SHIRIKA la Ndege la Etihad lenye makao makuu yake Nchi za
Falme za Kiarabu limeendelea kujihimarisha barani Afrika kupitia ushirikianao
mpya wa kibiashara walioingia na Kulula, washindi wa tuzo ya ndege ya gharama
nafuu nchini Afrika Kusini.
Ushirikiano huo wa biashara utawawezesha wateja wa
Shirika la Ndege la Etihad kufika miji mbalimbali ndani ya Afrika Kusini
ikiwamo miji ya Cape Town, Durban, George na East London via Johannesburg.
Shirika la Ndege la Etihad litaweka namba yake ya EY kwenye
ratiba za ndege za Kulula kati ya Johannesburg na miji mingine mikubwa maarufu.
Makubaliano hayo yanamwezesha mteja kupatiwa huduma zote anapoanza safari na
anakofikia.
Huduma hiyo mpya itaanza kuuzwa kuanzia Octoba 3, 2016
kwa kuanza na safari kutoka maeneo ya Kaskazini kwa ratiba ya tarehe 30 Octoba
mwaka huu.
Makubaliano hayo baina ya Shirika la Ndege la Etihad
na Kulula ni mwendelezo wa juhudi za shirika hilo kutokana na dhamira yake ya kuongeza
idadi ya safari za ndege zake zinazotoa huduma kwenye bara hili kwenye maeneo
23 kupitia ushirikiano uliopo kupitia Shirika la Kenya Airways, Royal Air Maroc na
mpango wa ushirikiano ulipo kwenye Shirika la Air
Seychelles.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege la Etihad, Peter
Baumgarter alisema, “Shirika la Ndege la Kulula limekuwa na ubunifu wa hali ya
juu na mshindi wa tuzo ya usafiri wa anga hivyo makubaliano haya ya kibiashara
kwenye sekta ya anga yanadhihirisha juhudi za Shirika la Ndege la Etihad katika
kupanua shughuli zake za kibiashara barani Afrika. Kupitia mkataba huu Kulula
itawapa huduma wateja wetu wanaotoka Johannesburg kupitia safari nne
zilizoanzishwa katika ukanda huo. Ni matumaini yangu ushirikiano huu
ulioanzishwa utaleta manufaa kwa wasafiri wa daraja la biashara na wale wa
starehe kwa usawa.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya mama Comair ya Kulula,
Erik Vanter alisema,
“Tunajivunia kushirikiana na Shirika la ndege la
etihad kuwa miongoni wa washirika wetu kwenye huduma za usafiri wa anga na kuwa
chachu kwenye kuongeza fursa za ushirikiano. Tunawakaribisha wateja wa Shirika
la Ndege la Etihad kwa moyo mkunjufu kwenye jumuiya yetu ya usafirishaji.
Kwa barani Afrika Shirika hilo la ndege la Etihad linatoa huduma zake
kwenye miji 10 barani afrika ambayo ni Johannesburg, Nairobi, Entebbe, Dar es
Salaam, Khartoum, Casablanca, Rabat, Lagos, Cairo na Mahé visiwa vya Seychelles.
No comments:
Post a Comment