JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


WATUHUMIWA 1,065 WAKAMATWA KATIKA OPERESHENI JIJINI DAR ES SALAAM.

Share This
 Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kukamata watuhumiwa 1,065 kwa makosa mbalimbali yakiwemo makosa ya unyang’anyi kwa kutumia nguvu.

Watuhumiwa hao  ni wapiga debe katika sehemu mbalimbali za vituo vya daladala, watengenezaji pombe haramu ya Gongo waliokamatwa na lita 952 ikiwemo na mitambo mitatu ya kutengezea pombe hiyo, Kikosi cha mbwa mwitu 10, wauzaji na wavutaji bhangi puli 277, Kete 210, misokoto 144, pamoja na  wacheza kamari.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Polisi Kanda Maalum, Simon Sirro amesema kuwa watuhumiwa 1,065 walikamatwa katika operesheni inayofanywa na jeshi hilo.

Amesema katika operesheni Julai  21 wameweza kufanikiwa kupata silaha aina ya gobore yenye namba za usajili HD 201-2014 kutoka kwa watuhumiwa wanaotumia silaha katika matukio ya uhalifu iliyotelekezwa na watu wasiofahamika baada ya raia wema kuhisi kuna mtu anamiliki silaha na msako ukaendelea.

 Aidha amesema mnamo Juni 16 hadi 19  Polisi wamemkamata lita 952 za Gongo katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam kati ya lita hizo 420 zilikamatwa katika maeneo ya Kinzudi Wazo Hill kutoka kwa watu sita, mitambo mitatu ya kutengeneza pombe haramu ya Gongo pamoja na kukamata sukari kilo 100.

 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro akionesha  waandishi wa habari  vitu mbalimbali leo jijini Dar es Salaam

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro akionesha simu zilizoibwa na majambazi mbalimbali jijini Dar es Salaam waandishi wa habari.
 
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro  akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam, juu ya  operesheni walioifanya na kufanikiwa kukamata watuhumiwa sugu 1,065 wa makossa mbalimbali  jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel Massa,Globu ya jamii).

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad