shoo love ndani ya Str8Muzik Festival ilivyokuwa

Monday, November 30, 2009
Wadadazz wakigombea taulo alilokuwa akilitumia D banj alipokuwa jukwaani,mara baada ya kumaliza shoo akalitupa kwa mashabiki wake wakiwemo hawa walimbwende ambao walibahatika kulidaka kwa raha zao,tatizo walikuwa watatu sijui nani alikubali kumuachia mwenzake,kaaazi kweeli kweli.!
Wazee wa GENGE,shoto ni Nonini na Juacali wakiwa wamepozi mwishoni mwa wikend kwenye tamasha la Str8Muzik Festival;Intercollege special 2009,kabla ya kukamua jukwaani.
Mkali wa Crank bongo Cpwaa akiwa amepozi na Juacali
"Ebwanaee mzee wa genge unajua nini inabidi tutoe singo moja matata sana,au unasemaje ?"Prof Jay anaonekana akimwambia maneno hayo mkali mwenzake wa kufloo Juacali.
Marlow naye alipata ladha ya kupozi na msanii wa kihip hop toka kwa watani wetu wa jadi,aitwaye kwa jina la kisaniii Juacali.
Wote wakali katika anga ya muziki wa kufoka foka,shoto ni msanii wa hip hop kutoka Kenya ambao wao wanauita 'Genge',Nonini akiitazama kwa makini Cd ya albamu mpya ya muziki wa hip hop hapa bongo a.k.a bongofleva Albert Mangwea iitwayo Nn'ge.Ni bonge ya albamu ambayo kiukweli imeandaliwa vyema kabisa,iko sokoni kwa sasa,inasambazwa na Zizzou Entertainment.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 30, 2009 | | Permalink | Maoni 0

nonini na ujumbe wake kwa wabongo


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 30, 2009 | | Permalink | Maoni 0

shindano la uniq modo lazidi kupamba moto





Mwandaaji mkuu wa shindano la Uniq Modo,Taji Liundi wa pili kushoto akifafanua jambo mbele ya majaji wa shindano hilo.
Baadhi ya washiriki wa shindano la Uniq Modo wakiwa wamepozi katika picha ya pamoja

Baadhi ya washiriki wa shindano la Uniq Modo wakikatiza ufukweni,Cine Club walipokuwa wakifanyiwa usahili wa kushiriki


Shindano la Uniq Modo mwishoni mwa wiki lilifanya usaili na kuwapata washiriki wake 12 kesho,ambao majaji walikuwa ni Kanumba, Sylvia na Kemmi,waliokutana ana kwa ana na mamodo 40.

Baada ya kuwachuja kwa kuangalia picha zao wiki mbili zilizopita, sasa watawaona moja kwa moja na kuamua 12 watakaoingia kwenye fainali.

Hao 12 watapigwa picha maalumu ambazo zitaonekana kwenye blog hii (http://modotz.blogspot.com/) nawe utapata fursa ya kuwa jaji pia.

Zawadi ni Tsh 2.5 milioni ambayo inatolewa kwa ufadhili wa SHEAR ILLUSIONS!!

Maduka bora ya mavazi ya TRUWORTHS nayo yatadhamini hao mamodo 12 nguo kwa ajili ya onyesho maalumu la mwisho siku ya kumtangaza mshindi.

Usaili huo umefanyika mwishoni mwa wiki kwenye fukwe za CINE CLUB, jijini Dar.

Blog ya Umodo inakaribisha wadau mbalimbali kama madizaina wapya, wadhamini kujiunga nasi katika kipindi hiki. Wasiliana na Taji kwenye +255 655 888 799.
Tafadhali piga kama upo serious tu! Hii kazi inahitaji umakini sana, nisingependa kuwapotezea wasichana washiriki, wadhamini wangu na mimi mwenyewe na hata wewe muda wako.
Ahsante!
Taji
"Shindano la Uniq Modo limeandaliwa kwa ushirikiano wa Gazeti la Ok! "Kila Wiki" na blog ya Umodo".
Kwa habari zaidi za shindano hili bofya HAPA

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 30, 2009 | | Permalink | Maoni 1

Invitation for Tanzania's Independence day


 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 30, 2009 | | Permalink | Maoni 0

mzee wa njia panda sebastian ndege alivyoinyakuwa nondo yake pale ifm

Mkurugenzi wa Ndege Insurance, Sebastian Ndege, na Mkewe, Wakiinua juu Glass katika kuwakaribisha, wageni waalikwa kwenye Sherehe za Kumpongeza, mara baada ya kunyakua nondo yake ya Post Graduate Diploma in Insurance & Risk Management, na kupata tuzo ya Overall Best Student, katika chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Mahafali yalifanyika kwenye Viwanja vya Karimjee na kufuatiwa na sherehe ambayo ilifanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Pick Cock Mellenium Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi wa Ndege Insurance,sebastian Ndege(kushoto), akiwa na Rafiki yake, Kinje, wakati wa sherehe za kumpongeza, katika sherehe fupi iliofanyika kwenye ukumbi wa hotel ya Mellenium Pick Cock, ambayo iliwajumuisha wafanyakazi wa Ndege Insurance, ndugu,jamaa na Marafiki.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Laurence Masha,(kushoto) akifurahia jambo wakati wa kumpongeza Mkurugenzi wa Ndege Insurance, Sebastian Ndege, baada ya kuhitimu mafunzo ya Post Graduate Diploma in Insurance & Risk Management, na kupata tuzo ya Overall Best Student, katika mahafali ya chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), katika sherehe iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Hotel ya Mellenium Pick Cock-Dar es Salaam.
Baadhi ya Wageni Waalikwa katika Sherehe ya Kumpongeza Mkurugenzi wa Ndege Insurance, Sebastian Ndege, wakijichana vilivyo kwenye sherehe fupi ya kumpongeza mara baada ya kunyakua nondo yake katika chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM).

Mkurugenzi wa Ndege Insurance, Sebastiani Ndege na Mkewe, wakikata Keki

Mkurugenzi wa Ndege Insurance, Sebastian Ndege, akifafanua jambo wakati wa Sherehe ya Kumpongeza kutokana na kupata Tuzo ya Mwanafunzi Bora(Best Student Overall ya Post Graduate Diploma in Insurance & Risk Management ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha(IFM), sherehe hizo zilifanyika katika viwanja vya Karimjee Dar es Salaam,kushoto ni Mkewe mama Sebastian Ndege.
Duh, hawa ni baadhi ya Wapiga Picha, na Waandishi wa Habari, wakifuatilia kwa makini matukio ya Mahafali ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), kwenye Viwanja vya Karimjee Dar es Salaam yaliyofanyika mwishoni mwa wiki

Mkurugenzi wa Ndege Insurance, Sebastian Ndege, akipongezwa na Mkewe, muda mfupi baada ya kupokea tuzo ya Mwanafunzi Bora,(Best Student ya Overall Best Student, ya Post Graduate ya Diploma in Insurance & Risk Management katika maahafali yaliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee Dar es Salaam .

Waziri wa Fedha Mstafa Mkulo, akimkabidhi Mhitimu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha, Sebastian Ndege, Tuzo ya Best Student Overall Best Student ya Post Graduate Diploma in Insurance & Risk Managament katika Mahafali yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Ndege Insurance Sebastian Ndege(kushoto), wakati wa wa mahafali ya kuhitimu Shahada ya Diploma(Post Graduate Diploma in Insurance & Risk Managament, ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), iliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 30, 2009 | | Permalink | Maoni 3

washiriki wa miss east africa 2009 kuanza kuwasili wiki hii

Rebecca Getachew (23) ETHIOPIA
Dalysha Nirena Doorga (21) MAURITIUS
Nediat (21) ETHIOPIA
Tabitha (20) KENYA

Fatma Abdulahi (20) SOMALIA
Queen Belle Monique (23) BURUNDI

Asli Osman Mahamud (18).
Warembo wanaoshiriki katika mashindano ya kimataifa ya urembo ya Miss East Africa 2009 wataanza kuwasili Nchini kuanzia wiki hii tayari kwa mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika tarehe 18 mwezi wa 12 katika ukumbi wa mlimani city jijini Dar es salaam.
Aidha, warembo watakaoiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo wanatarajiwa kutangazwa kesho kutwa baada ya kamati maalumu iliyopewa jukumu la kuratibu zoezi hilo kukamilisha kazi yake.
Mashindano ya Miss East Africa mwaka huu yanatarajiwa kuwa na mvuto wa aina yake kutokana na Nchi zinazoshiriki mashindano hayo kuchagua warembo wenye viwango vya hali ya juu ili kuziwakilisha katika mashindano ya mwaka huuMiss East Africa 2009 itashirikisha warembo kutoka katika Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Eritrea, Somalia, Djibouti, na Mauritius ambazo zote zimeshathibitisha ushiriki wao.
Mashindano hayo makubwa ya urembo kwa ukanda huu wa Africa yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Limited ya jijini Dar es salaam.Miongoni mwa makampuni yanayodhamini mashindano hayo kwa mwaka huu ni pamoja na Kunduchi Beach Hotel & Resort, EATV, Kings & Queens Worldwide, CMC Automobiles Limited na AKO Catering Services Ltd.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 30, 2009 | | Permalink | Maoni 0

SCHOLARSHIPS FOR AFRICAN COUNTRIES


University of Oslo, Norway - The International Summer School 2010 (June 26 - August 6)

http://makulilo.blogspot.com/2009/11/erasmus-mundus-msc-in-photonics-belgium.html
China Scholarships for International Graduate Students 2010

http://makulilo.blogspot.com/2009/11/china-scholarships-for-international.html
MSc Scholarships in African Studies, Oxford University

http://makulilo.blogspot.com/2009/11/msc-scholarships-in-african-studies.html
Hamburg International Graduate School for the Study of Regional Powers, GERMANY

http://makulilo.blogspot.com/2009/11/hamburg-international-graduate-school.html
Master of Agricultural development and management of natural resources

http://makulilo.blogspot.com/2009/11/ma-programme-euroculture.html
Master's course: Applied Ethics, Erasmus Mundus
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 30, 2009 | | Permalink | Maoni 0

SERENGETI BREWERIES LIMITED YADHAMINI KOMBE LA NYAMAGANA KWA SH. MILLIONI 10.


Jezi zilitolewa kwa waandaji kwa ajili ya maandalizi




Mkuu wa Masoko na Utekelezaji Bahati Singh akiwa amemkabidhi Diwani viti maalum Tatu
Mkuu wa Masoko na Utekelezaji Bahati Singh akimkabidhi jezi Diwani Biku wa Nyamagana.
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya bia ya Serengeti wakiwa wamepozi kwa pamoja,hivi karibuni jijini Mwanza.

======= ======== ======== ========== ======
SERENGETI BREWERIES LIMITED YADHAMINI KOMBE LA NYAMAGANA KWA SH. MILLIONI 10.
Kampuni ya bia ya Serengeti leo imekabidhi hundi ya shilingi milioni 10 kwa waandaaji wa kombe la nyamagana la mpira wa miguu.

Ndugu Bahati Singh Mkuu wa Masoko na Utekelezaji alikabidhi hundi ya Shilingi milioni kumi pamoja na vifaa vya michezo vikiwemo jezi, vikombe na medali katika hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika nyumbani hotel jijini Mwanza, Makabidhiano hayo ambayo yalihudhuriwa na Meneja mauzo wa kanda ya ziwa Bwana Avinash Maggirwar na Meneja Masoko kanda ya ziwa Bwana Yohana Manoli.

Akizungumza katika hafla hiyo Bwana Bahati Singh alisema’ NI heshima tele tena SBL kudhamini mashindano haya katika jiji la Mwanza kwa kuwa tuna kiwanda chetu na malengo makubwa ya SBL ni kukuza kiwango cha mpira wa miguu Nchini na pia katika mikoa ambayo tunaihudumia kijamii.

Mchango wetu wa leo ni kupitia zao la Premium Serengeti Lager tunaleta mahusiano mazuri na wanachi wa nyamagana na kuwaleta pamoja kwa njia ya mpira wa miguu na kuleta Amani, Urafiki, UPendo na Umoja kwa watu wa Mwanza.
Pamoja twaweza sema Asante kwa jamii ya watu wa Mwanza kwa kuunga mkono SBL na hii ni asilimia na kusema asante tena watu wa Mwanza.


Imesainiwa na:

Teddy Mapunda
MENEJA MKUU MAHUSIANO JAMII NA MAWASILIANO
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Monday, November 30, 2009 | | Permalink | Maoni 0

mie na mzee wa genge

Sunday, November 29, 2009
Mie nikiwa nimepozi kwa ajili ya picha na msanii wa muziki wa Genge ambaye kiuweki huwa namzimia sana kwa mashairi yake na pia anavyokamua jukwaani,jamaa anatoeka kenya naiatwa Juacali ,hii ilikuwa usiku wa kuamkia leo kwenye tamasha la Str8Muzik Festival;Intercollege special 2009,lililofanyika katika viwanja vya Tanganyika Packers,Kawe jijini Dar
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, November 29, 2009 | | Permalink | Maoni 0

dbanj achizika na kuchizisha mashabiki tamasha la Str8Muzik Festival;Intercollege special 2009


Kutoka kushoto ni Dr Sid Dr. Sid kutoka Mo Hits Records ya Nigeria,Rapa mahiri aliyeambatana naye D banj aitwaye Ikechukwau wakilishambulia jukwaa kwa pamoja
Nyomi la nguvu halafu liko live ile mbaya
D banj akiimba wimbo wake wa Fall in love mbele ya umati wa watu usiku wa kuamkia leo katika tamasha la Str8Muzik Festival;Intercollege special 2009,lililoandaliwa na kampuni ya sigara Tanzania TCC kupitia chapa yake ya muziki iitwayo Str8Muzik .
Ilikuwa shuhuli kweli kweli.
D banj akiwa amebebwa juu na mwanausalama wake huku akiwapungia na kuimba pamoja na mashabiki wake wimbo wa Fall in lone.
nani kakwambia muziki ni kuimba tu ohooooo.!Si unamuona D banj pichani
D banj alichenguka kwa namna ya kipekee mara baada washabiki wake wamechizika mbaya na songi lake la Fall in love ambalo limebamba ile mbaya hapa bongo.





D banj kulia akikamua na Dr. Sid kutoka Mo Hits Records pia toka Nigeria,palikuwa hapatoshi .


Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye amuwa ngumzo kila akitoka na singo yake,allibuka na bembeleza ikafanya vizuri,akaibuka na singo nyingine iitwayo pipii nayo ikampandisha chati na sasa anatamba na singo yake nyingine iitwayo Bidii na aliikamua usiku wa kuamkia leo katika tamasha la Str8Muzik Festival;Intercollege special 2009 na kufanya vyema kabisa.
Watu walikuwa kibao waliokwenda kujiachia tamasha la Str8Muzik Festival;Intercollege special 2009.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Sunday, November 29, 2009 | | Permalink | Maoni 0
Idadi ya watu