watu wanazusha tuu,sina mahusiano ya kimapenzi na msanii diamond.!

Tuesday, August 31, 2010

Muigizaji mahiri wa filamu hapa Bongo,ambaye wapenzi na washabiki wake wamekuwa wakimfananisha na muigizaji mwenzake nyota,Irene Uwoya,ajulikane kwa jina la Jackline Wolper amepinga vikali kuwa hana mahusiano yoyote ya kimapenzi na msanii wa muziki wa kizazi kipya aitwaye Diamond anaetesa na wimbo wake Mbagala.

Jackline ameyatamka hayo ndani ya kipindi cha Filamu kiitwacho TAKE ONE mtangazaji wake akiwa Zamaradi Mketema,kinachorushwa na Clouds TV kila siku ya Jumanne kuanzia saa tatu mpaka tatu na nusu usiku,Muigizaji huyo ameweka bayana kutokana na baadhi ya magazeti kuandika habari za mahusiano yao yaliyohusu mapenzi,habari ambazo hazina ukweli wowote.

"Unajua watu wakilishikilia jambo lao na kuanza kulisambaza kwa wengine si rahisi kuwazuia ,lakinni inafika mahali unawaacha waendelee kusema,ukweli unabaki pale pale kwamba mimi sina mahusiano ya kimapenzi na Diamond",Jackline amesema na kuongeza kuwa walikuwa na mahusiano ya kawaida tu ambayo yalitokea wakati wanaandaa filamu yao mpya.

Mbali ya mahojiano hayo Muigizaji huyo mwenye haiba ya ucheshi amekiri wazi kuwa anaogopa sana Chura, "ukitaka nitetemeke na nijihisi kufa wewe niletee chura tu,utakuwa umeniweza ile mbaya,kweli naogopa sana Chura",alisema Jackline huku akicheka.

Jackline amewaasa wanawake wenzeke kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kuwataka
wapendane na kuheshimiana,aidha ameongeza kuwa waache kuongea kitu ama jambo kama hawalijui badala yake ni vyema wakakaa kimya na kufanya mambo ya kimaendeleo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 1

mama salma kikwete ziarani mkoani singida leo

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA),Mama Salma Kikwete akimtambulisha mgombea Ubunge kupitia CCM Kondoa Mashariki Mkoa wa Singida,Bw.John Lwaji leo mjini humo.Mama Salma yupo mkoani Singida kuwahamasisha wanachama wa UWT kuhusu uchaguzi utakaofanyika hivi karibini mwaka huu.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete akiwa amewabeba watoto mapacha Agost 31,20101 alipowasili katika kijiji cha Kinya Mshindi Mkoani Singida kuanza ziara yake ya kuwahamasisha wanawake kuhusu uchaguzi mkuu.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete akikagua gwaride leo mara alipowasili Itigi Mkoani Singida katika shughuli zake za kuwahamasisha wanawake wa UWT kuhusu Uchaguzi Mkuu mwaka huu.Picha kwa hisani ya Mwanakombo Juma-MAELEZO.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 2

mkutano wa marais wastaafu wa afrika wakutana kuzungumzia maboresho ya ardhi jijini dar le

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Mauritius Karl Auguste Offmann (kushoto) akisoma maazimio ya mkutano wa marais wastaafu wa Afrika juu ya maboresho ya ardhi kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam . Katikati ni Waziri Mkuu Mstaafu wa Msumbiji Luisa Diogo na kulia ni Mkurugenzi wa kuhifadhi Kumbukumbu za Marais Wastaafu wa Afrika Balozi Charles Stith.

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa (kushoto) akimsikiliza Katibu Mtendaji wa African Forum Dr. John Tesha mara baada ya kumaliza mkutano wa marais wastaafu na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo uliokuwa unaelezea mikakati ya maboresho ya ardhi barani Afrika.

Rais Mstaafu wa Zambia Dr Keneth Kaunda katikati akisalimiana naWaziri Mkuu mstaafu wa Mozambique Luisa Diogo kuliani Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Mauritius Karl Auguste Offmann.


Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa (kushoto) akitoa ufafaunuzi leo jijini Dar es salaam kwa wanahabari mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Marais wastaafu wa Afrika uliokuwa unajadili juu ya maboresho katika sekta ya ardhi barani Afrika. Kulia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 1

habari njema kwa wajasiriamali.

Michuzi Jr,

Natumaini unaendelea vizuri na shughuli zako. Nina ujumbe hapa ambao itakuwa vema ukiwafikia Watanzania wengi zaidi, hasa wajasiriamali:

__________________________________________

According to a recent article in The Guardian, I/O Ventures, an angel investment fund and business incubator based in San Francisco is working with the government to setup a local incubator in Dar es Salaam.

For those unfamiliar with the concept of incubators, these are basically programs led by venture capital (VC) firms to develop early stage companies with seed capital, mentoring, coaching as well as assistance with resources such as office space and technology infrastructure. In return firms usually get a small stake in your company. In the case of I/O ventures, this comes with access to an exclusive network of mentors including founders of Silicon Valley giants such as Youtube and MySpace.

What does this development tell us? Investors and technologists are constantly seeking new markets and fresh talent. Tanzania with its stable environment, burgeoning economy and army of fresh talented graduates is a prime feeding ground. Tanzanians need to wake up and realize that foreigners have already realized the potential of our country even if we are still dozing. So if you have a great idea, are passionate about it and have some form of a business plan, wake up and get started.

If you have an idea, don’t know how to get started or are stuck on a problem reach out to myself or any member of the VijanaFM team and we will gladly help or point you in the right direction.

For more info/questions: http://vijana.fm

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

yale yale:zimwi sugu la mlimani city lazidi kuwasumbua wateja wake.! wizi wa loptop wakithiri eneo hilo


Salama kiongozi?

Hiyo picha ni jana majira ya saa kumi na moja jioni pale mlimani city mshkaji wangu kapigwa laptop kwa style ya kuvunjiwa kioo cha nyuma, alishuka kama dakika kumi tu kwenda kwenye ATM ya Exim bank na laptop akaificha chini ya kiti cha gari ile kurudi ndio akakuta ameshapigwa laptop na alivyowaeleza askari wa pale wakamjibu wao hawahusiki na issue za wizi sasa tukashindwa kuelewa kama hawahusiki na masuala ya wizi wako pale kufanya nini!!!!

Tukaambiwa na Taxi drivers pale kuwa last week alikamatwa mwizi ameiba laptop kwenye gari akapewa kisago askari wale wale wakamsaidia asiendelee kupigwa halafu akaachiwa na hakupelekwa hata polisi. TUTAFIKA???
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 5

rais karume afungua mkutano wa majaji wa kimataifa dhidi ya ugaidi nchi za afrika mashariki na kati.

RAIS wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, akifungua mkutano wa Majaji wa nchi za Afrika Mashariki na Kati, kuhusu mapambano dhidi ya ugaidi katika ukanda huo na uhalifu wa kimataifa,leo katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Amani Abeid Karume (kulia) akishiriki kuimba wimbo wa taifa wa Tanzania wakati wa ufunguzi wa mkutano wa siku tatu wa Kikanda wa Kimataifa wa kukabiliana na ugaidi na uhalifu wa kimataifa leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Augustino Ramadhani. Mkutano huo unaendelea katika Hotel ya Golden Tulip na unahudhuriwa na Majaji kutoka ndani na nje ya Tanzania.
Washiriki wa mkutano wa siku tatu wa Kikanda wa Kimataifa wa kukabiliana na ugaidi na uhalifu wa kimataifa unaendelea nchini Tanzania wakimsikiliza Rais Amani Abeid Karume wakati wa sherehe fupi za ufunguzi uliofanyika katika Hotel ya Golden Tulip na kuhudhuriwa na Majaji kutoka ndani na nje ya Tanzania.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

mufti mkuu wa zanzibar azikwa leo


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk Amani Abeid Karume,(wa tano kushoto)alijumuika na Viongozi wengine katika swala ya Maiti ya Marehemu Mufti Mkuu wa Zanzibar,Sheikh Harith Bin Helef,katika Msikiti wa Mwembeshauri leo.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

kambi popote ya clouds tv kuzinnduliwa kesho.

Kesho ni Fantastic wednesday ya KAMBI POPOTE ya ClOUDS TV na ANTONIO NUGA'S (pichani) rasmi kuzinduliwa hadharani hapa hapa mjengoni,Mikocheni jijini Dar.kipindi hicho cha burudani na matembezi kitaruka hewani LIVE kupitia CLOUDS TV.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

pingamizi la chadema dhidi ya mgombea urais wa ccm kujulikana baada ya siku tano


Msajili wa Vyama Vya Siasa Nchini John Tendwa amesema atatoa uamuzi wake dhidi ya malalamiko yaliyowasilishwa ofisini kwake jana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuhusu mgombea wa urais kupitia chama cha mapinduzi (CCM) baada ya siku tano.

Bwana Tendwa ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es salaam leo baada ya kupokea malalamiko hayo.

‘’Nitatoa maamuzi hayo baada ya kupokea maelezo kutoka kwa mlalamikiwa dhidi ya mlalamikaji yaliyowasilishwa,na nitatoa nakala ya maamuzi kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi,Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi na Katibu Mkuu wa chama cha CHADEMA’’,Alisema Tendwa.

Akifafanua suala hilo Tendwa amesema baada ya maamuzi yake mlalamikaji na mlalamikiwa kama hawataridhika na uamuzi wake wanayo haki ya kwenda kutafuta haki yao kwenye vyombo vya sheria.

Aidha Msajili huyo wa Vyama ameongeza kuwa amepokea malalamiko hayo kwa mujibu wa sheria ya gharama za uchaguzi inachomkataza mgombea yeyote ambaye yeye mwenyewe, wakala wake au Chama chake kitafanya kitendo ambacho kimekatazwa kama ilivyoelekezwa kwenye sheria hiyo atakuwa au kitakuwa kimepoteza sifa za kushiriki mchakato wa uteuzi au uchaguzi.

Pingamizi hilo liliwasilishwa jana ofisi ya msajili huyo na Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika wakimlalamikia Mgombea urais wa chama cha mapinduzi,Jakaya Mrisho Kikwete kutumia madaraka yake kutoa ahadi kwenye kampeni na kutangaza nyongeza ya mshahara kwa wafanyakazi wakati wa kampeni.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

marlow na remix yake jukwaani.!

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

mnyika aanza mbio za kampeni jimbo la ubungo

Mgomea Urais kwa tiketi ya CHADEMA,Dr. Willblod Slaa akimpa baraka zote na kumnadi wanachama na wapenzi wa chama hicho Mgombea ubunge wa jimbo la Ubungo, John Mnyika katika kampeni zake za Jimbo la Ubungo na kumhakikishia kuwa naye bega kwa bega katika kuhakikisha wanashinda.
Mpendazoe naye alikuawepo kumnadi Mnyika kwa wananchi wa Ubungo katika ufunguzi wa kampeni za chama hicho Kimara Suca.
Wasanii wa muziki wa Bongo Freva wakiongonzwa na mgombea Ubunge wa jimbo la Mbeya Mjini,Joseph Mbilinyi a.k.a Mr II (SUGU) wakilishambulia jukwaa la ufunguzi wa kampeni za Mnyika Kimara Suca
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 1

jarida maridhawa number 10 laingia mitaani.!



