JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MASAUNI AFANYA MKUTANO NA ASKARI WA USALAMA BARABARANI NA MADEREVA BODABODA.

Share This
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akimuuliza maswali Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa, wakati alipotembelea Ujenzi wa Kituo cha Polisi Mjimwema, Wilayani Kigamboni   kukagua maendeleo ya ujenzi huo. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke, Gilles Muroto na anayefuatia ni Mkuu wa Utawala Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Benadict   Kitalika.
 Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa, akimuonyesha eneo linapotakiwa kujengwa kituo cha Polisi Kibada, Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, wakati wa ziara ya naibu waziri,wilayani Kigamboni, Dar es  Salaam.
 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akikagua moja ya chumba cha mahabusu ndani ya kituo cha Polisi Mwasonga, wakati wa ziara ya ukaguzi wa vituo vya polisi wilayani Kigamboni, jijini Dar es Salaam.Katikati ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Hashim Mgandilwa.
 Muonekano wa nje wa Kituo cha Polisi cha Mwasonga kilichopo wilayani Kisarawe, kikiwa katika hatua za mwisho kabla ya ujenzi wake kukamilika.
 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na madereva bodaboda wakati wa ziara ya kikazi wilayani Kigamboni   ambapo aliwaasa madereva hao kufuata sheria za usalama barabarani pindi wafanyapo shughuli zao ili kuepuka ajali.
 Muendesha Bodaboda wa Wilaya ya Kigamboni, Said Athumani, akimuuliza maswali   Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani), wakati wa Mkutano ulioitishwa na naibu waziri huyo wakati wa ziara ya kikazi wilayani humo.
Muendesha Bodaboda wa Wilaya ya Kigamboni, Fredrick Swai, akimuuliza swali   Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani), wakati wa Mkutano ulioitishwa na naibu waziri huyo wakati wa ziara ya kikazi wilayani humo. 
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad