Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
JESHI
la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kukamata
watuhumiwa 1,065 kwa makosa mbalimbali yakiwemo makosa ya unyang’anyi
kwa kutumia nguvu.
Watuhumiwa
hao ni wapiga debe katika sehemu mbalimbali za vituo vya daladala,
watengenezaji pombe haramu ya Gongo waliokamatwa na lita 952 ikiwemo na
mitambo mitatu ya kutengezea pombe hiyo, Kikosi cha mbwa mwitu 10,
wauzaji na wavutaji bhangi puli 277, Kete 210, misokoto 144, pamoja na
wacheza kamari.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda
Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Polisi Kanda Maalum, Simon Sirro
amesema kuwa watuhumiwa 1,065 walikamatwa katika operesheni inayofanywa
na jeshi hilo.
Amesema
katika operesheni Julai 21 wameweza kufanikiwa kupata silaha aina ya
gobore yenye namba za usajili HD 201-2014 kutoka kwa watuhumiwa
wanaotumia silaha katika matukio ya uhalifu iliyotelekezwa na watu
wasiofahamika baada ya raia wema kuhisi kuna mtu anamiliki silaha na
msako ukaendelea.
Aidha
amesema mnamo Juni 16 hadi 19 Polisi wamemkamata lita 952 za Gongo
katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam kati ya lita hizo 420
zilikamatwa katika maeneo ya Kinzudi Wazo Hill kutoka kwa watu sita,
mitambo mitatu ya kutengeneza pombe haramu ya Gongo pamoja na kukamata
sukari kilo 100.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro akionesha waandishi wa habari vitu mbalimbali leo jijini Dar es Salaam
Kamanda
wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro akionesha simu
zilizoibwa na majambazi mbalimbali jijini Dar es Salaam waandishi wa
habari.
Kamanda
wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro akizungumza na
waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam, juu ya
operesheni walioifanya na kufanikiwa kukamata watuhumiwa sugu 1,065 wa
makossa mbalimbali jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massa,Globu ya jamii).
No comments:
Post a Comment