliongeza kwamba msaada huo umefuatia KCB Tanzania kutambua umuhimu wa jamii na kufahamu ukweli kuwa maendeleo ya jamii ni maendeleo ya taifa zima. Aidha alisema bila jamii yenye maendeleo uwepo wao kama benki utakuwa na mashaka.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho Margareth Mwegalawa alisema kuwa licha kuhudumia watoto yatima 11 wanaoishi bweni, pia wanahudumia watoto wengine wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuwapatia vifaa vya shule na mahitaji mengine.

Hata hivyo wanakabiliwa na uhaba wa vyumba vya kulala watoto, vitanda, uchakavu milango na madirisha ya jengo la kituo hicho jambo linalochangia kituo kuchukua watoto wachache wanaoendelea kuishi kwenye mazingira magumu.

Kutokana na hilo waliiomba KCB Tanzania na taasisi zingine kujitokeza kukisaidia kituo hicho kwa kukipa misaada mingine ikiwemo magodoro, vitanda, vifaa vya kusomea watoto, vyakula, madawati ya kukalia na vifaa vya kufundishia.

Nae Afisa Maendeleo ya Jamii kata ya Bunju, Syzgo Alexander aliiopongeza benki hiyo kwa kuwa na moyo huo wa kujitolea na kusema kutokana na mahali kilipo kituo imeonesha imejitoa kuihudumia jamii kwa hali na mali jambo alilotaka liiungwe mkon o na Watanzania.

KCB Tanzania ni benki kubwa Afrika Mashariki ikiwa na rasilimali nyingi ikiwemo matawi zaidi ya 200 na mashine zaidi ya 400 za kutolea fedha (ATM) zilizotawanywa kote Afrika Mashariki na mtandao unaofikia nchi za Rwanda na Sudan Kusini.


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

mjue mgombea ubunge wa chadema.


Mjue Mgombea Ubunge Kinondoni kwa tiketi ya CHADEMA Bw Phillip Nyanchini MOGENDI Tembelea tovuti yake hapa http://phillipmogendi.com/
Asante!
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 4


WATOTO MKOANI KIGOMA NA RUKWA KUPATIWA CHANJO YA POLIO.

Na. Aron Msigwa - MAELEZO.


Serikali imewataka wananchi wa mikoa ya Kigoma na Rukwa kushiriki kikamilifu katika awamu ya pili ya zoezi la utoaji wa chanjo ya ugonjwa wa kupooza (polio) kwa watoto walio chini ya miaka mitano litakolofanyika tarehe 4 hadi tarehe 7 mwezi Oktoba, 2010.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Bi. Blandina Nyoni amesema kuwa hatua ya kufanyika kwa zoezi la utoaji wa chanjo ya polio kwa watoto katika mikoa hiyo, inafuatia taarifa ya kutokea kwa mlipuko wa Ugonjwa huo katika wilaya ya Kalemie nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mwezi Agosti mwaka huu.

Amesema Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii ilichukua hatua za haraka za kudhibiti ugonjwa huo usiingie nchini kutokana na jiografia kati ya Tanzania na DRC ,pamoja na muingiliano wa watu katika maeneo hayo kwa kuihamasisha jamii na viongozi wa ngazi zote mkoani Kigoma na Rukwa na wadau wengine kuhusu mlipuko wa ugonjwa huo .

Mbali na hatua hiyo amesema, serikali iliendesha zoezi la kutoa chanjo ya polio kwa watoto wote walio na umri chini ya mika mitano kwa njia ya Kampeni , Kuimarisha utoaji wa taarifa za wagonjwa waliopata ulemavu wa ghafla na uimarishaji wa utoaji wa chanjo za kawaida ambapo matokeo ya zoezi la awali yanaonyesha mafanikio kwa kufikia kiwango cha asilimia 90 ya chanjo kwa watoto chini ya miaka mitano.

Amesema mwongozo wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) unabainisha kuwa ili kudhibiti mzunguko wa virusi pori vya ugonjwa wa polio ni muhimu kutoa chanjo za ziada kwa njia ya kampeni kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka angalau kwa awamu mbili.

Hata hivyo amefafanua kuwa Wizara ya Afya kwa kushirikiana na wadau wa Maendeleo watahakikisha kuwa vitendea kazi kwa ajili ya Kampeni hiyo zikiwemo chanjo na vifaa vingine vinaapatikana katika muda muafaka .

“Kampeni na zoezi la utoaji wa chanjo hii katika mikoa ya Rukwa na Kigoma litafanyika kwa mafanikio makubwa kutokana na kuwepo kwa vifaa muhimu kwa shughuli hiyo ambavyo tayari vimeanza kusambazwa” amefafanua Bi.Nyoni.

Amesitsitiza kuwa chanjo hii ya Polio itakayotolewa kwa watoto walio chini ya umri wa miaka 5 wapatao 703,389 katika mikoa yote miwili ni salama na itatolewa na wataalam wa afya kwa njia ya matone kinywani kwa watoto wote bila kujali kama walipata chanjo hiyo hapo awali au hawakupata.

Ametoa wito kwa wazazi na wananchi wote kushiriki kikamilifu katika zoezi hili kwa kushirikiana na wataalam wa afya watakaopita nyumba hadi nyumba na kuongeza kuwa watoto wote watakaopata chanjo hiyo watawekewa alama maalum katika kidole kidogo cha mkono wa kushoto ili kusaidia ufuatiliaji na uhakiki pamoja na kuweka alama kwenye nyumba zitakazofikiwa kulingana na hali ya chanjo ya watoto waliopo katika nyumba hizo.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

16 waibuka nusu fainali ya mavazi,kushiriki onyesho la mavazi swahili fashion week 2010

Mama Shalua(Left),Charles Washoma(Middle) and Manju Msita on their judge duty

===== ====== ===== =====

Jopo la majaji lakutana kuchagua walifanikiwa kuingia nusu fainali shindano la mbunifu wa mavazi wanaochipukia

16 waingia katika nusu fainali ya wabunifu wanaochipukia na majina yao yatajwa

“Contemporary Swahili” ni kauli mbiu ya shindano 2010


Majina ya wabunifu 16 wenye vipaji ambao wataingia katika nusu fainali na kushindania zawadi ya mwaka katika onyesho kubwa la wiki la mavazi Swahili Fashion Week 2010 wapatikana.

Uchaguzi wa wabunifu wa mavazi wanaochipukia umefanyika Septemba 29 katika hotel ya Southern Sun jijini Dar es salaam, ambapo majina 16 yalichaguliwa na jopo la majaji watatu ambao ni Manju Msitta kutoka Smart Afrika Design Label, Charles Washoma, CEO of African Life assurance and One of Dar es Salaams Fashionable man na Director of arts Nsao Shalua of Baraza la Sanaa la Taifa (National arts Council).


Wabunifu hao 16 waliochaguliwa katika nusu fainali, kwa mara nyingine tena watachuana katika mchujo wa kuwapata wabunifu wa mavazi wanaochipukia wanane (8) ambao watashindana katika kuonyesha kazi zao katika onyesho kubwa la wiki la mavazi Swahili Fashion Week litakayofanyika mwezi wa Novemba mwaka huu.


Mratibu wa Swahili Fashion Week, Ndugu Washington Benbella amesema kuwa “Muitikio umekuwa ni mzuri, ari na hamu imeonyesha vipaji vya hali ya juu vya ubunifu wa mavazi ambavyo vipo hapa nchini, lakini kwa wale ambao hawakupahatika kupata nafasi ya kuchaguliwa wasiishie hapa na wasikate tamaa bali waendelee na kuhakikisha kwamba wanafanikiwa na kufikia malengo yao”


Wabunifu wa mavazi wanaochipukia waliofanikiwa kuingia nusu fainali ni pamoja na Zarina Suleiman, Pooja Narendrakumar Jeshang, Abduel Urasa, ShaibMfaume, Annette Ngogi, Mwajabu Sadiki, Diana Malenge, Mgece Makory, Omary Bundalah, Kelvin Boniface, Subira Rahma Wahure, Nadia. A. Ahmed, Angelina Muna, Jacqueline Chipeta, Bami Musese na Grace Kijo.

Majaji walikuwa na kazi ya ziada, kwani walikuwa makini katika kuangalia mambo mbalimbali ili kuweza kupitisha majina ya wabunifu wa mavazi wanaochipukia, kwani walilazimika kualiangalia uwezo katika ubunifu na kuchora, kwa kiasi gani mchoro unavitia, rangi iliyotumika katika mchoro na mambo mbalimbali yanayohusiana na ubunifu kwa ujumla.


Sahili Fashion Week ni jukwaa pekee linalowaleta pamoja wabunifu wa mavazi na watengenezaji wa bidhaa za mapambo kutoka nchi zote zinazozungumza lugha ya Kiswahili, ili kuonyesha ubunifu wao, kuuza bidhaa wanazozalisha, kubuni ajira, sambamba na kutengeneza mtandao kwa wabunifu kutoka maoneo hayo wanayoongea lugha ya Kiswahili, sambamba na kuhimiza dhana nzima ya kuthamini bidhaa zinazotengenezwa Afrika Mshariki.

Msisitizo zaidi umewekwa katika kuhakikisha kwamba sekta ya ubunifu inakuwa kikanda. Swahili Fashion Week inalenga kukuza sanaa ya ubunifu na kuwa jukwaa bora la kibiashara kimataifa kwa nchi za Afrika Mahariki.Kwa mara ya tatu sasa Swahili Fashion Week imekuwa ikifanyika, ambapo kwa mwaka huu itafanyika November 2010, Dar Es Salaam, Tanzania.


Shindano hili linafanyika kwa mwaka wa tatu sasa, halina kikwazo cha umri, na linatoa fursa kwa watu wote wanaoamini kwamba wana kipaji cha ubunifu, na wanataka kuwa wabunifu. “Swahili Fashion Week ni jukwaa bora kwa wabunifu kuonyesha uwezo wao wa ubunifu na kuibua sindano la wabunifu wapya, ni jukwaa linalowawezesha watu kufikia malengo yao ”, aliongeza Mustafa Hassanali muandaaji wa Swahili Fashion Week.


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

mashabiki wa simba wapata ajali.




Baadhi ya mashabiki wa timu ya Simba wakiwa wamesurika na ajali iliyotokea jana maeneo ya Kibaha -Tanita wakati wakielekea mjini morogoro kwenye mpambano wa timu ya Simba na Mtibwa,mara baada ya basi lao kupinduka na kupelekea mtu mmoja kupoteza maisha.Picha kwa hisani ya Shafii Dauda wa Sports Bar ya Clouds TV.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

wenyewe hata sijui wanajiunga vipi na chama hiki.?

Nimepita mapema leo barabara ya Sokoine Drive,jijini Dar ambako lipo jumba hili la Wana wa Freemasons,ambapo pia inaelezwa kuwa kuna wimbi kumbwa la watu wakijiunga na chama hicho,Wenyewe hata sijui wanajiunga vipi kwa njia ya namna gani.?.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 7

DK. BILAL AZINDUA SHINA LA WAKEREKETWA LA WAJASILIAMALI LA WAUZA SAMAKI NA DAGAA SUMBAWANGA

Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akimvisha kofia yake Katibu wa Shina la Wakereketwa la Wajasiliamali la wauza Samaki na Dagaa, baada ya kuzindua shina hilo lililopo mtaa wa Karume Sumbawanga mjini leo.
Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akifunua kitambaa kuashiria kuzindua rasmi Tawi la Shina la Wakereketwa la Wajasiliamali la wauza Samaki na Dagaa, baada ya kuzindua shina hilo lililopo mtaa wa Karume Sumbawanga mjini leo .
Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal na mkewe Zakia Bilal, wakiinua mikono kuwasalimia wananchi wa Kijiji cha Ilembo Wilaya ya Mbeya Vijijini, wakati walipowasili kijijini hapo juzi Sept 28 kufanya mkutano wa kampeni.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

daraja la vingunguti/msimbazi mbioni kukamilika.

Mkazi wa Vingunguti akikatiza njia ya mkato mbele ya daraja linalotenganisha bonde la Msimbazi na Vingunguti mara baada ya kunaswa na kamera ya Jiachie jana jioni,daraja hilo ambalo lilikuwa kilio kikubwa kwa wakazi wa maeneo hayo liko mbioni kukamilika.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

Uchaguzi Express' @ 9pm on EATV.

Habari za asubuhi,
Here is a list of the confirmed and potential guests on tonight's 'Uchaguzi Express' @ 9pm on EATV.
  1. NCCR - Rajabu Kazimoto - Mgombea Ubunge - Jimbo la Ubungo
  2. UPDP - Richard Pius - Mgombea Ubunge - Jimbo la Kawe
  3. CUF - Joran Dashange - Naibu Katibu Mkuu
  4. APPT - Fitina Mohamed - Mgombea Ubunge - Jimbo la Kinondoni
  5. TLP - Mwansasu Kambona - Mgombea Ubunge - Jimbo la Ubungo
  6. CHADEMA - John Mnyika - Mgombea Ubunge - Jimbo la Ubungo
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

itazame picha hii kwa makini,halafu tafakari.!

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 5

wanamuziki wa ferre gola watua Dar,yeye kutua leo jioni.

Mmiliki wa bendi ya Mashujaa ajulikanae kwa jina la Mama Sakina,akiwaomba radhi baadhi ya waandishi wa habari usiku wa kuamkia leo katika uwanja wa kimataifa wa Mwl JK Nyerere,Kufuatia kutukanwa kwao na baadhi ya Mabaunsa waliofika uwanjani hapo huku wakiwa wamelewa,Mama Sakina pia alitoa ufafanuzi wa vurugu zilizotokea uwanjani hapo wakati wa kumpokea Ferre Gola,akieleza kuwa watu hao walikuwa wametumwa kwa ajili ya kuja kumuharibia mapokezi hayo wakiwemo na baadhi ya Mabaunsa ambao walikuwa wamelewa kupita kiasi huku wakitukana matusi mazito mazito kwa Waandishi wa habari waliokuja uwanjani hapo kufanya kazi yao.
Mwimbaji na rapa wa Mwanamuziki Ferre Gola kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Congo anayejulikana kama (Shikitu) akihojiwa na wanahabari kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu J.K,Nyerere, hata hivyo Kiongozi wao mwanamuziki Ferre Gola anatarajiwa kuwasili leo mnamo saa 12 jioni na anatarajia kufanya onyesho kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee kesho Ijumaa akishirikiana na bendi ya Mashujaa inayoongozwa na Mwanamuziki Jado Field Force.
Mwimbaji na rapa mahiri wa mwanamuziki Ferre Gola kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Congo anayejulikana kama (Shikitu) akipewa escot na Baunsa mara baada ya kuwasili usiku wa kuamkia leo uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu J.K,Nyerere.(Kwa Wahusika naomba nidhamu ya Baunsa huyu ambaye kwa bahati mbaya sikuweza kulibaini jina lake mapema,naomba ichunguzwe kwa makini awapo kazini) .!
Mwanamuziki mpiga gitaa la Sollo kutoka kundi la Ferre Gola anayejulikana kama Chally Sollo akihojiwa na vyombo vya habari kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K. Nyerere mara baada ya kuwasili kwa ajili ya onyesho lao linalotarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee kesho Ijumaa.
Baadhi ya Wanamuziki wa Bendi ya Mashujaa wakiongozwa na kiongozi wa bendi hiyo Jado Field Force (haonekani pichani) katika kutia nakshi nakshi ujio wa mwanamuziki Ferre Gola (Shetani) mbele ya Camera ya Clouds Tv wakati walipokuwa wakimsubiri mwanamuziki huyo kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu J.K.Nrerere usiku wa kuamkia leo, pamoja na shamra shamra hizo Mwanamuziki huyo hakuweza kuwasili usiku wa jana,badala yale anatua leo jioni jijini Dar mnamo majira ya saa 12 na ushehe hivi,waliotangulia ni wanamuziki wake.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, September 30, 2010 | | Permalink | Maoni 1

Mzee hamsini kutia nakshi nakshi onyesho la kanga za kale.!

Wednesday, September 29, 2010
Mama Asia Idarous Hamsini ambaye pia ni mkongwe katika fani ya ubunifu wa mavazi amenaswa na kamera Jiachie usiku huu ndani ya Uwnja wa ndege wa kimataifa wa Mwl JK Nyerere alipokuwa akimpokea mumewe Mzee Hamsini kutoka huko Ughaibuni ,ambaye ametua rasmi kwa ajili ya onyesho la usiku wa Kanga za Kale litakalofanyika ijumaa usiku katika ukumbi wa Diamond VIP.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, September 29, 2010 | | Permalink | Maoni 0

sikiliza miss Tanzania akizungumza machache wakati akiagwa leo.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, September 29, 2010 | | Permalink | Maoni 1

vodacom miss tanzania 2010 akabidhiwa bendera ya taifa leo jijini dar,kutimka kesho kwenda china

Vodacom Miss Tanzania 2010 Genevieve Emmanuel akiwa amepozi kwa picha huku akiwa ameishikilia bendera ya Taifa kwa ajili ya kwenda kuiwakilisha katika mashindano ya Miss World yatakayofanyika hapo baadae mwaka huu nchini China.
Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji nchini (TIC) na Mlezi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw.Emmanuel Ole Naiko akimkabidhi kinyago Miss Tanzania 2010 Geneviev Emmanuel kama sehemu ya kwenda kuitangaza nchi yetu,Mlimbwende huyo anatarajia kuondoka nchini kesho kuelekea Beijing,China ambako mashindano hayo yatafanyika.
Miss Tanzania 2009 na Miss Tanzania 2010.
Kushoto ni Mama mzazi wa Miss Tanzania Genevieve wakiwa na aliyekuwa mgeni rasmi Mkuu wa Sekta Binafsi nchini Ester Mkwizu na baba yake Emmanuel Mpangala katika picha ya pamoja na Miss Tanzania 2010.
Kutoka kushoto ni mlezi wa Miss Tanzania ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kituo Cha Uwekezaji nchini (TIC),Emmanuel Ole Naiko,Mkuu wa Sekta Binafsi nchini Bi. Ester Mkwizu, Genevieve,
Mkurugenzi wa Utamaduni na Kaimu katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo Prof Helmas Mwansoko pamoja na Mkurugenzi wa Udhamini Vodacom Tanzania George Rwehumbiza.
Pichani kati ni mtaalamu wa mambo ya habari wa Vodacom Tanzania,Martina Nkurlu na wadau wengine wakifuatilia kwa makini hafla hiyo ya kukabidhiwa bendera ya Taifa,Vodacom Miss Tanzania 2010 Geneviev mapema leo asubuhi jijini Dar.
Baadhi ya wageni waalikwa mbalimbali akiwemi Miss Tanzania 2009,aliyemaliza muda wake Miriam Gerald pia alikuwepo kumsindikiza mlimbwende mwenzake.
Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji nchini (TIC) na Mlezi wa Kamati ya Miss Tanzania Bw.Emmanuel Ole Naiko akizungumza kwenye hafla fupi ya kumkabidhi bendera Miss Tanzania 2010 kwenye viwanja vya TIC mapema leo asubuhi jijini Dar.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, September 29, 2010 | | Permalink | Maoni 1

msondo ngoma a.k.a baba ya muziki kuwasha moto kanda ya kusini

Na Mwandishi wetu

BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo ngoma imeondoka jijini Dar es Salaam kwa ziara ya maonesho matano katika mikoa ya kusini kuanzia Oktoba mosi mwaka huu, baada ya kukaa muda mrefu bila kutembelea kanda hiyo.

Akizungumza jijini Dar leo, Msemaji wa bendi hiyo, Rajabu Mhamila 'Super D' (pichani)amesema kuwa ziara hiyo ni maalumu kwa ajili ya kuitamulisha albamu yao mpya ya Huna Shukrani.

"Tukiwa huko tutafanya kazi ya kuwapa burudani na wapenzi wetu watapata nafasi
ya kuona mambo mengi yanayohusu bendi yao kama hayo niliyoyasema.," alisema Mhamila.

Amesema kuwa wataanzia kuangusha burudani ya aian yake katika ukumbi wa Bwalo la Maendeleo, Kilwa na Hoteli ya Lindi Oktoba mosi, ambapo oktoba 2 watakuwa Brantare Hall na oktoba 3 watakuwa katika ukumbi wa Madeko Masasi, Oktoba 4 Nachingwea na 5 watakuwa Nyongoro Hall, Ruangwa.

Mhamila amesema kuwa mbali na utambulisho wa albamu hiyo, bendi hiyo pia itatoa fursa kwa wapenzi wake wa mikoa hiyo kwa lengo la kusikilizishwa vibao vipya ikiwemo Dawa ya deni kulipa na Lipi Jema vilivyoimbwa na wasanii mahiri akiwamo Edo Sanga.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, September 29, 2010 | | Permalink | Maoni 0

KAMA UNAHITAJI KURUDISHA FILE ZILIZOPOTEA KWENYE FLAsh

Programmed virus:

Watu wengi sana kwa sasa wanalalamika virus wamekula mafaili (Files and folder) kwenye flash drive.

Solution ipo kama unataka kuwa safe: KURUDISHA FILE ZILIZOPOTEA

maelezo machache:

There are some virus that will cause destruction such as encrypting recently used files so you are forced to buy the decryption key from the virus programmer.(from eastern Europe(..) and others country)

Then there’s another type of virus such as BDS.Mirc.Backdoor that will hide your documents files by setting the hidden and system attributes to the file. You can still see the files if you set to show hidden files and folders plus disabling hide operating system files. If the virus is capable of restricting Folder Options, chances are you think that your files has been wiped out by the virus but in fact it is hidden in your system.

Contact: DON COMPUTER CARE SERVICES

0787-291773 begin_of_the_skype_highlighting 0787-291773 end_of_the_skype_highlighting OR O716-291773

LOCATION: BHESCO BUILDING 1ST FLOOR, NEAR TO CHEF'S PRIDE RESTAURANT (DAR ES SALAAM)


KAMA UNAHITAJI KURUDISHA FILE ZAKO MUHIMU,

FOR BEST COMPUTER AND MEMORY STICKY SECURITY IN TANZANIA ,
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, September 29, 2010 | | Permalink | Maoni 1

mchango wako muhimu kwangu/nilipenda kusomea nchini australia.!

HABARI YAKAZI, KAKA MIMI NIKIJANA MWENYE UMRI WA MIAKA 26, NINA ELIMU YA FORM FOUR DARAJA LA TATU .

KAKA KAMA ILVYO KAWAIDA WIMBIKUBWA LA VIJANA WANA MAIZA KIDATO CHA NNE ILA NAMNA YA KUJIENDELEZA INA KUA NGUM KUTOKANA

NA HALI ZA KIUCHUMI.

NIWAZI NIMEJARIBU KUJIKUSANYA KWAKUFANYA KIBARUWA NA MPAKA SASA NINA $2000. JE NICHUO KIPI NINAWEZA KUPATA ELIMU YA I.T. INFORMATION technology katika ngazi za shahada nje ya nchi. Please naomba mchango wako wa mawazo.

Regards,

Mahuba H. Hilaly

Vodashop Consultant- Kigoma

Mob:(+255) 752 855 116 begin_of_the_skype_highlighting (+255) 752 855 116 end_of_the_skype_highlighting

Email:mhilaly@vodacom.co.tz

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, September 29, 2010 | | Permalink | Maoni 7

MSAADA TUTANI

Nina msaada ninaotaka kusaidiwa na watanzania wenzangu hasa walio Tanzania japokuwa hata wanje ya Tanzania nao waweza changia. Mim nipo huku ughaibuni kwa mda mrefu kidogo ila kwa sasa nataka nirudi nyumbani na kuanzisha biashara zangu binafsi ambazo zitakuwa zinahusika na uingizaji wa bidhaa ndani ya Tanzania kutoka USA, Je ni aina gani ya bishara ninayoweza kufanya yenye manufaa kwangu na watanzania?, ambayo itahusu mambo makuu matatu MAVAZI, CHAKULA NA MALAZI

Nitashukuru kwa mawazo na michango yenu!!!!!

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, September 29, 2010 | | Permalink | Maoni 5

kilimo kwanza.!

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, September 29, 2010 | | Permalink | Maoni 1

jiliwaze na less wanyika.!

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Wednesday, September 29, 2010 | | Permalink | Maoni 0

TANGAZO

Tuesday, September 28, 2010

TUPO KARIAKOO MTAA WA LINDI NA SWAHILI GEREZANI , UKIFIKA MAKUTANO YA MTAA WA LINDI NA SWAHILI UTAKUTA TRANSFOMA YA UMEME YA TANESCO , SISI TUNATIZAMANA NA TRANSFOMA, ULIZIA DUKA LA KOMPYUTA LA BRAND COMPUTER SOLUTIONS

bei zetu zinaanzia 15,000 na kuendelea kutokana na urefu wa mkanda wako , na kama ni wa siku nyingi sana mchafu sana tunajaribu kuubadilisha na kuwa dvd..


tupo wazi kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa kumi na moja na nusu jioni , siku zote za wiki mpaka jumapili tupo wazi
karibuni wote
www.bcstz.com

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, September 28, 2010 | | Permalink | Maoni 3

dr gharib bilal atua mbeya,aanza kampeni zake mjini humo leo.

Mgombea Mwenza wa urais Dk. Mohamed Gharib Bilal, akizungumza na Jeras Fungo, ambaye ni mlemavu wa miguu Mkazi wa Kijiji cha Ihai, Kata mpya ya Ihai, aliyefika katika mkutano wa kampeni kijiji cha Chimala, baada ya kumalizika kwa mkutano huo uliofanyika katika eneo la Stendi ya zamani ya Mabasi Wilaya ya Mbalali Mkoani Mbeya leo.
Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilala, akimnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Mbalali, Modestus Kilufi, wakati alipokuwa akifanya mkutano wa kampeni kwenye eneo la Stendi ya zamani ya Mabasi Wilaya ya MbalaIali leo.
Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya Viongozi wa CCM wa Kijiji cha Chimala Isitu, wakati alipowasili kwenye eneo la Stendi ya zamani ya mabasi ya Chimala, Wilaya ya Mbalali Mkoa wa Mbeya kufanya mkutano wa kampeni leo.
Wananchi wa Kijiji cha Chimala Wilaya ya Mbalali Mkoani Mbeya, wamsikiliza Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akifanya mkutano wa kampeni katika kijiji hicho.
Wananchi wa Kijiji cha Chimala Wilaya ya Mbalali Mkoani Mbeya, wakishangilia wakati Mgombea Mwenza wa urais wa CCM, Dk. Mohamed Gharib Bilal, alipokuwa akifanya mkutano wa kampeni katika kijiji hicho.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, September 28, 2010 | | Permalink | Maoni 0

UNIQUE ENTERTAINMENT PRESENTS: GIRAFFE UNIQUE MODEL 2010

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, September 28, 2010 | | Permalink | Maoni 0

kumekucha usiku wa kanga za kale,kurindima ijumaa hii .

Moja ya vazi la kanga litakalooneshwa siku hiyo jukwaani.
Mbunifu mkongwe wa mavazi hapa nchini,Mama Asia Idarous Hamsini wa Fabak Fashions akizungumza leo asubuhi na waandishi wa habari kuhusiana na onyesho lake la usiku wa kanga za kale 2010.

===== = ==== ===== ====
ASIA IDAROUS FABAK FASHIONS WANAKULETEA (USIKU WA KANGA ZA KALE-2010 ) SIKU YA IJUMAA TAREHE 1 OCTOBA NDANI YA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE VIP HALL .

KUTAKUWEPO NA BURUDANI YA JAHAZI MODERN TAARAB KWA UDHANIMI WA TUSKER LAGER, MICHUZI BLOG, ANTELOPE TOURS, VAYLE SPRING, EVENTLIGHTS, MYRIAD, BIG SOLUTION, CHANNEL TEN, MAGIC FM, CLOUDS FM, MLIMANI TV, TBC1, I-VIEW PHOTOGRAPHY,

SHEAR ILLUSION, NEW HABARI CORPORATIONS, MICHUZIJR BLOG, FULL SHANGWE, 8020 BLOG, ABAYA CENTER, NA GEMA SOUND. NI ONYESHO LA MAVAZI YA KANGA NA VIONJO VYAKE.

NYOTA WAIMBAJI WA TAARAB KAMA KHADIJA KOPA, RUKIA RAMADHAN, SABAH MUCHACHO NA BABY MADAHA WA BSS WATATUMBUIZA PAMOJA NA HAYO WABUNIFU WA MAVAZI PAMOJA NA MASTAR KIBAO WATAPANDA JUKWAANI KUONYESHA MAVAZI YA KANGA.

MADHUMUNI YA ONYESHO HILO NI KUKUZA HADHI YA KANGA KWA NI MOJA YA VAZI LA UTAMADUNI KWA MTANZANIA, KIINGILIO NI 10,000 NA 20,000 KWA VITI MAALUMU, PIA MAVAZI YATAUZWA NA VIONJO VYAKE BAADA YA SHOW.

KARIBUNI NYOTE AKINA MAMA NA AKINA BABA TUFURAHI KWA PAMOJA NA UKIPENDA UJE NA VAZI LA KANGA ASANTENI. KWA MAWASILIANO KAMA UNATAKA KUUZA KANGA ZAKO AU VIONJO VYAKE PIGA SIMU NO 0713263363 AU 0784263363.
Pichani kulia ni Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa kampuni ya bia ya Serengeti,Bw. Iman Lwinga akizungumza machache mbele wa waandishi wa habari leo asubuhi ndani ya ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Regency,jijini Dar kuhusiana na udhamini wao kupitia bia yao ya Tusker ndani ya onesho hilo la Usiku wa kanga za kale 2010.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, September 28, 2010 | | Permalink | Maoni 0

Orodha ya PILI ya waliochaguliwa na TCU kujiunga na Vyuo Vikuu

Monday, September 27, 2010
Kwa wale waliokuwa na wakiulizia kuhusu vyuo vingine kwa waliochaguliwa kujiunga Vyuo Vikuu, TCU wametoa orodha ya pili na unaweza kujipakulia nakala kupitia linki hii: http://bit.ly/tcu2010
Subi
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, September 27, 2010 | | Permalink | Maoni 0

jk atua shinyanga kwa staili ya pekee,aunguruma ndani ya uwanja wa Kambarage jioni ya leo .

Mgombea ubunge wa CCM jimbo la Shinyanga mjini akiwa na mkewe baada ya kunadiwa na JK uwanja wa Nyerere mjini Shinyanga leo jioni .
JK akinadi Bw. Masele mgombea ubunge shinyanga mjini
JK akihutubia umati wa wanashinyanga leo jioni
Ze original Comedy wakiburudisha uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga leo.
Sehemu ya Umati wa wananchi waliojitokeza kmumsikilia JK leo uwanja wa Kambarage
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili uwanja wa Kambarage Shinyanga Mjini tjioni ya leo tayari kwa mkutano wa kampeni. Mheshimiwa Kikwete aliwateka maelfu ya wana Shinyanga alipoamua kuingia uwanjani hapo bila magari.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, September 27, 2010 | | Permalink | Maoni 0
Idadi ya watu