kila la kheri na maisha marefu
Tuesday, March 31, 2009




Other Products at House of Glamour
40ft x 100ft Marquee - Green and Gold deco
40ft x 100ft Marquee - Red deco outside
Clear Span Marquee at Bongo Fiesta 1
Clear Span Marquee at Bongo Fiesta


Ebwanaaae.! Pichani nilikutana na wadau kutoka chuo Mzumbe,kulia ni Rehema,Mdau wa kutoka Dar Cathbert Kajuna,Irene ,Mie,Amina pamoja na swaiba.Haya Wikiend ijayo tukutane ndani ya Moro halafu tuone wadau au sio.PAMOKO
Dj wa Clouds FM Mully B aliyekuwa akikamua mbaya kwenye mashine akiwa amepozi na kichwa kingine mahiri katika safu ya utangazaji ya wana wa Clouds B 12 wakishangaa mmoja wa washabiki alipopandisha mzuka wa kucheza kiaina
Wasanii wa kizazi kipya kutoka mjini Mbeya waitwao Isanga Family wakiwa jukwaani na mabegi yao kama wasafiri halafu wamekosa nauli,lakini wamejiandaa kwa safari
Mdau kutoka kijiji cha Isanga mbeya nae hakutaka kuyamis matukio ya shangwe ndani ya Dhandoo,alirekodi taratiiiibu
Prof Jay akicheza na moja ya shabiki wake jukwaani kupitia wimbo wake uliowahi kutamba sana hapa bongo uitwao Zali la Menatal
Prof Jay akiwarusha wakazi wa Mbeya vilivyo,na pasi hiyana walijiachia ile mbaya
Prof Jay akiwauliza wakazi wa Mbeya waliofika kwenye uzinduzi wa Albamu ya Shangwe ndani ya Dhando wanataka nini
Watu walikuwa kibao ndani ya Dhando hall,kwa aliyekosa shangwe za uhakika shauri yake
Dj Choka akifanya vitu vyake kwenye mashine kabla ya Prof Jay hajapanda jukwaani
Moja ya wasanii mahiri katika makamuzi ya hip hop hapa bongo,Mangwea akiwarusha wakazi wa Mbeya hivi karibuni
Kulikwepo na shangwe za kila aina Jukwaaani kama uonavyo pichani mdau
Nature akiimba moja ya wimbo mpya uliopo kwenye albamu yake ya Tugawane umasiki ambayo iko sokoni kwa sasa, uitwao Afrika nambari one
Agghaa, aaghaaaa, aghaaa..Waali Naziii!!Juma Nature akiangusha moja moja kwa staili ya kipekee kabisa,Nature aliwakonga vilivyo wakazi wa Mbeya
Rich One na Juma Nature wakishambulia jukwaa kwa vina mbele ya umati mkubwa uliofika kushuhudia uzinduzi huo wa aina yake mjini mbeya
Kundi Wanaume Halisi TMK likiongozwa na Juma Nature aliyezindua albamu yake ya tugawane umasikini hivi karibuni, wakijiachia vilivyo jukwaani mbele ya washabiki wao ambao walionekana kuvutiwa mno na staili mpya ya Wanaume Halisi.Pichani kulia ni Dollo na Juma Nature akijiduarisha na moja ya wimbo wao uliopo kwenye mahadhi ya mchiriku
Feroouz na akimdis Mr Policeman mbele ya wakazi wa Mbeya waliofurika ndani ya ukumbi wa Dhando mwishoni mwa wiki
Ilifika zamu ya Mr Policeman a.k.a Ferooz (shoto) akiimba pamoja na mtu mzima Pro Jay wimbo wao wa Starehe ambao ulikubalika kwa kiasi kikubwa ndani ya washabiki wa muziki wa bongofleva,kati ni Kiboya kutoka kundi la Wanaume Halisi alikiwapa tafu
Ilikuwa ni shangwe tu kwa wakazi wa Mbeya
Matonya akiwa amenaswa kwa ukaribu kabisa na kamera ya jiachie
Matonya akiimba kwa hisia wimbo wake wa Anita mbele ya wakazi wa Mbeya
Eehbwana.! Vichwa vyote kutoka Tanga hivi ambayo vinafanya vyema katika muziki wa kizazi kipya,Kasim pamoja na Matonya wakiimba kwa pamoja hali ambayo iliwavutia mno wakazi wa mbeya,hasa kwa mpangilio wa sauti zao zilizojaa hisia kali za kumbembeleza
Kasim akiimba kwa makini moja ya wimbo wake wa AWENA mbele ya washabiki wake mjini Mbeya
Wakazi wa Mbeya wakishangweka ile mbaya
Mwishoni mwa wikend Ziara ya uzinduzi wa Shangwe albam inayodhaminiwa na kampuni ya sigara ya TCC kupitia kitengo chao Str8 Muzik,ilikuwa mjini Mbeya ndani ya ukumbi wa Dhando na kuhudhuriwa na wakazi kibao wa mjini humo.Pichani ni msanii wa kizazi kipya ajulikanae kwa jina la kisanii PNC akifanya mambo jukwaani
Kamera ya Jiachie ilifika pia chuo cha ualimu tukuyu kilichopo Bulyaga..Tukuyu mjini
Pichani ni wafanyabiashra wakiendelea na biashara zao za kila siku katika soko la Madaraka lililopo Tukuyu mjini
Pichani kama uonavyo hilo jengo lilikuwa ni moja ya duka kubwa la jumla na maarufu sana mjini tukuyu,lilikuwa linamilikiwa na mhindi mmoja aliyejulikana sana kwa jina la Kaka,na ndiye aliyekuwa anaimiliki timu ya Tukuyu Stars a.k.a Banyambala.Kwa habari nilizozipata ni kwamba mhindi huyo alifariki kitambo na kupelekea duka hilo kufa kabisa na hata timu hiyo na yenyewe kushuka kabisa
Hapa tayari tuko ndani ya jiji la Mbeya,ilikuwa jioni flani hivi