SAFARI HII KUNA EXCLUSIVE INTERVIEWS TANO HAIJAWAHI TOKEA,
HAYA NDO MAPINDUZI HALISI

NUMBER 10 USO KWA USO NA:

1. McDONALD MARIGA-KIUNGO WA INTER MILAN NA KENYA
2. PETR CECH- GOLIKIPA WA CHELSEA
3. RUUD GULLIT- NYOTA WA ZAMANI WA UHOLANZI
4. TONU PULIS-KOCHA WA STOKE CITY
5. JABIR AZIZI -KIUNGO MPYA WA AZAM FC
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

chadema waweka pingamizi dhidi ya mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete


Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, akiwa ameshika nakala ya pingamizi dhidi ya mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete, wakidai mgombea huyo amekiuka kanuni za sheria ya gharama za uchaguzi baada ya kuiwasilisha kwa msajili wa vyama vya siasa jana jijini Dar es Salaam.Picha na Zacharia Osanga

Geofrey Nyang’oro

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeteketeza azma yake ya kumwekea pingamizi mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete.

Taarifa zimeeleza kuwa chama hicho kiliwasilisha pingamizi hilo kwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini jana saa 7:30 mchana.Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho John Mnyika, ndiye aliyewasilisha pingamizi hilo.

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa alipoulizwa hakutaka kukubali au kukataa kuliona pingamizi hilo na akasema atazungumzia suala hilo leo.

Awali Chadema ilipanga kuweka pingamizi hilo la kutaka Kikwete azuiwe kugombea urais, Agosti 27 mwaka huu, lakini, ilisitisha kwa kile ilichoeleza kuwa inasubiri mambo mengi zaidi ambayo wangeyaingiza kwenye pingamizi hilo.

Chama hicho awali kilitaka kuweka pingamizi hilo kwa kile kilichoeleza kuwa Rais Kikwete amekiuka Sheria ya Gharama za Uchaguzi kwa kutangaza nyongeza ya mishahara ya wafanyakazi kwenye kampeni.

"Tulishindwa kupeleka pingamizi hilo jana kwa sababu tumesikia kwamba huku anakoendelea na kampeni zake, mgombea huyo ameendelea kufanya makosa mengine ambayo tutataka tuyaingize kwenye pingamizi hilo," alisema Mnyika mwishoni mwa wiki. Habari zaidi bofya hapa
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Tuesday, August 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

timu ya taifa stars kutimka kesho kwenda algeria

Monday, August 30, 2010
Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF) Leodgar Tenga (Katikati) akitoa nasaha zake kwa wachezaji wa timu ya Taifa 'Taifa Stars' hawapo pichani wakati akiwaaga, ambapo kesho wataondoka nchini kwenda Algeria kuanza Kampeni ya kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika (CAN).Mechi hiyo itafanyika Septemba 5.kwa habari zaidi ingia ndani ya Bongoweekend
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, August 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

baada ya kutikisa na lovely gamble,sasa Urban Pulse waja na kitu kipya


Salam Ankal,

Mwezi Juni mwaka huu tuzo maarufu ya kimataifa iitwayo Ashden Awards iilitolewa kwa wahusika kadhaa duniani zikiwepo nchi za Afrika Mashariki. Tuzo hiyo hutolewa na shirika maalum lililoundwa na duka maarufu la matajiri wa Uingereza yaani Sainsbury Kutoka katika Ashden Trust Charity ambapo mlezi wake akiwa ni Prince Charles.

Lengo lake ni kusaidia kurekebisha na kuboresha mazingira duniani . Tuzo ya mwaka huu ilitolewa kwa watafiti na wabunifu waliotengeneza zana za kutengeneza umeme kutokana na nguvu asilia za jua yaaani Solar Energy.

Ingawa wabunifu walitoka mataifa mbalimbali ya Marekani, Asia na Afrika washindi pia walihusisha Kenya, Uganda na Tanzania.Umeme Jua, Bio gas( Gas Itokayo kwenye kinyesi cha ng'ombe) ni zana ambayo itawasaidia watu maskini hasa wanaotoka nchi kama yetu Bongo vijijini.

Baada Ya Mafanikio makubwa la movie ya £ovely Gamble Urban Pulse wakishirikiana na Msanii/ Mhariri Freddy Macha Wamepewa mzigo mwingine wa kutengeneza documentary ambayo itakuwa hewani tarehe 2 sept 2010 na kurushwa katika tv za hapa ukerewe na mabara mengine ya ulaya.

Hivyo basi utawala wa Urban Pulse Unawaletea trailer ya documentary hiyo kwa kubofya clip video hiyo hapo juu

Baada ya uzinduzi tutawapatia kipindi chote

Asanteni sana

Urban Pulse Creative

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, August 30, 2010 | | Permalink | Maoni 3

FILAMU ZA KIBONGO MAADILI YAKE NI KIFO KWETU?

Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Marerego (Kushoto) akisisitiza jambo wakati akichangia mada kwenye Jukwaa la Sanaa kuhusu Filamu na Maadili ya Mtanzania.Kulia ni Mwasilishaji wa Mada Richard Kallling,Rais wa Chama cha Wamiliki wa Video Library.
Mwongozaji chipukizi wa Filamu nchini, Christian Kauzeni ambaye pia ni msanii kutoka Kundi la Kidedea akitoa mchango wake kwenye Jukwaa.
Mtaalamu na Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam anayefanya masters yake kwenye masuala ya sanaa, Issa Mbura akifafanua juu ya utafiti wake alioufanya kuhusu filamu za kibongo.
Mwalimu Rashidi Masimbi akichangia kwa hisia kali juu ya Maadili katika Filamu zetu.Kulia kwake Ni Mkongwe wa Muziki wa Dansi,Kassim Mapili.

Sehemu ya umati wa wadau wa sanaa waliohudhuria kwenye Jukwaa la Sanaa Jumatatu hii.

FILAMU ZA KIBONGO MAADILI YAKE NI KIFO KWETU?


Wadau,kama kawaida leo hapa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwenye Jukwaa la Sanaa kulikuwa na Mjadala Mkali kuhusu Filamu za Kibongo na maadili yake kwa jamii za kitanzania.

Mjadala huo uliohudhuliwa na zaidi watu 100 na kuchokozwa na Rais wa Chama Cha Wamiliki wa Video Library,Richard Kallinga, ulijikita kwenye haja ya waandaaji wa filamu za kibongo kutengeneza filamu zenye ubora, zenye kubeba maadili ya mtanzania, zilizo na uhalisia wa maisha yetu ya kila siku,zisizokuwa za kuiga kutona Nollywood (Nigeria), zenye ujumbe unaoeleweka na kwa ujumla zenye mvuto.

Katika mjadala wake, wadau wengi walisema kwamba, Industry ya Filamu hapa Bongo imeajiri vijana wengi na inafanya vizuri ila hawakusita kutaja matatizo sugu ambayo lazima yafanyiwe kazi ili kubadili industry hii ambayo hapana shaka imekuwa kimbilio la wengi.Matatizo yaliyoainishwa ni pamoja na:

1. Wizi wa kazi za wasanii (Piracy) ambapo ilishauriwa kwamba Cosota lazima ibadilike, ipewe meno na iweze kupambana vilivyo na tatizo hili ambalo limekuwa likiwakwamisha wasanii wengi.


2. Kunakiri (copying) kazi za wasanii wa Nigeria na kutumia muziki (Sound Tracks) za wasanii wa muziki bila idhini yao.Katika haya wasanii wa Filamu wameshauriwa kuwa makini kwani sheria ya Hakimiliki inaweza kuwafunga.Kwa ujumla wasanii walishauriwa kuwekeza ubunifu binafsi na kubeba uhalisia wa sanaa yetu badala ya ilivyo sasa ambapo filamu zetu zimekuwa zikifanana fanana na zile za Nigeria.


3. Uchafu wa Filamu-Wadau wengi wamesema kwamba, filamu za kibongo zimekuwa na maadili mabovu yanayotokana uvaazi wa vichupi kwa wasanii wa kike, uoneshaji wa matendo ya faragha (mapenzi) mara kwa mara, script zenye kushabikia matendo maovu na yasiyofaa kwa jamii nk.Wadau walishauri Bodi ya Filamu, vituo vya TV na wasanii wenyewe kuhakikisha wanadhibiti filamu zisizo na maadili kwani zimekuwa zikitia aibu/kichefuchefu.Ilielezwa kwamba, baadhi ya filamu hazibebi uhusika wenye ufanano na maisha/maadili ya kitanzania.


4. Wasanii kuact maisha ya juu mara kwa mara tofauti na uhalisia wao.Mtaalamu wa Filamu kutoka Chuo Kikuu,Bw.Ndunguru alieleza kwamba,filamu nzuri ni ile inayobeba uhalisia.Aliongeza kwamba, wasanii wanapenda kutumia magari ya gharama kama Hammer, majumba ya thamani, maisha ya anasa nk. kwenye filamu zao kueleza uhalisia usiokuwepo katika maisha yetu.


5. Ubunifu mdogo wa waongozaji, watengenezaji na mameneja wa Filamu ambao umekuwa ukiwafanya muda mwingi wautumie kunakiri (copying) kazi za kigeni.Ilishauriwa kwamba, wataalamu hawa wafikirie walau kupata elimu,semina na mafunzo ya muda mfupi kwenye taaluma zao badala ya ilivyo sasa.


6. Kutokuzingatia mikataba kwenye kazi zao.Ilielezwa kwamba, wasanii wengi wamekuwa wakiwalalamikia wasambazaji wa kazi (Distributors) huku wakiwa wamesainiana mikataba.Kumbe tatizo lililopo ni wasanii wenyewe kusaini mikataba kwa pupa, uroho wa fedha, bila kuisoma mikataba husika na wakati mwingine bila kuandikiana bali kwa mazungumzo tu.Ilishauriwa kwamba, wasanii lazima wasimamie mikataba na kuhakikisha inawanufaisha.Wasilalame tu, wachukue hatua pia.


Picha/Habari na Afisa Habari wa BASATA,Alistide Kwizela


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, August 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

mgombea mwenza wa urais ccm dk bilal ndani ya nanyumbu na masasi

Mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Bilal akizungumza na wanachi wa Wilaya ya Nanyumbu baada ya kuingia mpakani mwa wilaya hiyo na Masasi leo.
Kamanda wa Chipukizi wa Wilaya ya Masasi, Fatuma Rajab akimvisha skafu Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal alipokuwa akiingia mpakani mwa Wilaya ya Masasi akitokea Wilaya ya Newala leo mchana.
Mgobea Mwenza wa urais, Dk. Mohamed Gharib Bilal akisalimiana na wananchi na viongozi wa Chama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Masasi, baada ya kuingia mpakani mwa wilaya hiyo na Newala, leo.Picha kwa hisani ya Muhidin Sufian.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, August 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

cuf walivyozindua rasmi mbio za kampeni zao kidongo chekundu

siku CUF walipozindua rasmi kampeni za uchaguzi mkuu
Mwenyekiti wa CUF na mgombea urais wa chama hicho cha wananchi Profesa Ibrahim Lipumba akisalimia wanachama wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni katika viwanja vya Kidongo Chekundu jijini Dar.
Profesa Lipumba akisalimiana na Mh. Hamad mmoja wa wanachama na viongozi waandamizi wa CUF.
Sehemu ya umati wa wana CUF waliofika kwenye mkutanoni chama hicho kwenye viwanja vya Kidongo Chekundu jijini Dar.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, August 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

masha afungua mkutano wa mwanaka wa maofisa waandamizi wa jeshi la magereza

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Lawrence Masha akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa maofisa waandamizi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara leo jijini Dar es salaam.
Kamishna Mkuu wa Magereza Augustino Nanyaro akimkaribisha Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Lawrence Masha jana jijini Dar es salaam kwa ajili ya ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa Maofisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara leo jijini Dar es salaam.

Picha na Tiganya Vincent-MAELEZO-Dar es salaam

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, August 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

Mama Mwanamwema amnadi mgombea urais wa ccm zanzibar dk shein

Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe. Mama Mwanamwema Shein kulia, akisalimiana na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi na Wananchi wa Mkoa wa kusini Unguja alipowasili katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kati Unguja Dunga kwa ajili ya kuwahutubia wananchi hao mkutano wa ndani leo.

Mke wa Makamu wa Rais na Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe. Mama Mwanamwema Shein, akihutubia Wanawake wa Jumuiya ya UWT Mkoa wa Kusini Unguja kwenye mikutano ya ndani ya CCM uliofanyika leo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kati Dunga.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, August 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

ndesamburo naye atikisa moshi mjini .!

Mgombea Ubunge Jimbo la Moshi mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Philemon Ndesamburo akihutubia wananchi wa Jimbo hilo waliojitokeza wakati wa uzinduzi wa kampeni za chama hicho hivi karibuni kwenye viwanja vya Manyema.
Umati mkubwa wa wafuasi wa Chadema na Wananchi wa Jimbo la Moshi mjini waliofurika viwanja vya Manyema katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni wa mgombea Ubunge wa chama hicho,Philemon Ndesamburo hivi karibuni.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, August 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

MBWANA MATUMLA APOTEZA UBINGWA WA WBC UKRAINE

BONDIA Mbwana amepoteza kwa point ubingwa wa WBC international alipopambambana jana nchini Ukraine na kupata pointi 120-118,119-109 na 116-114 .Ahsante Juma Ndambile -Manager.Mambo mengine kwa habari za michezo bofya mamapipiro.blogspot.com.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, August 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

Msiba Ireland na Tanzania


Hayati Mnomba Jaidi enzi za uhai wake


Kwa niaba ya familia na ukoo wa Njaidi, tunasikitika kutangaza kifo cha ndugu na rafiki yetu, MNOMBA NJAIDI kilichotokea ghafla Ijumaa ya tarehe 27 August 2010 huko Ireland. Marehemu alipendwa sana na wengi lakini Muumba alimpenda zaidi - tunamwombea mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amina.

Maombi ya Ushirikiano:
Kwa niaba ya familia na marafiki wa marehemu, tunaomba msaada wa hali na mali toka kwa watanzania wote waliowahi na ambao hawakuwahi kumfahamu. Michango yenu ya hali na mali inatakiwa ili kufanikisha usafirishaji wa mwili wa ndugu na rafiki yetu kuelekea Tanzania (Toka Ireland).

Kwa michango tafadhali tumia details zifuatazo;

United Kingdom:
Account name: Y W Mirambo
Account number: 726 59 181
Sort Code: 09-01-26
Bank: Santander Bank

International transfer number: Above details zitafaa lakini namba tutaweka hivi karibuni kurahisisha International transfers

Simu: Yusuph +44 7972256826 begin_of_the_skype_highlighting +44 7972256826 end_of_the_skype_highlighting, Munde +44 7869410750 begin_of_the_skype_highlighting +44 7869410750 end_of_the_skype_highlighting, Chambi +44 7900626410 begin_of_the_skype_highlighting +44 7900626410 end_of_the_skype_highlighting

ASANTENI KWA NIABA YA FAMILIA YA MAREHEMU NA MUNGU AWAJAALIE NA AWAONGEZEE SABA MARA SABINI

Mungu alitoa na Mungu ametwaa
Jina lake litukuzwe
- Amen!!
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, August 30, 2010 | | Permalink | Maoni 0

mgombea urais chama cha ccm mh jakaya kikwete akihutubia tunduma leo jioni

Sunday, August 29, 2010
Mgombea Urais Kwa tiketi ya Chama Cha mapinduzi,Mh Jakaya Kikwete akihutubia umati wa wakazi wa Tunduma jioni ya leo wakati akianza kampeni yake mkoa wa Mbeya.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, August 29, 2010 | | Permalink | Maoni 0

wanawake wakiwezeshwa wanaweza.

Mama muuza vyungu akichora vyungu vyake jioni ya leo maeneo ya barabara ya Kawe chini kama ambavyo wengi wamekuwa wakiita,tayari kwa kuwauzia wateja wake.Ama kwa hakika Wanawake wakiwezeshwa wanaweza,basi na wapewe fursa.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, August 29, 2010 | | Permalink | Maoni 1

kajua kalee kateremke mama..!

Jua lileee linaishia na giza tayari limekwishaingia.
Jua likihangaika kuzama jioni ya leo maeneo ya Kawe karibu na viwanja vya Tanganyika Pekaz
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, August 29, 2010 | | Permalink | Maoni 0

Chama cha nccr Mageuzi chazindua ilani yake ya uchaguzi leo


Pichani ni mgombea urais kwa Chama cha NNCR Mageuzi, Hashim Rungwe akionyesha ilani ya uchaguzi ya chama hicho wakati wa uzinduzi wa kampeni ya chama hicho leo jijini Dar.

CHAMA cha NCCR Mageuzi leo kimezindua ilani yake ya Uchaguzi huku kikitaja mambo 12 ambayo chama hicho kitaelekeza nguvu iwapo kitapewa ridhaa ya kuongoza nchi.Wakati wa uzinduzi huo Mwenyekiti wa chama hicho taifa James Mbatia alisema chama chake kitazindua kampeni zake kitaifa Septemba 11 baada ya mfungo wa ramadhani ili kutowakwaza Waislam ambao wako kwenye mfungo wa mwezi mtukufu.“Ajenda yetu kuu itakuwa ni katiba, tumeainisha mambo yatakayokuwemo kwenye katiba hiyo, hili ndilo nataka wagombea wetu mlizungumzie kwa kina,” alisema Mbatia.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, August 29, 2010 | | Permalink | Maoni 0

jk aziteka hisia za wakazi wa mpanda na sumbawanga

Mgombea wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM,Mh Jakaya Kikwete amefanya mkutano wa kampeni jana na kuhutubia katika uwanja wa Mandele mjini Sumbawanga,amb wakazi wa Sumbawanga walijitokeza kwa wingi kutoka vitongoji mbalimbali vya mji huo. Pichani Mh Jakaya Kikwete akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia chama cha CCM Bw. Hayeshi ambaye kama atashinda kuomngoza jimbo hilo atakuwa anachukua nafasi ya aliyekuwa mbunge wa Sumbawanga mjini Mzee Paul Kimiti aliyeng'atuka madarakani mara baada ya kulitumikia jimbo hilo kwa muda mrefu.
Mgombea Urais kwa chama cha CCM,Mh Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi mara baada ya kuwasili mjini mpanda na kufanya mkutano wa kampeni mjini humo jana.
Mgombea Urais kwa tiketi ya chama cha CCM,Mh Jakaya Kikwete akishuka kwenye Helkopta mara baada ya kuwasili Sumbawanga mjini tayari kwa mkutano uliofanyika jana kwenye uwanja wa Mandele mjini humo.
Wanachi wakiwa wamefurika ndani ya Uwanja wa Mandela-Sumbawanga
Wananchi wa mjini Sumbawanga wakimsubiri mgombea Urais kwa tiketi ya chama cha CCM,Mh Jakaya Kikwete kuwasili uwanjani hapo tayari kwa kuanza mkutano.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, August 29, 2010 | | Permalink | Maoni 1
Idadi ya watu