JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


WAZIRI MHONGO ATEMBELEWA NA BALOZI WA JAPAN NCHINI TANZANIA.

Share This
BBALOZI wa Japan nchini Tanzania, Masaharn Yoshida amemtembelea Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na kuzungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya nchi zao hususan katika sekta ya nishati.

Balozi Yoshida, aliyeambatana na Ujumbe wa baadhi ya maofisa kutoka Ubalozini na wataalam kadhaa kutoka Shirika la Japan Oil, Gas and Metals National Corporation (JOGMEC), alimtembelea Prof Muhongo Agosti 3 mwaka huu ofisini kwake, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa tatu kutoka kulia) akizungumza na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharn Yoshida (Kulia kwa Waziri) na Ujumbe wake, walipomtembelea Waziri ofisini kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni. 
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharn Yoshida (kushoto) na Mtaalam kutoka Shirika la Japan Oil, Gas and Metals National Corporation (JOGMEC) la nchini Japan, walipomtembelea Waziri hivi karibuni.
 Kutoka kushoto ni Bwana Hitoshi Suzuki (Ofisa kutoka Ubalozi wa Japan nchini Tanzania), Bibi Sakura Nishioka (Mtaalam kutoka Shirika la Japan Oil, Gas and Metals National Corporation (JOGMEC), Masaharn Yoshida (Balozi wa Japan nchini Tanzania), Profesa Sospeter Muhongo (Waziri wa Nishati na Madini), Bwana Yoshiaki Igarashi (JOGMEC), Bibi Ayumi Kosug (JOGMEC) na Tamiko Hirata (Ofisa kutoka Ubalozini). Balozi Yoshida na Ujumbe wake walimtembelea Waziri Muhongo ofisini kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad