JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


SONGAS FOOTBALL CLUB WAENDESHA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO JIJINI DAR.

Share This
Mechi mbalimbali zikiwa zinaendelea katika Bonanza hilo ambalo lilikuwa na lengo la kuhamasisha Michezo, usafi na Afya Bora.
Baadhi ya watu wadogo kwa wakubwa wakiendelea kufuatilia Bonanza hilo kwa makini 
MC Fadhili Nandonde akiendelea kutoa utaratibu wa Mechi mbalimbali zilizokuwa zikicheza katika Bonanza hilo.
Mgeni Rasmi katika Bonanza hilo Albert Kimaro ambaye ni Mkufunzi Mwandamizi Idara ya Michezo Chuo Kikuu cha Dar es salaam akikagua moja ya Timu hizo katika Bonanza hilo.
Mgeni Rasmi katika Bonanza hilo Albert Kimaro ambaye ni Mkufunzi Mwandamizi Idara ya Michezo Chuo Kikuu cha Dar es salaam akizungumza na watu waliofika katika bonanza hilo na kuwapongeza waandaaji kwa kuona umuhimu wa Mazoezi, usafi na Afya Bora pia amewasihi watu wawe na utaratiu wa kufanya Mazoezi.
Mwakilishi Kutoka Benki ya NMB ambao walikuwa ni moja ya wadhamini 
wa Bonanza hilo Frank Rwamugira akiwasihi watu kuwa na utaratibu wa kujiwekea akiba 
Watu mbalimbali wakiendelea kufuatilia Michezo hiyo , hata Boda boda nao walikuwa bize na Bonanza hilo.
Mbuzi huyu ndio ilikuwa zawadi ya Mshindi katika Bonanza hilo lililoandaliwa na Songas Football Club.
Rais wa Songas Football Club Ismail Sheha ambao ndio walioandaa Bonanza hilo akitoa neno la shukurani kwa wote ambao walihudhulia katika Bonanza na kusisitiza kuwa huo haukuwa mwisho wataendelea zaidi kuhamasisha Michezo, usafi na Afya Bora.
Watu mbalimbali wakiwa katika Banda la NMB kwa ajili ya kufungua akaunti ya Chapchap ambapo Mteja anaipata papo hapo na kupata maelezo ya huduma mbalimbali zinazotolewa na Benki hiyo.
Moja ya timu ikiwa imefungwa goli la kizembe huku goli kipa asijue cha kufanya na wachezaji wengine kukimbia kwa ajili ya kujipanga zaidi.
Mpira ukiendelea huku watu mbalimbali wakifuatilia Burudani hiyo kwa makini.

Picha na Fredy Njeje/Blogs za Mikoa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad