JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


HIVI NDIVYO MAMBO YALIVYOKUA KATIKA TAMASHA LA KANDANDA

Share This
TIMU ya soka ‘Team Ismail’ imefanikiwa kuwagaragaza wapinzani wao wa jadi 'Team Dizo Moja' kwa kipigo cha mabao 4-1, katika tamasha la Kandanda day, lililofanyika Jumamosi katika Viwanja vya Jakaya M Kikwete Youth Park.


Kipigo hicho kwa 'Team Dizo', ni mfululizo wa matokeo mazuri ya Team Ismail,ambayo mwaka huu imeonekana kulipiza kisasi cha kuchapwa idadi hiyo ya mabao kama walivyofanya Team Dizo katika msimu wa mwaka 2014.

Mabao ya Team Ismail,yaliwekwa kimiani na Freddy Pastor aliyeweka kimiani mabao mawili,huku Gerald Bernald na Noah Katepa wakifunga bao moja moja na lile la kufutia machozi kwa timu Dizo likifungwa na mchezaji wao waliyemchukua kwa mkopo toka timu Ismail Wilfred Kadege.

Mwaka jana katika tamasha hilo, Timu Ismail,iliwatandika wapinzani wao kwa mabao 2 kwa mtungi,jambo ambalo mwaka huu liliongeza upinzani mkubwa ndani na nje ya uwanja kutoka kwa mashabiki wa timu hizo mbili.

Mbali na mtanange huo,mechi nyingine iliyovuta hisia za mashabiki waliohudhuria tamasha hilo ni mchezo wa fainali ya makundi ulizokutanisha timu za Dar City Fc na Coca Cola,ambapo katika mchezo huo, Coca waliigaragaza Dar City kwa mabo 3 kwa bila.


Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamati,Patrick Dumulinyi,aliwashukuru wadhamini wote pamoja na timu shiriki kwa kufanikisha lengo la tamasha la mwaka huu lililobeba kauli mbiu ya Mpira na Dawati kufana kwa kiasi kikubwa.

“Ningependa kuwashukuru wadhamini wetu na timu shiriki,kwa kuungana kutimiza ndoto zetu za mwaka huu za kuisaidia jamii kwa kukusanya fedha za madawati,ambayo kabla ya kuisha kwa mwezi huu tunatarajia kuyakabidhi katika shule husika,”alisema Dumulinyi.

Mshambuliaji wa 'Team Ismail', Nassor Bin Slum akijiandaa kuachia shuti kali kuelekea langoni mwa 'Team Dizo Moja', katika tamasha la wapenzi wa mchezo wa soka nchini 'Kandanda Day 2016', lililofanyika Jumamosi Oktoba 15, 2016 katika Viwanja vya Jakaya M Kikwete Youth Park, Jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad