watu wanazusha tuu,sina mahusiano ya kimapenzi na msanii diamond.!

Jackline amewaasa wanawake wenzeke kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kuwataka





Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Mauritius Karl Auguste Offmann (kushoto) akisoma maazimio ya mkutano wa marais wastaafu wa Afrika juu ya maboresho ya ardhi kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam . Katikati ni Waziri Mkuu Mstaafu wa Msumbiji Luisa Diogo na kulia ni Mkurugenzi wa kuhifadhi Kumbukumbu za Marais Wastaafu wa Afrika Balozi Charles Stith.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa (kushoto) akimsikiliza Katibu Mtendaji wa African Forum Dr. John Tesha mara baada ya kumaliza mkutano wa marais wastaafu na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo uliokuwa unaelezea mikakati ya maboresho ya ardhi barani Afrika.
Rais Mstaafu wa Zambia Dr Keneth Kaunda katikati akisalimiana naWaziri Mkuu mstaafu wa Mozambique Luisa Diogo kuliani Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Mauritius Karl Auguste Offmann.
For those unfamiliar with the concept of incubators, these are basically programs led by venture capital (VC) firms to develop early stage companies with seed capital, mentoring, coaching as well as assistance with resources such as office space and technology infrastructure. In return firms usually get a small stake in your company. In the case of I/O ventures, this comes with access to an exclusive network of mentors including founders of Silicon Valley giants such as Youtube and MySpace.
What does this development tell us? Investors and technologists are constantly seeking new markets and fresh talent. Tanzania with its stable environment, burgeoning economy and army of fresh talented graduates is a prime feeding ground. Tanzanians need to wake up and realize that foreigners have already realized the potential of our country even if we are still dozing. So if you have a great idea, are passionate about it and have some form of a business plan, wake up and get started.
If you have an idea, don’t know how to get started or are stuck on a problem reach out to myself or any member of the VijanaFM team and we will gladly help or point you in the right direction.
For more info/questions: http://vijana.fm
RAIS wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, akifungua mkutano wa Majaji wa nchi za Afrika Mashariki na Kati, kuhusu mapambano dhidi ya ugaidi katika ukanda huo na uhalifu wa kimataifa,leo katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
Washiriki wa mkutano wa siku tatu wa Kikanda wa Kimataifa wa kukabiliana na ugaidi na uhalifu wa kimataifa unaendelea nchini Tanzania wakimsikiliza Rais Amani Abeid Karume wakati wa sherehe fupi za ufunguzi uliofanyika katika Hotel ya Golden Tulip na kuhudhuriwa na Majaji kutoka ndani na nje ya Tanzania.


Mgomea Urais kwa tiketi ya CHADEMA,Dr. Willblod Slaa akimpa baraka zote na kumnadi wanachama na wapenzi wa chama hicho Mgombea ubunge wa jimbo la Ubungo, John Mnyika katika kampeni zake za Jimbo la Ubungo na kumhakikishia kuwa naye bega kwa bega katika kuhakikisha wanashinda.
Mpendazoe naye alikuawepo kumnadi Mnyika kwa wananchi wa Ubungo katika ufunguzi wa kampeni za chama hicho Kimara Suca.
Wasanii wa muziki wa Bongo Freva wakiongonzwa na mgombea Ubunge wa jimbo la Mbeya Mjini,Joseph Mbilinyi a.k.a Mr II (SUGU) wakilishambulia jukwaa la ufunguzi wa kampeni za Mnyika Kimara Suca

Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, akiwa ameshika nakala ya pingamizi dhidi ya mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete, wakidai mgombea huyo amekiuka kanuni za sheria ya gharama za uchaguzi baada ya kuiwasilisha kwa msajili wa vyama vya siasa jana jijini Dar es Salaam.Picha na Zacharia Osanga
Geofrey Nyang’oro
Salam Ankal,
Mwezi Juni mwaka huu tuzo maarufu ya kimataifa iitwayo Ashden Awards iilitolewa kwa wahusika kadhaa duniani zikiwepo nchi za Afrika Mashariki. Tuzo hiyo hutolewa na shirika maalum lililoundwa na duka maarufu la matajiri wa Uingereza yaani Sainsbury Kutoka katika Ashden Trust Charity ambapo mlezi wake akiwa ni Prince Charles.
Lengo lake ni kusaidia kurekebisha na kuboresha mazingira duniani . Tuzo ya mwaka huu ilitolewa kwa watafiti na wabunifu waliotengeneza zana za kutengeneza umeme kutokana na nguvu asilia za jua yaaani Solar Energy.
Ingawa wabunifu walitoka mataifa mbalimbali ya Marekani, Asia na Afrika washindi pia walihusisha Kenya, Uganda na Tanzania.Umeme Jua, Bio gas( Gas Itokayo kwenye kinyesi cha ng'ombe) ni zana ambayo itawasaidia watu maskini hasa wanaotoka nchi kama yetu Bongo vijijini.
Baada Ya Mafanikio makubwa la movie ya £ovely Gamble Urban Pulse wakishirikiana na Msanii/ Mhariri Freddy Macha Wamepewa mzigo mwingine wa kutengeneza documentary ambayo itakuwa hewani tarehe 2 sept 2010 na kurushwa katika tv za hapa ukerewe na mabara mengine ya ulaya.
Hivyo basi utawala wa Urban Pulse Unawaletea trailer ya documentary hiyo kwa kubofya clip video hiyo hapo juu
Baada ya uzinduzi tutawapatia kipindi chote
Asanteni sana
Urban Pulse Creative
FILAMU ZA KIBONGO MAADILI YAKE NI KIFO KWETU?
Mjadala huo uliohudhuliwa na zaidi watu 100 na kuchokozwa na Rais wa Chama Cha Wamiliki wa Video Library,Richard Kallinga, ulijikita kwenye haja ya waandaaji wa filamu za kibongo kutengeneza filamu zenye ubora, zenye kubeba maadili ya mtanzania, zilizo na uhalisia wa maisha yetu ya kila siku,zisizokuwa za kuiga kutona Nollywood (Nigeria), zenye ujumbe unaoeleweka na kwa ujumla zenye mvuto.
Katika mjadala wake, wadau wengi walisema kwamba, Industry ya Filamu hapa Bongo imeajiri vijana wengi na inafanya vizuri ila hawakusita kutaja matatizo sugu ambayo lazima yafanyiwe kazi ili kubadili industry hii ambayo hapana shaka imekuwa kimbilio la wengi.Matatizo yaliyoainishwa ni pamoja na:
1. Wizi wa kazi za wasanii (Piracy) ambapo ilishauriwa kwamba Cosota lazima ibadilike, ipewe meno na iweze kupambana vilivyo na tatizo hili ambalo limekuwa likiwakwamisha wasanii wengi.
2. Kunakiri (copying) kazi za wasanii wa Nigeria na kutumia muziki (Sound Tracks) za wasanii wa muziki bila idhini yao.Katika haya wasanii wa Filamu wameshauriwa kuwa makini kwani sheria ya Hakimiliki inaweza kuwafunga.Kwa ujumla wasanii walishauriwa kuwekeza ubunifu binafsi na kubeba uhalisia wa sanaa yetu badala ya ilivyo sasa ambapo filamu zetu zimekuwa zikifanana fanana na zile za Nigeria.
3. Uchafu wa Filamu-Wadau wengi wamesema kwamba, filamu za kibongo zimekuwa na maadili mabovu yanayotokana uvaazi wa vichupi kwa wasanii wa kike, uoneshaji wa matendo ya faragha (mapenzi) mara kwa mara, script zenye kushabikia matendo maovu na yasiyofaa kwa jamii nk.Wadau walishauri Bodi ya Filamu, vituo vya TV na wasanii wenyewe kuhakikisha wanadhibiti filamu zisizo na maadili kwani zimekuwa zikitia aibu/kichefuchefu.Ilielezwa kwamba, baadhi ya filamu hazibebi uhusika wenye ufanano na maisha/maadili ya kitanzania.
4. Wasanii kuact maisha ya juu mara kwa mara tofauti na uhalisia wao.Mtaalamu wa Filamu kutoka Chuo Kikuu,Bw.Ndunguru alieleza kwamba,filamu nzuri ni ile inayobeba uhalisia.Aliongeza kwamba, wasanii wanapenda kutumia magari ya gharama kama Hammer, majumba ya thamani, maisha ya anasa nk. kwenye filamu zao kueleza uhalisia usiokuwepo katika maisha yetu.
5. Ubunifu mdogo wa waongozaji, watengenezaji na mameneja wa Filamu ambao umekuwa ukiwafanya muda mwingi wautumie kunakiri (copying) kazi za kigeni.Ilishauriwa kwamba, wataalamu hawa wafikirie walau kupata elimu,semina na mafunzo ya muda mfupi kwenye taaluma zao badala ya ilivyo sasa.
6. Kutokuzingatia mikataba kwenye kazi zao.Ilielezwa kwamba, wasanii wengi wamekuwa wakiwalalamikia wasambazaji wa kazi (Distributors) huku wakiwa wamesainiana mikataba.Kumbe tatizo lililopo ni wasanii wenyewe kusaini mikataba kwa pupa, uroho wa fedha, bila kuisoma mikataba husika na wakati mwingine bila kuandikiana bali kwa mazungumzo tu.Ilishauriwa kwamba, wasanii lazima wasimamie mikataba na kuhakikisha inawanufaisha.Wasilalame tu, wachukue hatua pia.
Picha/Habari na Afisa Habari wa BASATA,Alistide Kwizela
Mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya CCM,Dk. Bilal akizungumza na wanachi wa Wilaya ya Nanyumbu baada ya kuingia mpakani mwa wilaya hiyo na Masasi leo.
Kamanda wa Chipukizi wa Wilaya ya Masasi, Fatuma Rajab akimvisha skafu Mgombea Mwenza Dk. Mohamed Gharib Bilal alipokuwa akiingia mpakani mwa Wilaya ya Masasi akitokea Wilaya ya Newala leo mchana.
Mgobea Mwenza wa urais, Dk. Mohamed Gharib Bilal akisalimiana na wananchi na viongozi wa Chama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Masasi, baada ya kuingia mpakani mwa wilaya hiyo na Newala, leo.Picha kwa hisani ya Muhidin Sufian.
Mwenyekiti wa CUF na mgombea urais wa chama hicho cha wananchi Profesa Ibrahim Lipumba akisalimia wanachama wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni katika viwanja vya Kidongo Chekundu jijini Dar.
Profesa Lipumba akisalimiana na Mh. Hamad mmoja wa wanachama na viongozi waandamizi wa CUF.
Sehemu ya umati wa wana CUF waliofika kwenye mkutanoni chama hicho kwenye viwanja vya Kidongo Chekundu jijini Dar.Picha na Tiganya Vincent-MAELEZO-Dar es salaam

Mgombea wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM,Mh Jakaya Kikwete amefanya mkutano wa kampeni jana na kuhutubia katika uwanja wa Mandele mjini Sumbawanga,amb wakazi wa Sumbawanga walijitokeza kwa wingi kutoka vitongoji mbalimbali vya mji huo. Pichani Mh Jakaya Kikwete akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia chama cha CCM Bw. Hayeshi ambaye kama atashinda kuomngoza jimbo hilo atakuwa anachukua nafasi ya aliyekuwa mbunge wa Sumbawanga mjini Mzee Paul Kimiti aliyeng'atuka madarakani mara baada ya kulitumikia jimbo hilo kwa muda mrefu.
Mgombea Urais kwa chama cha CCM,Mh Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi mara baada ya kuwasili mjini mpanda na kufanya mkutano wa kampeni mjini humo jana.
Mgombea Urais kwa tiketi ya chama cha CCM,Mh Jakaya Kikwete akishuka kwenye Helkopta mara baada ya kuwasili Sumbawanga mjini tayari kwa mkutano uliofanyika jana kwenye uwanja wa Mandele mjini humo.
Wananchi wa mjini Sumbawanga wakimsubiri mgombea Urais kwa tiketi ya chama cha CCM,Mh Jakaya Kikwete kuwasili uwanjani hapo tayari kwa kuanza mkutano.