JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MPINGA CUP 2016 UWANJA WA KITUNDA SHULE KUNDI C

Share This

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Eric Ndidi akitoa  mipira kwa timu za kundi C zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kitunda Shule ya Msingi siku za Jumamosi na Jumapili, Lengo la Mashindano haya ni kutoa Elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Pikipiki ususani waendesha Boda Boda katika mkoa wa Dar es Salaam
 Polisi Konsitebo wa Kikosi cha Usalama Barabarani Makao Makuu, Sharifa Ismaili akikabidhi mipira kwa moja ya timu zilizofanikiwa kuibuka na ushindi kwenye michezo ya MPINGA CUP 2016, makundi raundi ya kwanza kutoka kundi C iliyofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kitunda, Lengo la Mashindano haya ni kutoa Elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Pikipiki ususani waendesha Boda Boda katika mkoa wa Dar es Salaam.
Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Eric Ndidi akifundisha kuzijua Alama za Barabarani kwa wachezaji wa  timu za kundi C kabla ya kuingia uwanjani kwenye Uwanja wa Kitunda Shule ya Msingi siku za Jumamosi na Jumapili, Lengo la Mashindano haya ni kutoa Elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Pikipiki ususani waendesha Boda Boda katika mkoa wa Dar es Salaam. 
  Staff Sajent wa Polisi, Enock Machunde akifundisha jambo kwa madereva wa Boda boda wakati wa michezo ya Mashindano ya MPINGA CUP 2016 kundi C zilizofanyika kwenye Uwanja wa Kitunda Shule ya Msingi siku za Jumamosi na Jumapili, Lengo la Mashindano haya ni kutoa Elimu ya Usalama Barabarani kwa madereva wa Pikipiki ususani waendesha Boda Boda katika mkoa wa Dar es Salaam.
 (Picha na Traffic Makao Makuu).

Na: Traffic Makao Makuu.
MASHINDANO ya Kombe la MPINGA CUP 2016 hatua ya makundi inayoendelea kwenye Mkoa wa Kipolisi Ilala iliyopangwa kwenye makundi sita tayari makundi matatu yamekamilisha ratiba baada ya kupata washindi wa michezo yao ya awali kutoka kundi C, timu hizo zimechuana kuwania nafasi ya kusonga hatua ya pili baada ya jana kukamilisha ratiba hiyo na kuwa kundi la tatu kuungana na kundi A na B ambayo michezo yake imeshakamilika.

Mchezo wa kwanza wa kundi C ulianza majira ya saa nne asubuhi katika Uwanja wa Kitunda Shule ya Msingi ikiwa ni siku ya Jumamosi tarehe 27/8/2016 ambapo timu ya Chakenge F.C iliweza kucheza dhidi ya timu ya Mara fc ikifuatiwa na Mchezo wa pili ambao timu ya Kivule C.C.M (A) ilipata Ponint za mezani baada ya timu ya Polisi Kitunda kushindwa kutokea Uwanjani na kukabidhiwa Mpira mmoja kwa ajili ya  kujinoa kwa kinyang’anyiro cha mzunguko wa pili.

Mchezo mwingine ilikuwa ni kati ya timu ya Mwembeni Fc Kivule iliyoshindwa kutumia vyema nafasi walizopata kipindi cha kwanza ambapo waliambulia kupata goli 1 dhidi ya wenzao wa Amani fc wakati timu ya Matembele Kivule walishinda kwa kupata magoli mawili (2) katika mchezo wa tatu huku mchezo wan ne (4) Njia Panda Msikitini fc Kitunda ilitolewa kwenye mashindano na timu ya Relini Kitunda iliyoibugiza kwa jumla ya mabao 3-2 na kuzawadiwa mpira ili wakajiweke vema na mzunguko wa pili.

Mwendelezo wa Mashindano haya ya MPINGA CUP 2016, ilifuata siku ya 28/8/2016 Siku ya Jumapili na michezo iliyochezwa ilikuwa ni mitano (5) ikiwa na jumla ya timu kumi zilizokutana kwenye kutafuta nafasi ya kusonga mbele hatua ya kwanza mtoano, Katika Mchezo huo mgumu kwa timu zote mbili, Matembele fc (KIPUNGUNI) dhidi ya timu ya Pentagini Fc ambapo mshindi alikuwa ni Matembele Kipunguni kwa njia ya Penalt -4-3 na kuzawadiwa mpira kwa ajili ya kwenda kujiandaa na mchuano wa dulu la pili.

Mchezo mwingine ulizikutanisha timu za Kitunda fc Kivule iliyocheza na timu ya Mwembeni fc  Kivule na timu ya kitunda Fc ilifanikiwa kuibuka na Ushindi wa mnono wa mabao 3-1 dhidi ya wenzao wa Mwembeni Fc na kuzawadiwa Mpira moja kwa ajili ya kwenda kujiandaa na raundi inayofuata.

Na mchezo wa Tatu uliokuwa na mshikemshike mkubwa dhidi ya timu zote kwa Mashabiki wao, Timu ya MACHIMBO F.C walifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya MUSOMA BUCHA F.C MACHIMBO ambayo hata hivyo mchezo huo ulimalizika kila timu ikiwa na mashike mshike mkubwa na ulikuwa ni mchezo wa kusisimua kutokana na ulivyochezwa kwa ufundi mkubwa na wachezaji wa timu zote mbili hata ivyo mshindi alizawadiwa mpira kwa lengo la kwenda kufanya maandalizi mazuri ya mzunguko wa pili.

Michezo yote hiyo iliongzwa na Mafunzo Muhimu kwa Walimu wa Masuala ya Elimu ya Usalama Barabarani ambao walitoa Mafunzo hayo kwa timu zote kabla ya kuingia uwanjani huku wakifundidishwa pia Alama za Barabarani na Kuulizwa Maswali na Washindi mbali mbali walizawadiwa Furana kutoka kwa wadhamini Mbali Mbali wa Mashindano haya ya MPINGA CUP 2016 yanayofanyika kwenye Mkoa wa Kipolisi ILALA.

Ambapo timu ya Kitunda Sabato Fc ilifanikiwa kuifunga timu ya Kipunguni Relini kwa jumla ya mabao 2-0 katika mchezo ambao ulikuwa wa Upande mmoja huku wachezaji wa timu ya Kipunguni Relini wakisingizia Uwanja kuwa na Michanga wakilinganisha na Beach Soccer, pamoja na yote lakini hatimaye washindi walipatikana na kufnikiwa kijipatia zawadi ya mpira mmoja kila timu iliyoibuka Kidedea.

Mchezo wa Mwisho Timu ya Kivule Silali ilipepetana na timu ya Nyantila fc, timu mbili ambazo ni wapinzani wa jadi walijikuta wakimaliza dakika 90 kwa kutoshana nguvu baada ya kumaliza wakiwa wamefungana bao moja kwa moja 1-1. Lakini hata hivyo kutokana na Sheria ya Mashindano mshindi ni lazima apatikane, walikwenda kwenye mikwaju ya Penalti na mshindi kuwa timu ya Nyantila Fc waliopata mikwaju ya Penali nne (4) huku wenzao wa timu ya Kivule Silali wakiambulia kupata mikwaju miwili (2) ya Penalti na hivyo kumaliza Kundi hilo na Sasa Mashindano Haya ya MPINGA CUP 2016 yatafanyika Kiwalani wiki hii kama ratiba inavyoonyesha.

RATIBA YA MASHINDANO YA BODABODA KUNDI D:
Uwanja ni Chuo cha Walemavu Kiwalani Tarehe 3/9/2016.

1. Mafundi Fc Vs PANDA KIWALANI F.C
2. BOMBOM F.C vs KIJIWE SAMLI KIWALANI
3. YOMBO HOSPT.KIWALANI vs MORNING STAR KIWALANI
4. KIPAWA FC vs KIPAWA SHELI FC
5. VINGUNGUTI SCANIA vs KIZOTA F.C VINGUNGUTI
6. MORNING STAR F.C vs WASHAWASHA F.C
7. KIWALANI BEACH F.C vs BODABODA GARDEN

KAtika UWanja huo huo tarehe 4/9/2016
1. VINGUNGUTI RELINI vs MAZIZI F.C
2. MTI PESA vs MASHUJAA F.C
3. TABATA DARAJANI F.C vs BALAKUDA HIGHLAND FC
4. GOGOVIVU F.C vs BODABODA F.C
5. MANDEZE F.C vs YOMBORELI F.C
6. VIPAJI FC vs GOLAN F.C

Inavyoonekana kwenye kundi hili kutakuwa na ushindani mkubwa sana kutokana na timu nyingi kujitokeza kujiandikisha kutoka maeneo ya kundi D, ambapo jumla ya 14 zitacheza siku hiyo ya jumamosi na siku inayofuata jumla ya timu 12 zitacheza na kupata washindi pekee watakaosonga mbele hatua inayofuata ya mashindano haya a kusisimua na yenye mafunzo mazuri kwa madereva wa Boda boda.


Wadhamini mbali mbali wamejitokeza kudhamini na kuweza kufanikisha michezo hii kuwa ya aina yake mwaka huu ikiwa ni pamoja na Udhamini Wa G.S.M wauzaji wa Piki waliotoa zawadi ya Pikipiki kwa Mshindi, Cool Blue Tanzania ambao kwa hakika wameonyesha Sapoti nzuri kwa kutuhakikishia Maji kwa wachezaji wakati wote wa michezo sambamba na kampuni ya Coca Cola,Big Bon, NMB, Zantel, Haki Elimu, Star Times, Windhoek, Red Bull, NHIF, PUMA, Yono, Dar City Promotions, TBL, Milcom, E.F.M Radio, T-Marc Tanzania, Michuzi Blogs, Mwananchi Communications, Dira Tv, My Way Entertainment, Mashujaa Band, MpaluleBlogs: Miss Demokrasia Tanzania, Balozi wa Demokrasia Tanzania, na Jeshi la Polisi Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad