JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


TUZO YA MWAJIRI BORA 2016 YAZINDULIWA LEO JIJINI DAR.

Share This

 Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Aggrey Mlimuka akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mratibu wa Mradi wa NHO, Joyce Nangai.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Aggrey Mlimuka akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kuzindua Tuzo ya Mwajiri bora wa mwaka 2016 ambayo itakuwa ikihamasisha na kuendeleza rasilimali watu ili kuleta maendeleo. Kulia ni Mratibu wa Mradi wa NHO, Joyce Nangai.Baadhi ya wafanyakazi na waandishi waki msikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Aggrey Mlimuka.
Picha na Avila Kakingo.

CHAMA cha waajiri Tanzania (ATE) wazindua Tuzo ya Mwajiri bora wa 2016 ambayo itakuwa ikihamasisha na kuendeleza rasilimali watu ili kuleta maendeleo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa tuzo hiyo jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waajiri Tanzania(ATE), Aggrey Mlimuka amesema kuwa kwa mwaka huu hafla ya tuzo hiyo itafanyika Desemba.

Mlimuka amesema kuwa lengo la tuzo hiyo ni kutambua wanachama wenye sera nzuri za usimamizi wa rasilimali watu katika taasisi na makampuni mbalimbali mwanachama hapa nchini.

Amesema kuwa tuzo hiyo itafuata mbinu za Kisayansi na kitaalamu ili kuangalia umuhimu wa Rasilimali watu katika makampuni ya Kibiashara makubwa na madogo na yale ya kati ili kuinua ujuzi wa wafanyakazi wanaofanya kazi kwa kujituma sehemu zao za kazi.

Amesema tukio lakutafuta msihindi wa tunzo hiyo limegawanyika katika makundi mawili ambapo wataanza kufanya utafiti kwa kutumia Mshauri mwelekezi pamoja na kuwa na hafla ya tuzo itakayo fanyika Desemba mwaka huu.

Amesema kuwa kwa tunzo ya mwajiri bora mwaka huu wataangalia kipengele cha ushirikishaji wa watu wenye ulemavu pamoja na hali ya kujali wafanyakazi katika sehemu za kazi.

Mlimuka amesema kuwa tuzo hio pia itajikita zaidi katika kuangalia maeneo muhimu ya rasilimali watu, uongozi,utawala, usimamizi wa Rasilimali watu, kusaidia jamii pamoja na kuwajibika katika jamii, ubora na uzalishaji, amesema kuwa wanachama ashiriki kujaza kwa mkono dodoso kwaajili ya kushiriki.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad