JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


WASHINDI WA UWEKAJI WA AKIBA WA FNB WATANGAZWA LEO JIJINI DAR.

Share This
 Meneja Masoko wa First National Bank, Blandina Mwachang’a akiwapigia simu washindi wa droo ya kampeni inayoendeshwa na benki hiyo kuhamasisha uwekaji akiba ili kujikwamua kiuchumi ambapo washindi kumi walijipatia shilingi milioni moja kila mtu. Wengine kwenye picha ni Meneja wa Sheria wa benki hiyo, David Sarakikya (kushoto), Mtaalamu wa Mfumo wa Habari na Mawasiliano wa FNB, Bi. Ilakiza Hezwa na Mkaguzi Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemed (kulia).

Mkaguzi Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemed (kulia) akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni kumi kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha wateja wa rejareja wa First National Bank, Francois Botha (kushoto) kwa niaba ya washindi kumi wa kampeni inayoendeshwa na benki hiyo kuhamasisha uwekaji akiba ili kujikwamua kiuchumi. Makabidhiano hayo yamefanyika jijini Dar es salaam leo. 
(Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog). 

 First National Bank Tanzania imetangaza washindi wa droo ya pili ya kampeni yake ya kuhamasisha uwekaji akiba. Kupitia droo iliyofanyika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es salaam leo jumla ya washindi kumi wamejishindia shilingi milioni moja kila mmoja kupitia mpango huo wa kuwahamasisha Watanzania kuwa na utamaduni wa kujiwekea akiba benki.

 Akiongea jijini Dar es salaam leo, Mkuu wa Kitengo cha wateja wa rejareja wa FNB Tanzania, Francois Botha alisema mbali na kuhamasisha uwekaji akiba, kampeni hiyo inalenga kuhimiza wananchi wote nchini ambao hawajafungua akaunti benki kujitokeza na kuweka akiba. Kupitia droo hiyo ya pili, shilingi milioni kumi imetolewa kwa jumla ya washindi kumi ambao ni Gabriel Mrosso wa Mwanza, Agnes Mndasha wa Dar es salaam, Ebenezer Moshi wa Mwanza, Amiri Mziray wa Dar es salaam, Nelis Kashanga wa Mwanza, Festo Msofe wa Dar es salaam, Daniel Kakesyo wa Mwanza, Boniface Likingo wa Dar es salaam, Michael Lusana wa Mwanza, Benedicto Makoye wa Dar es salaam.

 Botha aliwapongeza washindi hao na kuongeza kwamba benki hiyo inaendelea kufanya jitihada kubwa kuboresha huduma na kuongeza kwamba kampeni hii ni sehemu ya jitihada hizo zilizolenga pia kuongeza idadi ya watumiaji huduma za kibenki nchini. Kupitia kampeni hiyo inayofanyika kwa muda wa miezi mitatu, wateja wa FNB waliopo na wateja wapya wanaingizwa kwenye droo moja kwa moja kutokana na kila shilingi elfu hamsini wanayoweka akiba katika benki hiyo. 

Jumla ya washindi 30 watanufaika kupitia kampeni katika muda wa miezi mitatu. Click here to Reply or Forward 2.02 GB (13%) of 15 GB used Manage Terms - Privacy Last account activity: 21 minutes ago Details Cathbert Kajuna's profile photo Cathbert Kajuna Show details

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad