TIMU
ya soka ‘Team Ismail’ imefanikiwa kuwagaragaza wapinzani wao wa jadi
'Team Dizo Moja' kwa kipigo cha mabao 4-1, katika tamasha la Kandanda
day, lililofanyika Jumamosi katika Viwanja vya Jakaya M Kikwete Youth
Park.
Kipigo hicho kwa 'Team Dizo', ni mfululizo wa matokeo
mazuri ya Team Ismail,ambayo mwaka huu imeonekana kulipiza kisasi cha
kuchapwa idadi hiyo ya mabao kama walivyofanya Team Dizo katika msimu wa
mwaka 2014.
Mabao ya Team Ismail,yaliwekwa kimiani na Freddy
Pastor aliyeweka kimiani mabao mawili,huku Gerald Bernald na Noah Katepa
wakifunga bao moja moja na lile la kufutia machozi kwa timu Dizo
likifungwa na mchezaji wao waliyemchukua kwa mkopo toka timu Ismail
Wilfred Kadege.
Mwaka jana katika tamasha hilo, Timu
Ismail,iliwatandika wapinzani wao kwa mabao 2 kwa mtungi,jambo ambalo
mwaka huu liliongeza upinzani mkubwa ndani na nje ya uwanja kutoka kwa
mashabiki wa timu hizo mbili.
Mbali na mtanange huo,mechi
nyingine iliyovuta hisia za mashabiki waliohudhuria tamasha hilo ni
mchezo wa fainali ya makundi ulizokutanisha timu za Dar City Fc na Coca
Cola,ambapo katika mchezo huo, Coca waliigaragaza Dar City kwa mabo 3
kwa bila.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamati,Patrick
Dumulinyi,aliwashukuru wadhamini wote pamoja na timu shiriki kwa
kufanikisha lengo la tamasha la mwaka huu lililobeba kauli mbiu ya Mpira
na Dawati kufana kwa kiasi kikubwa.
“Ningependa kuwashukuru
wadhamini wetu na timu shiriki,kwa kuungana kutimiza ndoto zetu za mwaka
huu za kuisaidia jamii kwa kukusanya fedha za madawati,ambayo kabla ya
kuisha kwa mwezi huu tunatarajia kuyakabidhi katika shule
husika,”alisema Dumulinyi.
Mshambuliaji wa 'Team Ismail', Nassor Bin Slum akijiandaa kuachia shuti kali kuelekea langoni mwa 'Team Dizo Moja', katika tamasha la wapenzi wa mchezo wa soka nchini 'Kandanda Day 2016', lililofanyika Jumamosi Oktoba 15, 2016 katika Viwanja vya Jakaya M Kikwete Youth Park, Jijini Dar es salaam.
No comments:
Post a Comment