JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TAWI LA CHUO KIKUU CHA MISRI KUANZISHWA TANZANIA- WAZIRI MKENDA

Share This

 

Na Mathias Canal, WEST-Dodoma
CHUO Kikuu cha Misri kimebainisha kusudio la kuanzisha tawi lake nchini Tanzania kwa ajili ya kuanza kutoa elimu katika fani mbalimbali.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ameeleza hayo Leo tarehe 16 Agosti 2022 wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Misri nchini Tanzania Mhe Mohamed Gaber Abulwafa katika ukumbi wa mikutano wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jijini Dodoma.

Waziri Mkenda amemueleza Balozi huyo kuwa serikali ya Tanzania imetoa fursa ya wawekezaji kuja nchini kufuata taratibu za kisheria na kuwekeza haraka iwezekanavyo.

Amemualeza Balozi huyo kuwa wakati taratibu zingine zinaendelea za uwekezaji huo, Chuo kikuu hicho kinaweza kuunda ushirika na Chuo Kikuu chochote kilichopo nchini ili kuanza kutoa elimu kusudiwa kwa haraka.

Waziri Mkenda amemuelekeza Mkurugenzi anayeshughulikia Vyuo Vikuu katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt Kenedy Hosea kuhakikisha anaanza mazungumzo na vyuo vikuu nchini ili kuona ni chuo gani kipo tayari kuanza ushirikiano huo ili utekelezaji uanze.

Kwa upande wake Balozi wa Misri nchini Tanzania Mhe Mohamed Gaber Abulwafa amemuhakikishia Waziri Mkenda kuwa nchi yake itaendeleza ushirikiano na Tanzania katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya elimu.

Katika mazungumzo hayo wamejadiliana pia namna ya kuanza utekelezaji wa haraka wa (MOU) zilizosainiwa wakati wa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoifanya nchini Misri.

Pia Balozi Abulwafa amewasilisha mualiko wa Waziri wa Nishati wa Misri kumualika katika mkutano utakaokuwa unajadili masuala ya Atomiki pamoja na mwaliko wa Waziri wa elimu wa Misri ili kujadili kwa kina umuhimu wa kuimarisha ushirikiano katika sekta ya elimu.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad