JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


WHC WAFUNGUA DIRISHA JIPYA LITAKALOWEZESHA WATUMISHI WA SEKTA BINAFSI KUWEZA KUNUNUA NYUMBA.

Share This
Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mauzo wa Watumishi Housing Company (WHC), Raphael Mwabuponde akifafanua jambo wakati wa kufungua dirisha jipya  litakalowezesha watumishi wa sekta binafsi  kuweza kununua nyumba zake kwa garama nafuu na kuwainua kiuchumi. katikati ni
Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Company (WHC),  Dkt. Fred Msemwa na kulia ni Afisa Uhusiano na mauzo wa Watumishi Housing Company (WHC),  Maryjene Makawia.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Company (WHC),  Dkt. Fred Msemwa (Katikati)akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kufungua dirisha jipya  litakalowezesha watumishi wa sekta binafsi  kuweza kununua nyumba zake kwa garama nafuu na kuwainua kiuchumi. Kushoto  ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mauzo wa Watumishi Housing Company (WHC), Raphael Mwabuponde na Kulia ni Afisa Uhusiano na mauzo wa Watumishi Housing Company (WHC),  Maryjene Makawia.
kulia ni  Afisa Uhusiano na mauzo wa Watumishi Housing Company (WHC),  Maryjene Makawia akizungumza na waandishi wa ahabari jijini Dar es Salaam leo. kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Company (WHC),  Dkt. Fred Msemwa.

Kulia ni Afisa Mauzo wa Watumishi Housing Company (WHC), Irene Kasanda akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mauzo wa Watumishi Housing Company (WHC), Raphael Mwabuponde, Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Company (WHC),  Dkt. Fred Msemw na Afisa Uhusiano na mauzo wa Watumishi Housing Company (WHC),  Maryjene Makawia.
Picha na Avila Kakingo, Blog ya Jamii.
 
Na Karama Kenyunko blogu ya jamii.
WATUMISHI Housing Company (WHC),  wamefungua dirisha jipya  litakalowezesha watumishi wa sekta binafsi  kuweza kununua nyumba zake kwa garama nafuu na kuwainua kiuchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa WHC,  Dkt. Fred Msemwa, amesema, dirisha hilo ambalo litajumuisha Watumishi wote wale wa umma na wa binafsi, litawawezesha wafanyakazi wote kuwa na makazi bora kupitia umiliki wa nyumba kwani nyumba hizo wanaweza kuzitumia kwa kukopa kuanzisha miradi mbali mbali ya uchumi.

Amesema Watumishi hao wa sekta binafsi ambao nao wanapata fursa ya kununua nyumba hizo ni wale ambao hawako katika utumishi wa umma lakini wanachangia katika mifuko ya pensheni.

Ameongeza kuwa, wigo huo mdogo unatokana na mahitaji ya wengi kwani watu wengi ukitoa Watumishi wa umma ambao hapo awali ndio walikuwa na sifa ya kununua nyumba hizo,wanashida ya makazi bora na ya kisasa

"Kufuatia uamuzi huu, WHC sasa itakuwa ikiwahudumia Watumishi wa umma pamoja na wafanyakazi wengine walioko katika sekta binafsi ikiwa ni muendelezo wa juhudi za Serikali na mifuko ya hifadhi ya jamii katika kuwawezesha wafanyakazi wote kuwa na makazi bora na kuwainua kiuchumi kupitia umiliki wa nyumba", amesema Dkt Msemwa.

Naye Mkuu wa Kitengo cha mauzo na masoko wa WHC, Raphael Mwabuponde amewaalika watanzania wote wenye uhitaji wa nyumba hizo, kutuma maombi kwa kuchukua fomu katika tovuti ya WWW.whctz.org.
Ameongeza mpaka sasa bado kuna nyumba za kuuza zilizopo Bunji B, Gezaulole Kigamboni, Mkundi Morogoro, Mwanza Kisesa na Njedengwa Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad